MUSOMA
MBUNGE wa Jimbo la Musoma Mjini, Vicent Nyerere,(CHADEMA)
amewadanganya wanachi wa Jimbo lake kuwa Ikulu ndogo inadaiwa Sh. Bilioni 1, za gharama za maji huku Mamlaka ya Maji safi na taka (MUWASA) ikikanusha vikali kauli
hiyo ya Mbunge na kudai kuwa gharama hizo ndiyo bajeti ya Mamlaka yao.
Mbunge huyo ambaye pia ni Mjumbe wa bodi ya Maji hivi
karibuni katika Mkutano wa hadhara uliofanyika hivi karibuni katika viwanja wa Shule
ya Sekondari ya Mara alitamka kuwa Ikulu ndogo inadaiwa Bilioni 1 ambazo gharama
hizo wananchi ndio wanaozilipa.
Akikanusha kauli hiyo wakatia kizungumza na waandishi wa
habari, Kaimu Meneja wa Mamlaka ya maji safi na taka Musoma ( MUWASA), Emmanuel
Ruyobya alisema kuwa siyo kweli kwamba Ikulu ndogo inadaiwa fedha hizo.
Alisema kuwa Taasisi zinazodaiwa ni Hospitali M.40, Polisi
M. 96,Shule za Msingi M.8 jeshi kwa maana ya watumishi na nyuma zo ni Sh. M1.2
na RAS Mara kwa maana ofisi pamoja na Ikulu ndogo ni Sh. M. 10 si Bilioni 1
kama ambavyo Mbunge huyo alidai.
Alisema kuwa MUWASA inaendelea na shughuli zake za maendeleo
ikiwa ni pamoja na kuunga wateja wapya kulingana na miundo mbinu iliyopo,pia
imepata mkandarasi wa kuweza kujenga mradi mkubwa wa Maji eneo la Bukanga, Makoko utakaogharimu kiasi
cha Sh. Bilioni 41 na utakamilika mwaka 2014.
Mradi huo utakapokamilika utatoa huduma zaidi ya asilimia 95
ya wakazi wa Musoma kwa kuzalisha mita za ujazo 36,000 kwa siku ikilinganishwa
na mahitaji ya mita za uajzo 24,000 za sasa.
Alisema kuwa kutokana na kukatatika kwa mabomba,mafundi
wanafanya jitihada ili kurejesha huduma hiyoa mbapo leo baadhi ya maeneo
yataanza kupata maji.
No comments:
Post a Comment