Friday, August 19, 2011

AMREF WAANZA MIRADI YAO MKOA WA MARA.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara,Clement Lujaji mwenye suti nyeusi akipeana mkono na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika AMREF,Festus Ilako,mara baada ya kuweka saini za makubaliano kati ya AMREF na Serikali kuhusu uendeshaji wa miradi ya afya ya mama na motto na maendeleo ya janii Mkoa wa Mara kwa wilaya mbili za Tarime na kijiji cha Tegeruka cha Wilaya ya Musoma vijijini.

RAS huyo pia alishuhudia,usainiaji wa mikataba ya makubaliano kati ya Shirika la AMREF Tanzania na Serikali kuhusu uendeshaji wa miradi ya afya ya mama na mtoto, miradi ya TUIMARISHE uzazi wa mpango,afya ya mama na maji, wa Musoma vijini utakaogharimu kiasi cha Sh.M 322 na Mradi wa Uzazi wa mpango na maendeleo ya mwanamke ambao pia utagharimu kiasi cha Sh M. 464 na Wilaya ya Tarime katika mradi wa uimarishaji utoaji wa huduma ya afya ya msingi utakaogharimu kiasi cha Sh.B.1.3, baina ya Mkurugenzi Mkazi wa Shirika hilo, Festus Ilako na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Musoma vijijini, Jamhuri William iliyofanyika katika bwalo la Polisi leo mchana.







No comments:

Post a Comment