katikati ni afisa Usalama Mkoa wa Mara.
Monday, February 23, 2015
GLORIOUS LUOGA-DC TARIME
MKUU wa Wilaya ya Tarime, Glorious Luoga akipokea vitendea kazi.
MKUU wa wilaya ya Tarime akisaini kiapo.
Akiwa na mkewe, Mrs Stella Nyandindi mara baada ya kuapa.
Wakuu wa Wilaya,katika Mkoa wa Mara, wakiwa katika picha ya pamoja, mara baada ya kuapa, hapa ni bustani ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.
DC MPYA TARIME AKILA AKIPO CHA UTII
Wednesday, February 4, 2015
NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, ZIARANI.
ISIBANIA.
Jengo lenye rangi ya ugoro ni la kenya.
WATANZANIA, wametakiwa kuchangamkia fursa za kufanya biashara nchi jirani ili kukuza kipato chao na si kukaa na kulalamika kama ilivyo sasa.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Amantius Msole alipokuwa akizungumza na wafanyabiahara wadogo wadogo katika mpaka wa Tanzania na Kenya (Sirari) Mkoa wa Mara.
Amesema watanzania wanapaswa kufahamu juu ya Umoja wa Afrika Mashariki na kujua sheria zake ili wapate fursa za kufanya biashara na kwamba wawe tayari kufanya ushindani wa biashara kabla ya nchi nyingine kuingia ndani na kufanya biashara ambazo wao wanaweza kufanya.
“Nashangaa kuona hata maji ya kunywa, tunakunywa kutoka nchi ya Kenya na Uganda na huku tuna viwanda vingi nchini kwetu vyenye ubora ule ule, kwa hilo tu unaweza kuona wafanyabiashara wenzetu wamechangamkia fursa hii, pia sisi watanzania tumekuwa na kasumba ya kutopenda bidhaa zinazotengenezwa nchini kwetu,tuweni wazalendo” Alisema Msole.
Amesema kuwa katika ziara yote ya kutembelea maeneo ya mipaka kote nchini amegundua kuwa watanzania wengi hawajapata elimu juu umoja wa Afrika Mashariki na fursa ambazo wanaweza kuzitumia ili waweze kufanya kazi kwa pamoja, hivyo ameagiza wadau wote wanaohusika kutoa elimu haraka iwekezanavyo ili waweze kunufaika na umoja huo.
Akizungumza na Naibu Katibu Mkuu, Ofisa wa Mapato wa Mamlaka ya Mapato ya Kenya (KRA), Kingori Mwangi alimweleza kuwa kwa upande wa Kenya, jengo la Mamlaka yao limeishakamilika kwa kiasi kikubwa na kwamba lina eneo la wanyama kama Ng’ombe, Mbuzi Kondoo na ndege aina ya Kuku(Animal Holding), ambapo wafanyabiashara wa Tanzania wanapofika wataweka mifugo yao tayari kwa kukaguliwa na kusafirisha nchini Kenya kwa kuuza.
Amesema kuwa kwa upande wa vyumba mbalimbali vilivyokamilika amesema kuwa vyumba vingi muhimu vimekalimika vikiwemo vya kukagua bidhaa zinazofaa na zenye sumu (Poison and Health Room), X-ray Chumba cha kuteketeza madawa yasiyofaa yanaoingia mpakani mwa Tanzania na Kenya (Incinerator), chumba cha kuifadhia samaki,chumba cha mbwa wa upelelezi wenye uwezo wa kunusa wezi, sumu, madawa ya kulevya na kadhalika ambalo litakabidhiwa mwezi feburari mwaka huu, huku jengo la Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) bado halijakamilika.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki na viongozi wake wote kutoka Wizarani walifanya ziara katika Mikoa iliyoko mipakani, Mtukula, Sirari, Kabanga, Namanga na Hororo kwa lengo la kujifunza na kuhamasisha wananchi kuchangamkia fursa za biashara.
Subscribe to:
Posts (Atom)