Wednesday, August 8, 2012

MAJITA WAPINGA MAKAO MAKUU YA WILAYA.

 MUSOMA VIJIJINI (MAJITA)

BARAZA la madiwani wa halmashauri ya Musoma limegawanyika kwa mara ya kwanza na kufanya baadhi ya madiwani kutoka nje na kususia  kikao baada ya kutofatiana kimtazamo juu ya ugawaji wa halmashauri ndani ya wilaya ya Butiama.
Tofauti hiyo ilitokea Agosti 7 wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambayo makao makuu yake bado yapo ndani ya Manispaa ya Musoma.
Baadhi ya madiwani hasa upande wa  kambi ya upinzani walikuwa wakidai kuwa wananchi wa kata ambazo zimegawanywa na kuwa halmashauri ya Musoma hawatatendewa haki endapo  watakuwa chini ya Mkuu wa wilaya ya Butiama.
Akichangia hoja hiyo diwani wa kata ya Bukima Ruti Mayamba  alisema wawo kama wawakilishi wa wananchi hawatakuwa wamewatendea haki kutoka kata za majita na Lukuba kwani watakuwa mbali na huduma za kiutawala .
Mayamba alisema huduma zitakuwa karibu endapo watakuwa chini ya mkuu wa wilaya ya Manispaa ya Musoma.
“Tunataka kata hizi kumi na saba ziungane na kata 13 za Manispaa ya Muasoma ili kutengeneza wilaya ya Musoma”,alisema Mayamba.
Kwa upande wa  madiwani  wa chama Tawala waliazimia kuwepo na halmashauri mbili ya Musoma na Butiama ndani ya wilaya ya Butiama ambazo zitakuwa chini ya Mkuu wa wilaya hiyo ya Butiama.
 
Kikao cha baraza  la madiwani ndicho kikao kilichotajiwa kutoa maamuzi ya mugawanyo huo wa hamashauri mbili zilizopo ndani ya wilaya ya Butiama ambapomapendekezo yalielekezwa kuwepo na halmashauri mbili za musoma na Butiama ambazo zitakuwa chini ya Mkuu wa wilaya ya Butiama kwa kupigwa kura.
 
Katika mgawanyo huo wa halmashauri mbili zenye jumla ya kata 34, katika  halmashauri ya Musoma kuna 17 ambazo ni  pamoja na    Nyegina,Etaro,Nyakatende,Mugango, Kiriba ,Bukumi,SugutiNyamrandirira,Nyambono,Bugwema, Murangi,Bukima,Buringa,Bwasi,Makojo,Tegeruka na Busambara ambapo makao makuu ya halmashauri hiyo yatakuwa Suguti-Kwikonero.

Halmashauri ya Butiama nayo inakata 17 ambazo ni Nyankanga,Buruma,Bukabwa,Bwiregi,Nyamimange,Buswahili,Sirolisimba,Mirwa,Buhemba,Muriaza,Kukirango,Busegwe,Butiama,Masaba,Bisumwa na Kyanyari ambapo makao makuu ya halmashauri hiyo yatakuwa Butiama
  

No comments:

Post a Comment