Thursday, December 6, 2012

MAHAFALI YA KWANZA MTWARA (STEMMUCO)




Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga akiteta jambo na Mhashamu Baba Askofu MKUU wa Chuo Kikuu cha Stella Maris( STEMMUCO) Norbet Mtega, mara baada ya kumaliza hotuba yake katika mahafali ya kwanza ya Chuo hicho.

MWENYEKITI wa Bodi ya Chuo  Kikuu kishiriki  cha Stella Maris,Tawi la Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (STEMMUCO),Mhashamu, Gabriel Mmole ameipongeza Serikali kupitia bodi ya mikopo  kwa kutoa mikopo kwa wanafunzi wa Chuo hicho.


Aliyasema  hayo  juzi  katika mahafali ya kwanza ya Chuo hicho ya kuhitimu Shahada ya kwanza ya Sanaa/ualimu (Bachelor of Art with Education) wakati akimkaribisha mgeni rasmi kufungua mahafali hayo yaliyofanyika katika viwanja wa Chuo Mjini Mtwara.


Alisema anaishukuru Serikali kwani bila wao pasingekuwepo na mafanikio yoyote ya Chuo kwani ukubaliwa wao wa kutoa mikopo kwa Chuo hicho ndio umesababisha mafanikio katika kufanikisha wanachuo  kumaliza masomo yao vyema.

“Natoa pongezi za dhati kwa serikali ya awamu ya nne ambayo imetuwezesha kutoa mikopo kwa wanafunzi wetu bila kubagua itikadi za dini ukizingatia kuwa sisi ni taasisi ya dini,bila wao tusingefanikiwa”. Alisema Mhashamu Baba Askofu Mmole.

Akifungua Mahafali hayo ya kwanza ambayo yalianza kwa maandamano, Naibu Waziri wa Kazi na Ajira  Makongoro Mahanga alisema  ukosefu wa ajira kwa vijana walio wengi unatokana na baadhi ya wahitimu wa Vyuo Vikuu kutotaka ama kutoweza kuchukua masomo ya Sayansi na hisabati, pia fani ya ualimu ambazo zina fursa ya ajira.

Alisema kuwa tatizo la wahitimu wa Vyuo Vikuu kurudisha mikopo waliokopeshwa bado ni kubwa, ambapo kufikia Juni 2012, madeni ya wahitimu wa Vyuo Vikuu yakiyokuwa yameiva yalikuwa Bilioni 160.7 na kati yake, Sh Bilioni 39.5 zilitakiwa ziwe zimeishakusanywa kutoka kwa waliokopa lakini asilimia 49 tu kati ya hizo zilikuwa zimekusanywa na bodi ya mikopo ya wanafunzi.

Aidha ametoa wito kwa Vyuo vya elimu ya juu kurekebisha kasoro zilizopo kwa kutilia maanani masomo ya Hisabati na Sayansi na kuhakikisha kila fani au program katika vyuo vikuu vyote kunakuwepo na masomo ya ujasilimali (Bachelor of Business Administration/Management in Entrepreneurship)  ili kuwaandaa  wahitimu kujiajiri kama hawatapata kazi za kuajiriwa.

Alitoa wito kwa wahitimu kuwa tayari kufanya kazi popote bila kubagua maeneo kama kama wengi wao wanavyopenda Mijini.


Katika awamu ya nne ya Serikali kutoka mwaka 2005/2006-2011/2012, Serikali kupitia Bodi ya Mikopo Iliyoundwa mwaka 2005, ilikopesha wanafunzi 480,472 jumla ya Sh. Trioni  1,133,386,869,000 ambapo Chuo hicho kimefaidika n amikopo hiyo ambapo asilimia 94 ya wahitimu,pia imetoa ekari 140 kwa ajili ya mendeleo ya Chuo hicho,ambapo jumla ya wahitimu (kifungua mimba) wapatao 1,100 wamehitimu.

Naye Mhitimu katika Chuo hicho, Wini Israel Musiba aliishukuru Serikali kwa kutoa mikopo hiyo  na kwamba inajali familia duni  si kama awali ambapo jamii ilidhani mikopo ni kwa  watoto wa wakubwa peke yao,pia alitoa wito kwa Serikali kuweka miundo mbinu ya barabara na Umeme ili walimu wafanya kazi zao kwa umakini zaidi  kwa kuzingatia masomo ya sayansi yanayohitaji maabara zenye Umeme hasa vijijini.

No comments:

Post a Comment