Wednesday, October 2, 2013

MJI WA MUSOMA WAKUMBWA NA UHABA WA MAJI



MUSOMA


ZIWA Victoria limekuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Mji wa Musoma kutokana na tatizo la ukosefu wa maji katika baadhi ya maeneo ya Mji wa Musoma Mkoa wa Mara, ambapo kwa sasa ni la  takribani siku tano.

Uchunguzi uliofanywa na blog hii, umebaini kuwa wakazi wa maeneo ya kando kando ya ziwa hasa, Baruti, Bweri na Iringo wamekuwa wakichota maji katika ziwa hilo kutokana na kukosa maji ya bomba katika maeneo wanayoishi huku njia mbalimbali za boda boda na baiskeli na vichwa vya  akina mama wakibeba maji hayo kutoka ziwa hilo.

Wakizungumzia suala hilo kwa nyakati tofauti, Mkazi wa Bweri, Gabriel Kambuga Mkazi wa Kata ya Bweri, alisema kuwa kwa sasa wana takribani wiki moja hawajapata huduma hiyo na hivyo kuwalazimu kwenda kuchota ziwani ambapo maji hayo hayana usalama.

Naye mkazi wa Kigera, Edward Patrick aliyefika katika ofisi za Muwasa kutaka kujua   huduma hiyo itarejea lini,alisema kuwa eneo hilo halijapata maji kwa muda wa wiki moja,lakini tatizo lao halihusiani na kutatika kwa bomba Mtaa wa  Nyerere.

Afisa Mahusiano wa Mamlaka ya  Maji safi na Taka Mjini Musoma(MUWASA), Emmanuel Ruyobya  amesema kuwa tatizo hilo limetokana na upanuzi wa barabara ambapo Kampuni ya Kichina imekata mabomba ambayo yanasafirisha maji kwenda kwa wakazi sehemu mbalimbali za mji huo.

“Mabomba yaliyopo yamechakaa sana, na yana miaka kama 50 hivi, sasa yanapokuwa yanahamishwa ili kupisha ujenzi wa barabara yanakatika, hilo ndo tatizo kubwa lililosabisha wakazi hawa kukosa maji,jitihada zinafanywa ili kurejesha huduma hiyo haraka” Alisema Ruyobya

Maeneo ambayo hayana  Maji ni Iringo, Nyamatare, Mkendo kati, Kigera, Kwangwa, Nyakato, Nyasho, kitaji,Bweri na Kiara.

No comments:

Post a Comment