Sunday, December 9, 2012
MIAKA 51 YA UHURU YAFANA NA HALAIKI YA AINA YAKE
MIAKA 51 YA UHURU.
DAR ES SALAAM.
RAIS Jakaya Kikwete kwa mara ya kwanza leo katika maadhimisho ya Miaka 51 ya Uhuru amevunja rekodi ya kuhutubia kwani hotuba hiyo huwa inafanyika baada ya miaka mitano,ametoa hotuba ya kutambulisha viongozi wenzake wa nchi wanachama wa Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)na kusema asiye na macho aambiwi tazama,asiye an
masikio aambiwi asikie.Rais Kikwete ameamua kutoa hotuba hiyo kwa ajili ya kuwatambulisha wageni kwa lugha ya Kiswahili na kusema kwa lugha ya Kiingereza kuwa kama hawafahamu Kiswahili watafuraia kwa kusikia majina yao na watainuka kwa kuwapungia mkono watanzania.
“Leo tuna bahati kubwa kwa kuwa tuna viongozi wa Nchi za kusini mwa Afrika SADC,wageni 12 tu wamepata fursa ya kuja kuona maadhimisho haya ya Miaka 51 ya Uhuru na kwa kuwa ratiba ya ndege inawalazimu kuondoka inanipasa niwatambulishe kwenu na niwakaribishe.
Ametoa pongezi kwao kwani wameifanya sherehe ya Miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika kuwa njema kwake kutokana na kwamba hotuba hiyo ndiyo ya mwisho kwake kwani hatatoa hotuba tena,kwani hotuba hiyo anapaswa kutoa Rais mwingine wa 2015.
Alitoa fursa kwa Rais wa Namibia kutoa salamu zake kwani siku hii na yake kwani siku nchi yetu inapata Uhuru ndiyo siku alikuja Tanzania kutoka Namibia kuja kujipanga kuhusu ukurasa mpya wa kupata ukombozi wa Msumbiji ambapo Tanzania imetoa mchango mkubwa kwa nchi yake kupata Uhuru.
Marais waliokuwepo ni pamoja na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Armando Guebuza,Rais wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila,Rais wa Namibia,Ifikepunye ,Waziri Mkuu wa Lesotho na wengine.
Alisema yeye ana uhusiano maalumu na Tanzania kwani wakati Nchi yetu inapata Uhuru 9 Disemba 1961,ndiyo siku aliyokua Tanzania na alikimbia makaburi huku Namibia na kuja hapa kujipanga kuanza vita ya Ukombozi nchini kwake na kuja Tanzania kujipanga kwa ajira ya kuikomboa
Rais wa Namibia alitoa pongezi kwa watanzania kwa maendeleo ambayo imeyapata na kusema kuwa wakati nchi yetu inapata Uhurundiyo siku alifika nchini hapa,na baada ya kuondoka Dar es Salaam alikwenda Mjini Dodoma ambapo alikuwa na Hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere.
Sherehe hizo zilipambwa na gwaride la halaiki, ambapo mwaka huu lilikuwa la aina yake huku likifunua vitabu ,zoezi ambalo ni staili ya China,ngoma kutoka Ukerewe ambapo watoto wa Umri wa miaka mitatu walikoga nyoyo za Marais wa nchi nyingine na watanzania ,ngoma nyingine kutoka Dodoma,Zanzibar Msondo Ngoma na TMK.
Kauli mbiu ya Maadhimisho hayo ya mwaka huu ni uwajibikaji,Uadilifu na Uzalendo ni nguzo ya maendeleo.
Pamoja na kupewa kadi za mialiko,viongozi wa vyama vya siasa,baadhi yao hawakuhudhuria sherehe hizo,akiwemo, Dk Wilbroad Slaa,Zitto Kabwe,Prof Ibrahimu Lipumba,waliokuwepo ni Mh.John Cheyo,Dk.Bhatt Mtamwega Mgaywa.
Uenda walituma wawakilishi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment