Wednesday, September 19, 2012

MTOTO WA BABA WA TAIFA,MAGIGE NYERERE ULINGONI.

MUSOMA




KATIBU wa CCM Wilaya ya Butiama,Mkoa wa Mara, Mercy Mollel amewatahadharisha wagombea katika nafasi mbalimbali ili kujiepusha na rushwa pindi wanapoomba ridhaa ya kuwatumikia wananchi.

Aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake na kutangaza majina ya wagombea katika nafasi mbalimbali ndani ya Chama.

Alisema wakereketwa wengi wamejitokeza katika kuomba nafasi mbalimbali za uongozi kwa kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho chenye mvuto kwa jamii kubwa kutokana na sera zake zinazoaminika na kwamba ndhicho kinachoongoza nchi.

Alisema katika nafasi ya Ujumbe Mkutano Mkuu wa CCM Taifa waliojitokeza ni wanachama  wapatao 43,ambapo katika mchujo wanachama wapatao 15 ndio walioteuliwa ambapo watatakiwa wajumbe watano, aliwataja kuwa ni Nyageti Adamu, Eva-Sweet Musiba,Bhoke Ngurube, Rosemary Orinda, Wegesa Witimu,Vivian Juma,Joseph Magere, Brasius Chuma, Fidelis Kisuka, Gerald Kasonyi, Sebastian Makakira, Rashid Gewa, Jerome Masawe, Nyabukika Nyabukika, Magige Nyerere.

Aidha katika nafasi ya Katibu wa Siasa na  Uenezi walijitokeza wanachama wapatao tisa, ambapo waloiteuliwa kugombea nafasi hiyo ni wajumbe wapatao watatu nao ni, Bwire Gibuma Ntobi Zedesi Ntobi na Japhet Werema,nafasi ya Uchumi na fedha waliojitokeza walikuwa sita na waliopita katika mchujo ni Baraka Imanyi (Obama), Haruni Munema na Magina Nyauko.

Katika nafasi ya Ujumbe Mkutano CCM Mkoa waliojitokeza ni Wegesa Witimu,Break Chisumo, Yohana Munema, Rudia Mazera, Nestory Matiko na Happiness Nyamasagara.

Alisema kuwa katika kundi la wanawake jumla ya wakereketwa wapatao 32 walijitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo, walioteuliwa ni Thabita Idd, Wegesa Witimu, Mwajuma Magoti na Bhoke Ngurube,ambapo Wazazi walioteuliwa kugombea ni Fidelis Kisuka, Wambura Kishemuri, Ihunyo Marwa, John Nyamisana, Ibrahim Makanya na James Matongo.

Alisema kuwa kwa upande wa kundi la vijana nafasi ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya walijitokeza wagombea wenye umri mkubwa na hivyo kusababisha kutoteuliwa.

Aliongeza kuwa kwa upande wa nafasi za Mwenyekiti na Wajumbe wa NEC yanasubiriwa kutoka Halmashauri Kuu Taifa irejeshe majina  ya wanachama walioomba nafasi hizo.




Monday, September 3, 2012

JUMUIYA ZA CCM ZA UWT NA WAZAZI MUSOMA MJINI WAPATA VIONGOZI WAO.





JUMUIYA ZA CCM ZA UWT NA WAZAZI MUSOMA MJINI WAPATA VIONGOZI WAO.

MUSOMA.

JUMUIYA ya Wanawake (UWT) ndani ya Chama Tawala CCM,Mkoa wa Mara imepata viongozi wao wakaokitumikia Jumuiya kwa Miaka mitano.

Akizungumza na Mwandishi wa Habari hii, ofisini kwake, Katibu wa UWT Wilaya ya Musoma Mjini Ashura Kimwaga alisema uchaguzi huo uliofanyika hivi karibuni ulikuwa na Changamoto mbalimbali kwa akina Mama kuwa na mwamko mkubwa wa  kujitokeza kuchukua fomu za kugombea.

Katika nafasi ya Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo waliojitokeza  kuchukua fomu walikuwa watano lakini ulipofanyika mchujo watatu waliteuliwa kuchukua,wakiwemo Dinna Samanyi ambaye alipata kura 111 akifuatiwa na Odina Lujaji ambaye aliambulia kura saba, huku Amina Masisa akichukua nafasi hiyo kwa kuibuka mshindi kwa kupata kura 143.

Katika nafasi ya Ujumbe Mkutano Mkuu wa Taifa waliojitokeza walikuwa wagombea tisa,ambapo nane waliteuliwa katika kinyang’anyiro hicho ambapo nafasi hiyo inapaswa kuwa na wajumbe watatu,waliopata ushindi ni Godriver Magoti aliyepata kura 147, Zainabu Musiba(126) na Riziki Hamis(119),naye Rukia Wandwi ambaye aliwahi kugombea Ubunge viti Maalum akiambulia kura (109), Kura zilizopigwa zilikuwa 262 na kura moja kuharibika.

Katika nafasi ya Ujumbe Mkutano Mkuu wa Mkoa waliojitokeza kuchukua fomu walikuwa saba, waliopitishwa walikuwa na nane ambao waliingia katika mchuano mkali na hatimaye washindi kupatikana,walishinda ni Nyambura Mtani alipara kura 130 akifuatiwa na Rehema Nyabina alitepata kura 128 na Twaiba Makangara aliyepata kura 127.

Aidha waliojitokeza katika kuwania nafasi ya Baraza la UWT walikuwa 12 ambapo waliyeuliwa 11 katika kugombea nafasi hizo, washindi waliopatikana na kura zao zikiwa kwenye mabano ni Nyambura Kunani(121), Maimuna Kimaro (108), Naima Minga (98), Rehema Nyambina(95), Stella Mtani (90), Janeth Mkilimali (88), kura zilizopigwa zilikuwa 262 na kura 10 ziliharibika.

Alisema katika nafasi ya Ujumbe wa halmashauri Kuu ya CCM Wilaya waliojitokeza walikuwa wawili aliyepata ushindi ni Agness Rambo (122) huku Maimuna Kimaro akipoteza nafasi hiyo kwa kupata kura 116.

Walipoita bila kupigwa kwa upande wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya ni Zainabu Kigera, Wazazi, Riziki Shabani na Vijana ni Lina Lucas.

Akitoa matokeo kwa washindi ndani ya Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Musoma Mjini, Katibu wa Wazazi Wilaya ya Musoma Mjini, Suzana Sije alisema nafasi ya  Mwenyekiti ilichukuliwa na Koshuma Koshuma aliyewabwaga wenzake wawili kwa kupata kura 120, na Felix Salumu kura 87 na aliyewahi kuwa Diwani kata ya Kamunyonge Deogratius Chrispine aliambulia kura 10.

Nafasi ya Ujumbe Halmashauri Kuu na Mkutano CCM, aliyeibuka mshindi ni Isack Ng’ariba alipata kura 149 huku akiwaacha wenzake kwa mbali sana akiwemo Sabato Manyasi aliyepata kura 56 na Magreth Wambura kura saba.

Mkutano Mkuu wa Wazazi Mkoa, Juma Meko alishinda kwa kura 161 ambapo Twaiba Mkangara akipata kura 51,nafasi ya Mkutano Mkuu wa Wazazi Taifa walishinda ni Stella Manyonyi(123), Ally Jama (122) na Masumbuko Magesa (113),nafasi ya Katibu Elimu, Malezi, Uchumi na Mazingira alipita Phares Maghubu aliyepata kura 37 akiwatuma wenzake wawili Mayagi Ngeja(11) na Vicent Malima (4)

Waliopita bila kupigwa katika nafasi ya wajumbe watatu wa Baraza la Wazazi Wilaya ni Munyu Matara, Jumapili Mbogha na Egdi Manyama.

Naye Katibu wa CCM Wilaya ya Butiama, Mercy Mollel alisema kuwa katika nafasi ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) waliochukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi hiyo  ni wagombea wapatao saba akiwemo Mwandishi wa Habari Eva-Sweet Musiba.