Monday, December 16, 2013

KEGONGA WAOMBA ENEO KATIKA HIFADHI YA SERENGETI


NYANUNGU-TARIME.

WAKAZI wa Kijiji cha kegonga kata ya Nyanungu Wilaya ya Tarime wameiomba hifadhi ya Taifa ya Serengeti kugawa eneo la malisho ya mifugo katika bonde hilo ili kuondoa mgogoro uliopo.

Wakizungumza na waaandishi wa habari waliokuwa na ziara katika maeneo ya bonde hilo wananchi hao wameiomba pia Serikali kuangalia upya mipaka iliyowekwa kwa ajili ya kutenga eneo la hifadhi ya mbuga ya Serengeti na eneo la kilimo na mifugo.

Hata hivyo maisha duni na uelewa mdogo wa sheria mpya kwa wakazi wa bonde hilo ndicho chanzo cha kuwepo kwa migongano kati yao na hifadhi ya Taifa ya Serengeti (Senapa).

Elimu ya ufugaji bora na kilimo inatakiwa kutolewa kwa wakazi wa bonde hilo lililoko Wilaya ya Tarime ambalo linapakana na hifadhi hiyo ili kuondokana na migogoro mbalimbali inayojitokeza katika bonde hilo.

Vile vile imeonekana kuwa Maafisa ugani hawatembelei katika maeneo hayo ili kuwasaidia wananchi juu ya kilimo na ufugaji bora wa kisasa ambao una tija kwa wananchi.

Elimu hiyo itasaidia mfumo wa maisha duni waliyonayo wakazi hao ili kwenda maisha bora kwani wana mifugo mingi ambayo wangeweza kuiuza na kubakiza mifugo michache wangeweza kusomesha watoto wao pia kujenga nyumba bora.

Naye Lucia Mariane alisema kuwa kuwa chanzo ya mgogoro huo ni eneo la kuchungia na kulima ambapo alidai kuwa kwa muda mrefu walikuwa wakilitegemea bonde hilo la Nyanungu kwa shughuli hizo, lakini kwa mujibu wa sheria bonde hilo liko ndani ya hifadhi ya Serengeti hivyo hawapaswi kuendesha shughuli zozote za kibinadamu kwa hiyo endapo watapewa mafunzo wataweza kulima na kufuga kisasa hali itakayosababisha wahitaji eneo dogo.

No comments:

Post a Comment