Tuesday, December 18, 2012
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ZIARANI MKOANI WA MARA
WAZIRI wa Nishati na Madini,Profesa Sospeter Muhongo, kesho ataanza ziara ya kikazi Mkoa wa Mara.
Kwa Mujibu wa taarifa za uhakika kutoka ofisini kwake,Hii ni mara ya pili kufanya ziara Mkoano humo, kutokana na kwamba Waziri huyo amezaliwa Mkoa wa huo, katika Hospitali ya Serikali ya Musoma na amesoma Shule ya Msingi, Nanaxchand iliyokuwa ya Wahindi,ambapo walisoma watoto wenye vipaji na maarufu Musoma,sasa (Iringo)ni shule pia aliyosoma Mwl. Pearl Lucas Thomas Musiba,Binti pekee wa Mwasisi wa TANU na Mwenyekiti wa Halmashauri,NDUGU LUCAS THOMAS MUSIBA aliyetumikia Taifa kwa mihula miwili miaka 10 hadi kifo kilipomchukua, moja ya shule tano zilizoko katika kitovu cha mji wa Musoma.
Waziri Muhungo ana familia yake ambayo iko Mtaa wa Mwigobero ambapo kwa sasa kuna kivuko kipya cha Serikali ambapo kinafanya safari zake,kutoka Mjini Musoma na Wilaya ya Rorya.
Ziara yake ya kwanza, Waziri Muhongo ambaye hakutaka kuambatana na waaandishi wa habari
alitembea wachimbaji wadogo wadogo katika vijiji vya Seka na Suguti,Musoma vijijini, Wilaya ya BUTIAMA.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo Waziri wa Nishati na Madini atekwenda Wilaya ya Serengeti na Musoma.
kwa sasa nguzo za Umeme tayari zimetandazwa katika vijiji vya Bwai Paris,ambako ndo nyumbani kwa wazazi wa Profesa huyo.
Baadhi ya wakazi wa Majita(Tarafa ya Nyanja),wamemtaka Waziri huyo asiishie hapo bali afanye utandazaji wa nguzo hizo maeneo ya vijiji vyote.
"Hatukatai kuwa nyumbani kwanza,lakini asambaze nguzo hizo na kuhakikisha Umeme unawaka Vijijini,hii itasaidia vijana wengi wanaokimbilia mijini kwa kufuata huduma hiyo hasa jiji la Dar es Salaam, Mwanza na Arusha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment