Monday, December 2, 2013

Mwendesha Pikipiki afariki


MUSOMA.
Mwendesha Pikipiki maarufu kama Boda boda Ibrahim yusuph(17) mkazi wa Kamnyonge Mjini Musoma amegongana na gari uso kwa uso akiwa katika harakati za kujinasua na askari wa usalama barabarani kwa kosa la kutovaa kofia,akiwa anaivaa ambapo aliacha njia na kuifuata gari na kufa papo hapo na pikipiki kuteketea kwa moto kufuatia kulipuka kwa tanki la mafuta .

Ajali hiyo imetokea leo asubuhi majira ya saa moja, karibu na stendi kuu ya mabasi iliyoko Kata ya Bweri Manispaa ya Musoma ikihusisha gari lenye namba za usajiriT816 CLS lililokuwa likitokea makutano kuelekea mjini Musoma.

David Goodluck ni shuhuda wa ajali hiyo ambaye ni dereva wa daladala iendayo Wilayani Butiama alisema ameshangazwa na baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo badala ya kutoa msaada kwa majeruhi waliokuwa katika gari hiyo na aliyepoteza maisha ,walianza kuchangamkia samaki zilizomwagika katika mfuko na kutapakaa barabara nzima.
.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara ,SACP Ferdinand Mtui amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment