Sunday, September 29, 2013

PROF MBARAWA NA MKONGO WA TAIFA





MUSOMA.

WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa, amewataka wananchi wa Mkoa wa Mara, kutunza Mkongo wa Taifa kwani una manufaa makubwa kwa uchumi wa Taifa hili.

Ilikuwa ni siku ya kukamilisha ziara yake ya siku moj akatika Mkoa wa Mara,Wilayani Tarime mji wa  Sirari mara baada ya kumaliza kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mkongo huo na changamoto zinazoukabili.

Alisema Mkongo wa Taifa una manufaa makubwa kwa uchumi wa Taifa hili kwa kuwapatia  mawasiliano wananchi wake, ambapo Mikoa ya Tanga na Arusha ina watumiaji wengi na  Mkoa wa Mara bado haujawa na watumiaji wengi, ambapo pia kuna changamoto mbalimbali zinazoukabili ikiwa ni pamoja na maporoko upande wa  Arusha ambapo udongo umekuwa ukiingia kwenye miundo mbinu ya Mkongo huo.

Aliwahadharisha wananchi kuwa nyaya za Mkongo huo zina madhara makubwa kwa kuwa zimetengezwa kwa kioo maalumu, hivyo unaweza kuharibu Mkongo huo, huku ukiambulia upofu, kwani nyaya zake ni hatari sana ziiingiapo kwenye jicho.

“Ni kosa kubwa kuhujumu miundo mbinu, wananchi waelewe kuwa miundo mbinu hii ni kwa ajili ya manufaa yao na Taifa kwa ujumla,pia hakuna shaba katika mkongo huu, ambayo  wahujumu wanafikiri kuwa ipo, ila nyaya zake ni nyuzi laini kama unywele  ambapo waya huo ni hatari sana kwani unaweze kukutia upofu” Alisema Mbarawa.

Akizungumza na wafanyakazi  wa Kammpuni ya Simu ya Tanzania ( TTCL), Mkoa wa Mara na Posta, katika ofisi zake zilizopo mkabala na uwanja wa Michezo wa Karume, alisema kuwa wafanyazi hao  wana thamana kubwa ya kuutunza  kwani ndio waliokabidhiwa jukumu hilo.

“TTCL yaani nyie mmepewa jukumu la kuuendeleza mkongo kwa maana ya kuusambaza nchi nzima kwa niaba ya Serikali ili kuleta ubora wa huduma kwa gharama nafuu, usalama wa nchi, watu na mali zao” Alisema Mbarawa.
Alisema kuwa Serikali inataka kufanya ubia  kati ya Bat Airtel ya India na TTCL ambapo Bat Airtel yuko tayari kuachia hisa zote kwa Kampuni ya TTCL na kwamba kwa sasa kila kampuni iko kwenye mchakato wa kutathimini hisa zake na kwamba tayari Bat Airtel wamekamilisha.

Kwa upande wa Shirika la Posta nchini aliwataka wafanyakazi kuwa wabunufu kwani teknolojia zinabadilika na kwamba Wizara itaaendelea kushirikina na  Shirika hilo hili liweze kukua kwani lisiposaidiwea linaweza kupotea.

Alizitaka taasisi zote za Serikali kutumia huduma ya  shirika hili kwa kutuma vifurushi vyote kwa njia ya posta kwani kuna baadhi ya Taasisi za Serikali zimeacha kutumia Shirika hilo, na hivyo kusababisha kukosa mapato.

Kuhusu nyongeza ya Mishahara ambayo watumishi wa Posta walimlilia Waziri aliwataka kutuma maombi yao kwa bodi, ambayo ndiyo yenye thamana ya kufikia maombi yao hazina na hazina ikashughulikia hivyo ana imani kuwa nyonyeza ya mshahara inawezekana kwani  Serikali yao ni sikivu.