Monday, December 17, 2012
UCHUNGU WA MWANA AUJAE MZAZI HASA MWANAMKE
Usemi wa uchungu wa mwana aujuae mzazi unajitokeza hapa kwa mara nyingine hasa kwa mwanamke ambaye kila wakati amekuwa akiangaika huku na kule klutafuta riziki huku akiwa hana msaada wowote kutoka kwa mumewe.
hali hii inajitokeza kutokana na kwamba mwanamke anakuwa mwangaikaji wa kutafuta riziki tangu mwanae akiwa tumboni mpaka mwisho wa maisha yake (kifo), hii mpaka lini?
Kitendo cha Mama Bhoke Nyasenso, kunywa sumu baada ya kugundua wanae wamekufa kwa kukosa hewa wakati masikini Mama wa Watu akiangaika kuandaa chakula cha kesho kwa wanae wapendwa hao watatu MUNGU awapumzishe AMEN!
Mama Bhoke kwa uchungu wa kutunga Mimba Miezi tisa,kujifungua na kuhangaika kuwasomesha anaambulia sifuri kana kwamba ndo anaanza maisha.
Serikali naomba kwa roho ya huruma ingalie jambo hili na Mama huyo asichukuliwe hatua zozote kwani inatia huruma na inachanga akili sana,hata kama ingekuwa ni wewe najua ungefanya hivyo.
Aiha elimu juu ya mazingira na madhara ya Mkaa inapaswa kutolewa kaunzia shule za Msingi ili watoto waweze kujua madhara yake,laiti wangekuwa na Elimu hiyo,pia Kifo hicho cha kusitisha kisingewakuta kwani wangemweleza Mama yao ambaye hana Elimu yoyote kuhusu madhara ya Mkaa.
Hii ni mara ya pili tangu mwaka huu uanze kwa watoto kufia ndani kwa matukio m balimbali likwemo la moto ambao pia waliwasha mkaa na kuendelea kupika na wakaenda kulala, ili tukio lilikuwa maeneo ya Kamunyonge Mjini Musoma,ambapo si kijijini, hawa pia hawakuwa na elimu hii ya kwamba kuwasha mkaa na ukauacha ndani ya chumba unakosa hewa, ili ni somo la (Sayansi).
Watoto waliokufa ambao ni wanafunzi shule ya Msingi Nyangoto ni Naomi(14) wa darasa la VII,Magreth(10) wa darasa la IV, na Debora Nyasenso(6) wa darasa la I.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime na Rorya,Justus Kamugisha alidhibitisha tukio hilo.
Tukio la kifo cha watoto hao lilitokea Jumamosi Alfajiri,Dec.15 katika kijiji cha Nyangoto, Nyamongo, tarafa ya Ingwe,Wilaya ya Tarime.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment