Friday, August 10, 2012

TAASISI ya Kuzuia na kupambana na rushwa(TAKUKURU) Mkoa wa Mara, imemfikisha Mahakamani Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ,Christopher Nyandiga

MUSOMA



TAASISI ya Kuzuia na kupambana na rushwa(TAKUKURU) Mkoa wa Mara, imemfikisha Mahakamani Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ,Christopher Nyandiga kwa makosa ya kutumia nyaraka zenye lengo la kumdanganya mwajiri wake kinyume cha sheria na kuisababishia  serikali hasara ya jumla ya  Sh Milioni 24.



Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Naibu Mkuu wa Taasisi hiyo Mkoa, Yustina Chagaka imesema kuwa Mhandisi huyo ambaye kwa sasa yuko Wilaya ya Ledewa alifanya makosa na kudanganya mwajiri wake kinyume na kifungu cha 22 cha sheria ya kuzuia na kupambana an rushwa Namba 11 ya mwaka 2007 na kifungu cha 10(1) cha jedwali la wkanza kikisomwa pamoja na vigungu vya 57(1) na 60(2) vya sheria ya uhujumu uchuni Namba 200 kama ilivyofanyiwa mapitio mwaka 2002.



Ilisema baada ya uchunguzi uliofanywa na  TAKUKURU umebaini kuwa kampuni inayomilikiwa na mshitakiwa iitwayo Mbully Enterprises and Covil Works ilipewa zabuni na halmashaur ya Wilaya ya Bunda ya kutoa Wind mill aina ya Poldaw ya mita 5.8/mita 8.2 kwa gharama ya Sh. Milioni 24, kuisimika (installation)  kwa gharama ya Sh. Milioni 2,  kuifanyia majaribio (testing) kwa gharama ya Sh. Milioni 1  na  Jumla yake ikiwa  Sh Milioni 27 kwa ajili ya mradi wa umwagiliaji mazao katika kijiji cha Kasuguti.




Aidha uchuguzi uliofanywa umebaini kuwa Mnano Disemba 2007 kwa niaba ya Kampuni hiyo iliyowasilisha hati ya madai(invoice) namba 0152 na delivery note namba 0252 kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda zenye maelekezo ya uongo.



Maelezo hayo yalisema kuwa alinunua na kuwasilisha Wind Mill moja aina ya Poldaw ya mita 8.2 yenye thamani Sh Milioni 24 huku akijua kuwa si kweli kwa sababu Wind Mill hiyo haikuwa ya Poldaw ya Mita 8.2 bali ilikuwa chakavu ambayo haifai kwa matumizi yaliyokusudiwa.



 Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Mara inatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa.

No comments:

Post a Comment