MUSOMA.
Makarani waandamizi wasimamizi wa Washiriki wa Sensa ya watu
na makazi wameombwa kufuatilia na kusikiliza kwa makini mafunzo watakayopewa na
wawezeshaji wa zoezi hilo ili kuleta ufanisi katika zoezi hilo.
Hayo yamesemwa LEO na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Jackson Msome
wakati akifungua semina kwa Makarani Waandamizi na wasimamizi wa sensa na makazi katika ukumbi wa Chama Cha
Mapinduzi Mkoa wa Mara.
Jackson Msome amesema kuwa mafunzo hayo yatawawezesha
washiriki kupata mbinu za kuuliza maswali, namna ya kujaza dodoso refu na taarifa mbalimbali za kaya na kutambua namna ya kuhifadhi siri na taarifa za
kaya ambazo wamezipata.
Amesema kamati imewaamini kufanya kazi hiyo hivyo washiriki
wanaombwa watambue dhamana kubwa waliyopewa na serikali hivyo ufanisi na
uhodari wao katika kazi utapimwa kwa mafanikio ya sensa iyo itakayoanza Agosti 26,
2012.
Aidha Serikali
inapenda kuona sensa hiyo ikipata mafanikio makubwa hivyo semina hiyo inalenga
kuwajengea uwezo mkubwa na ufanisi ili kila wilaya ifanikishe zoezi hilo kwa
ufanisi zaidi kwa maslahi ya taifa kwa ujumla.
Aidha ametaka viongozi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya
habari kwani ndio sekta muhimu katika kuelimisha wananchi kuhusiana na sensa ya
watu na makazi na kwamba vyombo vya habari vina nguvu na mchango mkubwa katika
kutoa elimu ya uhamasishaji hivyo ni vema kama vyombo hivyo vitatumia nafasi
hiyo kuhamasisha wananchi ili watoe
ushirikano wa kutosha katika zoezi hilo.
Mafunzo hayo ya Sensa ya watu na makazi yamefunguliwa rasmi
Agosti 9 katika Wilaya ya Musoma na jumla
ya washiriki wapatao 200 wamehudhuria mafunzo hayo na kwamba yatafanyika muda
wa siku kumi na moja.
No comments:
Post a Comment