Friday, August 10, 2012

MWENGE WA UHURU KUANZA MBIO ZAKE MKOA WA MARA.


MUSOMA


MBIO za Mwenge wa Uhuru zinaanza  Agosti 13 katika Mkoa wa Mara ambapo utawasili katika Kijiji cha Robanda Wilaya ya Serengeti na kupokelewa Nabi -Gate  ambapo kutafanyika makabidhiano kati ya Mkoa wa Arusha na kuingia Mkoa wa Mara.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, inasema Mara baada ya kuokelewa utaanza mbio zake kwa kuzindua miradi mbalimbali ya Maendeleo.
Miradi itayowekewa jiwe la Msingi ni pamoja na Sekondari ya Robanda, kisima cha Motukeri, jengo la kituo cha wakulima Natta na kupokea taarifa ya ujenzi.

Ukiwa Wilaya ya Serengeti Mwenge huo  utafanya uzinduzi wa nyumba bota ya mwanakijiji wa Nyichoka,kupokea taarifa ya mwenye nyumba nay a ujenzi wa jengo la huduma ya Mama na Mtoto na kufungua jengo pia kuweka jiwe la msingi katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji ambapo zawadi na cheti zitatolewa kwa club ya wapinga rushwa.


Aidha katika Wilaya ya Tarime Mwenge huo utafungua SACCOS ya Masanga,kuweka jiwe la Msingi kituo cha  Afya cha Nyanungu, kutembelea shamba la Migomba la ekari tanio na kuzindua uvunaji maji ya mvua matenki mawili, kufungua jengo la utawala la Magoto Sekondari, kufungua ofisi ya Kata ya Nyarero,kuzindua daraja la Ronsoti na barabara yenye urefu wa Mita800, wodi ya Wazazi ya hospitali ya Wilaya,mradi wa kitalu cha kahawa na chai.

Mwenge huo ukiwa katika Wilaya hiyo pia utazindua klabu ya kuzuia rushwa na madawa ya kulevya, kufungua zahanati ya Ikoma, kuzindua kisima cha maji katika Sekondari ya Mirare, kufungua Saccos na kuweka jiwe la msingi Utegi Saccos, utatembelea hifadhi ya mazingira na ufugaji wa nyuki pamoja na kukabidhi Mizinga mitano ya nyuki na kisima cha Maji na kuweka jiwe la msingi baabara ya Buturi sekondari na kufanya ukaguzi wa Kilimo cha umwagiliaji na kukabidhi power tiller nne,Trekta mbili na mashine ya kukoboa mpunga na kutembelea kikundi hc kuteketeza nyavu haramu kilichoko Kinesi.

Katika Manispaa ya Musoma Mwenge huo utaweka jiwe la misngi kwenye nyumba bora ya mwananchi, kufungua mradi wa maji Shule ya Sekondari ya Ufundi,kuweka jiwe la msingi maabara ya sekondari ya Bweri  na kuzindua klabu ya TAKUKURU, kuweka jiwe la msingi katika wodi ya watoto iliyoko Nyakato, kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya Kwangwa kilometa 2, kufungua vyumba vinne vya madarasa shule ya msingi kigera na kupanda miti ya vivuli na matunda pia kufungua Kantini  ya Chuo cha VETA.

Utafungua pia jengo la kuhifadhi maiti(Mochwari), kukagua na kuhasisha kikundi cha vijana cha useremala na Saccos ya akinamama iliyoko uwanja wa Mpira wa Karume na kutoa hundi ya Sh. 100,000.


Agosti 17 Mwenge huo utaelekea katika Wilaya ya Butiama ambapo makabididhiano yatafanyika kijiji cha  Nyankanga na kuelekea Butuguri.




No comments:

Post a Comment