Tuesday, October 15, 2013

WANARIADHA WAMUENZI NYERERE



BUTIAMA

CHAMA cha riadha Mkoa wa Mara, Oktoba 14 mwaka huu, kilimuenzi Baba wa Taifa,Hayati Mwl.J.K Nyerere kwa kufanya mbio ya Kilometa 21 na ushindi kupatiwa zawadi.

Akizungumza mara baada ya Mashindano hayo, Kamishina wa habari na uenezi  wa Chama chama cha riadha Mkoa wa Mara, Eva-Sweet Musiba alisema kuwa Chama kimeamua kufanya mbio hiyo ili kuenzi mchango wa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere katika nchi hii kwa kuleta Uhuru, uzalendo,Amani na Utulivu katika nchi hii.

“ Tumeamua kuunga mkono jitahada za Mwalimu Nyerere alizozifanya katika nchi hii, pia kuipenda michezo,hatukutaka kuwa nyuma kwa michezo ingawaje yeye alikuwa anapenda mchezo wa bao, lakiji sisi tumeamua kufanya hivyo ili kumkumbuka Baba yetu ambaye alikuwa msitari wa mbele katika michezo yote” Alisema Musiba.

Pia alitoa shukurani kwa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara Barrick kwa kuchangia gharama za mashindano hayo na kuwataka wawekezaji wengine, mashirika  ya umma, watu binafsi na Serikali kuunga mkono jitihada za wawekezaji  ili kukuza mchezo huo ambao ndio pekee unalitangaza Taifa hilo kwa wachezaji kuwakilisha Taifa.

Mbio hizo zilizoanza majira ya asubuhi juzi ambapo Mkuu wa wilaya ya Butiama, Angeline Mabula alizianzisha kwa kupuliza kipenga,kutoka  viwanja vya Joseph Kizurira Nyerere kuelekea barabara ya Kiabakari na kurudi.
Mbio hizo zilishirikisha wanariadha wapatao 10 kutoka wilaya za Butiama, Musoma Mjini, Rorya na Tarime ambapo washindi  wa tano bora walipatiwa zawadi zao za fedha taslimu.


Mshindi wa Kwanza Majina yao na fedha zikiwa kwenye mabano ni Mwita Kopilo kutoka Wlaya ya Tarime aliyekimbia 1:05:23 alipewa Sh. (70,000), Mshindi wa pili Juma Issa Wambura wa Tarime aliyekimbia 1:10: 03 alipata Sh. (50,0000), Mshindi wa tatu,Mukama Magesa kutoka Wilaya ya Butiama 1:13:19 alipata Sh. (30,0000) wa nne  na wa tano ,Nyakutonya Berias wa Wilaya ya Butiama 1:20:47 na Chagembe Maira  1:22:00 walipewa Sh. 25,000 ambapo Mkuu wa Wilaya Angelina Mabula alikabidhi zawadi hizo.

Thursday, October 3, 2013

VICENT NYERERE MBUNGE WA MUSOMA ADANGANYA



MUSOMA

MBUNGE wa Jimbo la Musoma Mjini, Vicent Nyerere,(CHADEMA) amewadanganya wanachi wa Jimbo lake kuwa Ikulu ndogo inadaiwa Sh. Bilioni 1,  za gharama za maji  huku Mamlaka ya Maji  safi na taka (MUWASA) ikikanusha vikali kauli hiyo ya Mbunge na kudai kuwa gharama hizo ndiyo bajeti ya Mamlaka yao.
Mbunge huyo ambaye pia ni Mjumbe wa bodi ya Maji hivi karibuni katika Mkutano wa hadhara uliofanyika hivi karibuni katika viwanja wa Shule ya Sekondari  ya Mara alitamka kuwa  Ikulu ndogo inadaiwa Bilioni 1 ambazo gharama hizo wananchi ndio wanaozilipa.

Akikanusha kauli hiyo wakatia kizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Meneja wa Mamlaka ya maji safi na taka Musoma ( MUWASA), Emmanuel Ruyobya alisema kuwa siyo kweli kwamba Ikulu ndogo inadaiwa fedha hizo.

Alisema kuwa Taasisi zinazodaiwa ni Hospitali M.40, Polisi M. 96,Shule za Msingi M.8 jeshi kwa maana ya watumishi na nyuma zo ni Sh. M1.2 na RAS Mara kwa maana ofisi pamoja na Ikulu ndogo ni Sh. M. 10 si Bilioni 1 kama ambavyo Mbunge huyo alidai.


Alisema kuwa MUWASA inaendelea na shughuli zake za maendeleo ikiwa ni pamoja na kuunga wateja wapya kulingana na miundo mbinu iliyopo,pia imepata mkandarasi wa kuweza kujenga mradi mkubwa wa Maji  eneo la Bukanga, Makoko utakaogharimu kiasi cha Sh. Bilioni 41 na utakamilika mwaka 2014.


Mradi huo utakapokamilika utatoa huduma zaidi ya asilimia 95 ya wakazi wa Musoma kwa kuzalisha mita za ujazo 36,000 kwa siku ikilinganishwa na mahitaji ya mita za uajzo 24,000 za sasa.

Alisema kuwa kutokana na kukatatika kwa mabomba,mafundi wanafanya jitihada ili kurejesha huduma hiyoa mbapo leo baadhi ya maeneo yataanza kupata maji.


Wednesday, October 2, 2013

MJI WA MUSOMA WAKUMBWA NA UHABA WA MAJI



MUSOMA


ZIWA Victoria limekuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Mji wa Musoma kutokana na tatizo la ukosefu wa maji katika baadhi ya maeneo ya Mji wa Musoma Mkoa wa Mara, ambapo kwa sasa ni la  takribani siku tano.

Uchunguzi uliofanywa na blog hii, umebaini kuwa wakazi wa maeneo ya kando kando ya ziwa hasa, Baruti, Bweri na Iringo wamekuwa wakichota maji katika ziwa hilo kutokana na kukosa maji ya bomba katika maeneo wanayoishi huku njia mbalimbali za boda boda na baiskeli na vichwa vya  akina mama wakibeba maji hayo kutoka ziwa hilo.

Wakizungumzia suala hilo kwa nyakati tofauti, Mkazi wa Bweri, Gabriel Kambuga Mkazi wa Kata ya Bweri, alisema kuwa kwa sasa wana takribani wiki moja hawajapata huduma hiyo na hivyo kuwalazimu kwenda kuchota ziwani ambapo maji hayo hayana usalama.

Naye mkazi wa Kigera, Edward Patrick aliyefika katika ofisi za Muwasa kutaka kujua   huduma hiyo itarejea lini,alisema kuwa eneo hilo halijapata maji kwa muda wa wiki moja,lakini tatizo lao halihusiani na kutatika kwa bomba Mtaa wa  Nyerere.

Afisa Mahusiano wa Mamlaka ya  Maji safi na Taka Mjini Musoma(MUWASA), Emmanuel Ruyobya  amesema kuwa tatizo hilo limetokana na upanuzi wa barabara ambapo Kampuni ya Kichina imekata mabomba ambayo yanasafirisha maji kwenda kwa wakazi sehemu mbalimbali za mji huo.

“Mabomba yaliyopo yamechakaa sana, na yana miaka kama 50 hivi, sasa yanapokuwa yanahamishwa ili kupisha ujenzi wa barabara yanakatika, hilo ndo tatizo kubwa lililosabisha wakazi hawa kukosa maji,jitihada zinafanywa ili kurejesha huduma hiyo haraka” Alisema Ruyobya

Maeneo ambayo hayana  Maji ni Iringo, Nyamatare, Mkendo kati, Kigera, Kwangwa, Nyakato, Nyasho, kitaji,Bweri na Kiara.