MUSOMA.
Madiwani wa Manispaa ya Musoma wametakiwa kusimamia
ukusanyaji wa mapato kikamilifu ili kuiwezesha Manispaa kupata fedha
zitakazotumika kuwahudumia wananchi wake.
Hayo yamesemwa na Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurura katika kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa.
Alisema halmashauri hiyo ya manispaa inavyo vyanzo vingi vyamapato,ambavyo vikikusanywa vizuri vitasaidia katika kuboresha huduma muhimu kwa wananchi kama vile huduma ya maji na barabara..
Naye Mchumi wa Manispaa ya Musoma John Masero alisema baadhi ya Madiwani na watumishi wa Manispaa wanatuhumiwa kwa kuwa na maslahi binafsi katika suala la kutoa zabuni mbalimbali katika Manispaa.
Masero alilieza baraza hilo kuwa hayo kufuatia baadhi ya Madiwani katika baraza hilo kushinikiza kupunguzwa kwa masharti katika mchakato wa kutoa zabuni hali ambayo itaipunguzuia Manispaa mapato.
Akichangia hoja hiyo diwani wa kata ya Kigera Charles Ocharo ameziomba Idara husika
kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo ili wote watakaobainika wachukuliwe hatua za kisheria.
Madiwani wa Manispaa ya Musoma wametakiwa kusimamia
ukusanyaji wa mapato kikamilifu ili kuiwezesha Manispaa kupata fedha
zitakazotumika kuwahudumia wananchi wake.
Hayo yamesemwa na Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurura katika kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa.
Alisema halmashauri hiyo ya manispaa inavyo vyanzo vingi vyamapato,ambavyo vikikusanywa vizuri vitasaidia katika kuboresha huduma muhimu kwa wananchi kama vile huduma ya maji na barabara..
Naye Mchumi wa Manispaa ya Musoma John Masero alisema baadhi ya Madiwani na watumishi wa Manispaa wanatuhumiwa kwa kuwa na maslahi binafsi katika suala la kutoa zabuni mbalimbali katika Manispaa.
Masero alilieza baraza hilo kuwa hayo kufuatia baadhi ya Madiwani katika baraza hilo kushinikiza kupunguzwa kwa masharti katika mchakato wa kutoa zabuni hali ambayo itaipunguzuia Manispaa mapato.
Akichangia hoja hiyo diwani wa kata ya Kigera Charles Ocharo ameziomba Idara husika
kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo ili wote watakaobainika wachukuliwe hatua za kisheria.
Manispaa inatajia kujenga barabara za Mitaa kwa kiwango cha
Lami na katika Mitaa kadhaa sanjali na kuweka vibao vya Mitaa ya baadhi ya majina ya waasisi wake ili waendelee kuezniwa ikiwa
pamoja na Mtaa wa Lucas Musiba eneo la Nyasho Kona, ambao kibao chake
hakijulikanai kilipelekwa wapi.
No comments:
Post a Comment