Friday, December 7, 2012

KIJIJI CHA NANGURUKURU-KILWA MASOKO WALILIA ZAHANATI




KILWA MASOKO.

WAKAZI  wa kijiji cha Nangurukuru,kata ya Kisingino,Wilaya ya Kilwa wameiomba Serikali kukamilisha zahanati ya Kijiji hicho ili waondokane na hadha ya kutembea umbali  mrefu kutafuta huduma hiyo muhimu.

Katibu wa Ujenzi wa Zahanati hiyo,Rashid Changa alisema kuwa ujenzi wa zahanati hiyo ulianza mwaka 2007, na mpaka sasa iko katika hatua za mwisho za upigaji bati  na baada ya hapo Serikali inapaswa kukamilisha ujenzi huo.

Jiwe la Msingi la Zahanati hiyo liliwekwa na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Utawala Bora George Mkuchika ,Machi 25 2011 ambapo ilitolewa ahadi ya kuchangia kukamilisha ujenzi huo kiasi cha Sh.Milioni 40,kutoka kwa Daktari wa Wilaya,Mike Mabimbi kwa ajili ya kumalizia jengo hilo.

Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Nangurukuru,Shaibu Mmula alisema kuwa zahanati hiyo kwa sasa imeanza kuweka nyufa kutoka na kukaa kwa muda mrefu na hivyo inaweza kuigharimu  serikali pamoja na wananchi fedha nyingi za ujenzi mpya endapo itabomoka.
Alisema kuwa wananchi wamechangia nguvu zao kiasi cha Sh. Milioni 34 na Halmashauri kupitia mfuko wa jimbo imechangia Sh Milioni 1.5 .

Kwa upande wa Chama cha Mapinduzi  (CCM) kuhusu idadi na ongezeko la wanachama ni hafifu kutokana na changamoto zinazoikabili Wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na zahanati,soko na stend, huduma ya maji.

Aidha Katibu Mwenezi wa tawi la Nangurukuru,Said matale alisema endapo changamoto hizo zitapata utatuzi,hakuna chama  chochote kinaweza kushinda uchaguzi Mkuu 2015 na ametoa wito kwa Serikali kuangalia uwezekano wa kuchimbiwa malambo hasa katika maeneo ya Kwakumtoni, Karasha, Dodomezi na Lingaula.

Aliongeza pia kuwa kumekuwa na unyanyasaji kwa upande wa wavuvi kubaguliwa kiitikadi na kwamba kama wewe si mwanachama wa Chama cha CUF uwezi  kuvua samaki katika Bahari,hiyo ambapo tatizo hilo linaonekana kuwa sugu kwa upange wa Kilwa Kivinje.

No comments:

Post a Comment