Monday, February 6, 2012

LUKUVI AONGOZA MATEMBEZI YA MSHIKAMANO YA CCM MKOA WA MARA.

SERENGETI.

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera na Utatibu wa Bunge pia Mlezi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara, Mh. William Lukuvi amewaasa wale wote wenye tabia za kukikumbatia Chama Cha Mapinduzi CCM kuwa ni Chama kutoka mifukoni mwao waache tabia hiyo mara moja ili kurudisha heshima na Chama na wananchi kukiamini Chama chao.

Aliyasema hayo juzi katika kilele cha Maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama ambapo kimetimiza miaka 35 sasa tangu kuzaliwa kwake, Wilaya ya Serengeti Mugumu mara alipokamilisha matembezi ya msikamano kukumbuka kuzaliwa kwa Chama.

Waziri huyo aliongoza matembezi ya mshikamano kutoka katika ofisi za Chama hicho mpaka viwanja vya mbuzi na kuhudhuriwa na baadhi ya wanachama wakiwemo viongozi wa Chama Mkoa na Wilaya, Wakuu wa Wilaya wa Wilaya za Musoma na Serengeti akiwemo Mkuu wa Mkoa.

Maadhimisho hayo yaliyotarajiwa kufanyika kimkoa katika Wilaya ya Serengeti, yaliadhimishwa kwa kila Wilaya ambapo kila Wilaya zilifanya matembezi yao ya mshikamano kujikumbushia Chama kilipotoka, kiko wapi na kinakwenda wapi.

Alisema kuwa kuna baadhi ya wanachama wamekifanya Chama Cha Mpianduzi kuwa Chama kutoka mifukoni kwao na kutozingatia maamuzi na ushauri kutoka kwa viongozi wengine.

Akizunguza katika Ukumbi wa Mikutano wa Musoma Mjini alipokutana na wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM Mkoa na Wilaya, Makatibu kata, Madiwani na wajumbe wa kamati za utekelezaji wa Wilaya za Musoma Vijijini na Mjini aliwaasa kuacha tabia hiyo ili kukiweka Chama pazuri.

Aliwataka kujiimarisha wao wenyewe kwanza,kabla ya kuimarisha Mikoa mingine, ukizingatia kuwa Mkoa huo ni bigwa wa kupigia kampeni Mikoa mingine huku wao wakiwa nyuma.

“Nyinyi mnasifika kwa kupanga siasa za Mikoa ya wenzenu Mkoa wa Mara mko wachache sana lakini mkiamua jambo likuwa la kweli! Kweli! Mbona kwenu mnashinda. Mnasifika sana kwa kupanga siasa za mikoa mingine, Irekebisheni ya kwenu kabla ya kurekebisha ya wenzenu” Alisema Lukuvi huku ukimya ukitawala katika Ukumbi huo.

Aliwaasa kutumia uwezo huo walionao kujipanga upya na kuhakikisha Chama kinashinda kuanzia ngazi ya Shina na Matawi unaotajia kuanza mwezi huu.

“Safari hii hakikisheni mnachagua viongozi bora watakaoweza kukiongoza Chama na wenye moyo wa kujituma na uwezo wa kuwashawishi wanachama ili kupata ushindi, na wajue kuwa watakuwa na kibarua kigumu” Alisisitiza Lukuvi.

Alitumia fursa hiyo kumtaka kila mwana CCM, kutoka maoni yao juu ya mabadiliko ya katiba Mpya pindi tume itakapokuja kukusanya maoni.

Wakati huo huo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera na Utaribu wa Bunge na Mlezi wa Mkoa wa Chama Mkoa alizindua Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ambalo hadi kukamika kwake limegharimu kiasi cha Sh. M. 26.

Awali kabla ya uzinduzi huo aliwataka wananchi kutumia kwa uangalifu chakula walichopata na kuacha tabia ya kuuza mazao nje ya nchi na baadae kuiomba serikali kuleta chakula cha msaada, huku akizitaja wilaya za Bunda, Musoma Vijijini na Musoma Mjini kuwa waombaji wa misaada.

Kuhusu fedha zinazoletwa kwa ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali aliwataka madiwani wafuatilia kama fedha hizo zinatumika ipasavyo kwani kuna baadhi ya miradi haitekelezeki na matokeo yake wananchi wanaichukia serikali yake kwa baadhi ya watu wachache walio na ubadhilifu wa fedha. Wilaya hiyo imepewa B.19.7

Waziri pia alizindua Shina la kikundi cha Wajasiamali wadogo wa CCM wanaojishughulisha na fani za ufundi Seremala, Vyuma, cherehani, Uashi, Ususi na Upakaji rangi (SECHUWARA) wa Wilaya ya Serengeti ambapo alijibu risala yao kwa kuendesha mchango wa papo kwa papo ambapo Sh. M. 1.5 zilipatikana, ambazo zitawasaidia kuendeleza biashara ambapo pia aliagiza Halmashari kuwatafutia eneo ambalo watafanya shughuli zao bila kulipia ili kupunguza gharama na kuhakikisha kikundi hicho kinapata usajili ili waweze kupata mikopo.


Friday, February 3, 2012

SIKU YA SHERIA DUNIANI,JESHI LA POLISI LAWAMANI

Musoma

CHAMA cha Mawakili wa Tanganyika (TLS) Mkoa wa Mara wameonesha
kusikitishwa na Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani
wanaosimamia na kuhakikisha matumizi bora na sahihi ya barabara
wamegeuka kuwa hakimu wa makosa yote, pia wamepinga adhabu kwa mtu
aliyehukumiwa kuua kwa kukusudia ahukumiwe kifo na kusema kuwa hiyo
sio sahihi na wala haki.

Kauli hiyo ilitolewa na Wakili Baraka Makowe kwa niaba ya chama hicho
ambapo alisema kuwa askari hao wa barabarani wamekuwa wakitoza faini
kwa kwa mamlaka ambayo wamepewa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya
OCD na si Kamanda wa usalama barabarani (OCS) ama kamanda wa usalama
barabarani Mkoa (RTO).

“ kanuni za utoaji adhabu hazifuatwi wakati sheria
inaelekeza vipi atendewe mkosaji wa mara ya kwanza, mkosaji mzoefu na
kwa kiwango gani cha adhabu kitolewe, wenzetu leo kila kosa hutoza
faini ya shilingi 30,000,”alisema Wakili Makowe.

Alisema kuwa maudhui ya siku ya sheria nchini yanayohusu faida za
adhabu mbadala kwa jamii, hazitakosewa wakiendelea kusisitiza kuwa
adhabu huambatana na hatia na shurti itamkwe na kutolewa na na taasisi
yenye mamlaka hayo kisheria.

“Si kwa sera, mazoea au matakwa, kufanya hivyo ni kosa na ni kinyume
cha sheria, nataka kwanza tujikite katika utoaji wa adhabu mbadala
ndipo tuangalie faida husika. Kwa kuwa jambo hili ni pana, juhudi za
kulichambua kwa undani zitafanyika na hivyo huenda ikaathiri mtiririko wa uwasilishaji wa mada lakini nina imani tutagusa sehemu zote muhimu,”alisema.

Alisema kuwa kutokana na kupitia maudhui ya Adhabu mbadala katika kesi
za jinai, na faida zake kwa jamii kwa niaba ya chama cha mawakili wa
Tanganyika muda muafaka umefika na vifungu vya 197 na 26 (1) vya sura
ya 16 ya sheria za nchi vitazamwe upya.

“Ni muda muafaka kwa adhabu mbadala itumike na iamriwe hadi kugusa
kesi za mauaji ya kukusudia, pia kwamba hata vile vifungu vya 195 (1)
na 198 vya sheria hiyo navyo vitazamwe upya. Kwamba si jambo jema mtu
akae gerezani hadi atakapokufa adhabu mbadala yaweza kutolewa kwake,”
alisema.

Naye Hakimu Mfawidhi Mwandamizi wa Mkoa huo, Hussein Mushi alisema
kuwa adhabu mbadala inafaida nyingi katika jamii ambapo baadhi ya
faida ni pamoja na kupunguza msongamano magerezani ili kuipunguzia
serikali gharama za kuendesha magereza kwa kupunguza watu wanaotegemea
huduma magerezani.

“Hii ni pamoja na kuishirikisha jamii kwa kuwarekebisha wahalifu na
kuwawezesha wahalifu kuendelea kutunza na familia zao huku wakiendelea
kutumikia vifungo vyao, kutoa mchango wa maendeleo kwa jamii pale
wafungwa wa kifungo cha nje wanaposhiriki katika ujenzi wa wa shule,
hospitali, barabara, utunzaji wa mazingira na usafi katika ofisi za
umma hali itakayoipunguzia serikali gharama za shughuli hizo, alisema
Mushi.

Pia alitoa onyo kwa wananchi kuacha tabia ya kuingilia shughuli za
huduma za jamii wajue kuwa ni kinyume cha sheria na ni kosa la jinai
na mtu anapotiwa hatiani atapaswa kulipa faini ya shilingi Laki 5 au
kifungo cha miaka miwili jela au vyote viwili.

siku ya sheria nchini na inahashiria mwanzo wa shughuli za mahakama kwa mwaka 2012 ambapo maudhui yake ni adhabu mbadala katika kesi za jinai, faida zake katika jamii ambapo hufanyika mwezi wa pili wa kila mwaka.

Thursday, February 2, 2012

NNAUYE AKABIDHI MIFUKO YA SIMENTI.

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Nape Nnauye amekabidhi mifuko 400 ya simenti kwa Mkoa wa Mara kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa madarasa ambayo ni pungufu.

Akikabidhi mifuko hiyo kwa Katibu huyo, Mfanyabiashara ambaye ni Mkazi wa Mkoa wa Mara, Zulfikar Nanji,alisema amehamasika kusaidia jamii ya Mkoa huo kutokana na Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa akipokuwa akizungumzia upungufu wa madarasa uliopo katika Mkoa huo ambao umesababisha baadhi ya wanafunzi kutoendelea ma shule.

“Nimehamasika kutokana na kusikia kwenye vyombo vya habari taarifa ya Mkuu wa Mkoa akizungumzia juu ya upungufu wa madarasa yaliyosababisha baadhi ya watoto kukosa nafasi za kuendelea na masomo yao, nikaona si vyema na mimi kama mzaliwa wa Mkoa huu sina budi kuisaidia” Alisema Nanji.

Akitoa shukrani kwa mfanyabiashara huyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi (CCM), Nape Nnauye alisema wakati Chama kinaelekea kutimiza miaka 35 ya kuzaliwa kwake bado kiko imara na kitaziki kuwa imara kutokana na kwamba kinatekeleza ilani ya CCM.

“Wakati tukielekea katika maadhimisho ya miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCM, tunapata matukio mengi mazuri na yanayoashiria kukuwa na kuendelea kwa Chama kilichosheheni ubora, Amani na Utulivu wa nchi yetu” Alisema Nnauye.

Wakati wa makabidhinao hayo aliyofanyika katika uwanja wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, wakereketwa na viongozi wa CCM, pia walijitokeza kuunga mkono msaada huo, akiwemo Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, MNEC, Vedastus Mathayo akiyehaidi mifuko 100 ya simenti, Diwani wa kata ya Nzela Wilaya ya Geita Mkoa wa Mwanza, Joseph Msukuma ambaye pia akiahaidi mifuko 100, na Diwani Mstaafu wa kata ya Bweri Wilaya ya Musoma Mjini, Isaack Chacha ambaye pia aliahidi mifuko 20 ya simenti.

Akizungumzia upungufu wa madarasa uliopo, Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa alisema jumla ya madarasa 239 yanatakiwa kujengwa ili watoto wapatao 6,486 ambao mpaka sasa wako majumbani kufikia mwezi Machi wawe wameanza shule.

Wilaya zenye uhaba mkubwa ni Wilaya ya Bunda ambayo ina upungufu wa madarasa 88, Musoma vijijini madarasa 46 na Musoma Mjini madarasa 26