Thursday, December 1, 2011

MAAMBUKIZI YA UKIMWI MKOA WA MARA YAKO JUU

MUSOMA.

MKOA wa Mara unaongoza katika maambukizi mapya kwa asilimia 4.2 kwa mwaka 2007/2008 kutoka asilimia 3.5 mwaka 2003/ 2004.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa kwa niaba yake, Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Godfey Ngatuni katika siku ya maadhimisho ya Ukimwi Duniani kimkoa yalifanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Kamunyonge Manispaa ya Musoma.



Amesema kuwa kutokana na utafiti wa kisayansi uliofanyika mwaka 2007/ 2008 maambukizi kitaifa yamepungua kidogo kutoka asilimia 7 mwaka 2003/ 2004 hadi asilimia 5.7 wanawake wakiwa na asilimia 6.6 na wanaume wakiwa na asilimia 4.6.



Aidha amesikitishwa na ongezeko la maambukizi mapya kwa Mkoa wa Mara na kwamba ni jambo la aibu ambapo Mkoa uliokuwa ukiongoza wa Iringa, Wilaya ya Makete umeweza kupungua kutoka asilimia 2.3.
Amewataka viongozi pamoja na wananchi wa Mkoa wa Mara, kushirikiana pamoja na taasisi kufanya jitihada za kuwez kutokomeza ugojwa huo kama Mikoa mingine walivyoweza kujikinga.



Awali kabla ya kutoa hotuba yake, Mkuu wa Mkoa walipata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali ambayo yanafanya shughuli za kuelimisha jamii juu ya Ukimwi ni janga la Kitaifa na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na watu wanoishi na VVU, ambapo wawili walitoa ushuhuda wa jinsi wanavyoishi na VVU na kuwapa moyo waliombukizwa kutokata tamaa.


Tangu maadhimisho hayo yameanza Novemba 29- Disemba 1 mwaka huu jumla ya wakazi wa Musoma wapatao 784 wamejitokeza kupima ambapo kati ya hao walioathirika walikuwa 14. Wanawake SABA na wanaume SABA.


Kauli mbiu ya siku ya Ukimwi Duniani Kitaifa ni Tanzania bila ya maambukizi mapya, Unyanyapaa na vifo vitokanavyo na Ukimwi inawekana, ambapo kauli mbiu ya Mkoa ni Mara bila ya maambukizi mapya inawezekana.


Siku ya Ukimwi Duniani Kitaifa imefanyika Mkoa wa Shinyanga.
Naye Naibu Mkurugenzi wa Shirika ya Aids Relief Dk. Protace Ndayanga amesema ni wajibu wa kila mmoja kutofanya unyanyapaa kwa mtu mwenye virusi vya ukimwi na badala yake wananchi wasaidie kutoa huduma na kushiriana nao kwa pamoja kwa kuwaptia tiba na chakula bora.

Amesema pamoja na juhudi zinazofanywa na serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali bado maambukizi yamekuwa hali inayoweza kuwavunja moyo watoa huduma ili kutokomeza ama kupunguza ugojwa huu.
Ameongeza kuwa Shirika lake linafanya kampeni ya kila Wilaya ya kutoa elimu kupitia vyombo vya habari.

No comments:

Post a Comment