Tuesday, October 15, 2013

WANARIADHA WAMUENZI NYERERE



BUTIAMA

CHAMA cha riadha Mkoa wa Mara, Oktoba 14 mwaka huu, kilimuenzi Baba wa Taifa,Hayati Mwl.J.K Nyerere kwa kufanya mbio ya Kilometa 21 na ushindi kupatiwa zawadi.

Akizungumza mara baada ya Mashindano hayo, Kamishina wa habari na uenezi  wa Chama chama cha riadha Mkoa wa Mara, Eva-Sweet Musiba alisema kuwa Chama kimeamua kufanya mbio hiyo ili kuenzi mchango wa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere katika nchi hii kwa kuleta Uhuru, uzalendo,Amani na Utulivu katika nchi hii.

“ Tumeamua kuunga mkono jitahada za Mwalimu Nyerere alizozifanya katika nchi hii, pia kuipenda michezo,hatukutaka kuwa nyuma kwa michezo ingawaje yeye alikuwa anapenda mchezo wa bao, lakiji sisi tumeamua kufanya hivyo ili kumkumbuka Baba yetu ambaye alikuwa msitari wa mbele katika michezo yote” Alisema Musiba.

Pia alitoa shukurani kwa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara Barrick kwa kuchangia gharama za mashindano hayo na kuwataka wawekezaji wengine, mashirika  ya umma, watu binafsi na Serikali kuunga mkono jitihada za wawekezaji  ili kukuza mchezo huo ambao ndio pekee unalitangaza Taifa hilo kwa wachezaji kuwakilisha Taifa.

Mbio hizo zilizoanza majira ya asubuhi juzi ambapo Mkuu wa wilaya ya Butiama, Angeline Mabula alizianzisha kwa kupuliza kipenga,kutoka  viwanja vya Joseph Kizurira Nyerere kuelekea barabara ya Kiabakari na kurudi.
Mbio hizo zilishirikisha wanariadha wapatao 10 kutoka wilaya za Butiama, Musoma Mjini, Rorya na Tarime ambapo washindi  wa tano bora walipatiwa zawadi zao za fedha taslimu.


Mshindi wa Kwanza Majina yao na fedha zikiwa kwenye mabano ni Mwita Kopilo kutoka Wlaya ya Tarime aliyekimbia 1:05:23 alipewa Sh. (70,000), Mshindi wa pili Juma Issa Wambura wa Tarime aliyekimbia 1:10: 03 alipata Sh. (50,0000), Mshindi wa tatu,Mukama Magesa kutoka Wilaya ya Butiama 1:13:19 alipata Sh. (30,0000) wa nne  na wa tano ,Nyakutonya Berias wa Wilaya ya Butiama 1:20:47 na Chagembe Maira  1:22:00 walipewa Sh. 25,000 ambapo Mkuu wa Wilaya Angelina Mabula alikabidhi zawadi hizo.

No comments:

Post a Comment