Friday, November 15, 2013

TEMBO WAFANYA MAUAJI-SERENGETI.

SERENGETI.


SERIKALI imetakiwa kuchukua hatua za haraka ili kukabiliana na njaa pamoja na mauaji ya watu kutokana na tembo kuvamia maeneo ya mashamba na makazi ya watu wilayani Serengeti Mkoani Mara.

Wakizungumza katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo ,madiwani hao wamesema kuwa tembo wamekuwa tishio na kero kwa wananchi wa wilaya hiyo kutokana na kuvamia makazi na mashamba mara kwa mara na kusababisha madhara makubwa kwa wananchi.


Wamesema kuwa wilaya ya Serengeti haina tabia ya kuomb achakula cha msaada lakini kutokana na uvamizi huo wa tembo wameiomba serikali kuleta chakula cha msaada kwa wale wasio na uwezo pamoja na cha bei nafuu haraka iwezekanavyo kutokana na watu kuanza kula maembe usiku na mchana ili kunusuru maisha yao.

Waliongeza kuwa serikali imekuwa ikiwachukulia hatua kali na a kisheria kwa wananchi wanaowaua wanyama hasa tembo na faru lakini wanyama hao wanapowadhuru wananchi serikali imekuwa ikaa kimya bila kujali wananchi walioadhiriwa na wanyama hao hasa kwa familia iliyoachwa yatima kutokana na wazazi/mzazi wao kuuawa na tembo.

Waliiomba Tanzania National Park(TANAPA) kusimamia kikamilifu familia zilizoadhirika hasa watoto yatima kwa kuwasomesha watoto na kuwasimamia maisha yao yote mpaka pale watakapo jitegemea wenyewe ili kuweza kufikia malengo yao ya baadae.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw.John Ng’oina alisema kuwa Wizara ya Maliasili na utalii inatakiwa kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo na sababu kubwa hasa ya kuwafanya wanyama hao tembo kutoka maeneo ya hifadhi na kuvamia mashamba ya wananchi hadi kuua wananchi ili kuthibiti hali hiyo ambayo imeendelea kuleta hofu miongoni mwa wananchi.

“Nadhani kuna tatizo ndani ya hifadhi huenda wanyama hao wanabugudhiwa ndani ya hifadhi au chakula kimepungua na ndio maana wanyama hao wanaamua kutoka ndani ya hifadhi na kutafuta sehemu nyingine ambapo wanaweza kuishi lakini wanajikuta tayari wamevamia mashamba ya watu na kusababisha njaa”alisema Mwenyekiti huyo.

Akitoa tamko la baraza mwenyekiti huyo alisema kuwa ni vema sasa maeneo yote yanayozunguka hifadhi hiyo yakawekewa uzio ili kuthibiti hali hii kutokana na madhara makubwa ya njaa na vifo kwa watu kuendelea kutokea katika Halmashauri hiyo.

Hata hiyo waliongeza kuwa zamani tembo alikuwa haonekani katika maeneo ya makazi ya watu wakati wa mchana ilikuwa ni usiku tu lakini siku hizi hata muda wa mchana saa nane tembo anaonekana na kusababisha madhara makubwa kwa binadamu na mifugo kwani tayari ngombe watatu wamekwisha uawa na tembo.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Goody Pamba kuna haja kubwa ya madiwani kwenda katika maeneo mengine yanayozungukwa na hifadhi ya wanyama kama vile maasai Mara kujifunza namna wenzetu wanavyoishi na wanyama hao bila kuleta madhara yoyote.

Diwani wa kata ya Manchira Michael Shaweshi alisema kuwa imefikia hatu tembo anaingia hadi kwenye ghala la mtu alilohifadhia mazao ya chakula mbali na kuvamia mashambani hali inayoendelea kuleta adhari kuwa wananchi ili hali walikuwa wamelima chakula cha kutosha.

No comments:

Post a Comment