Monday, December 16, 2013
KEGONGA WAOMBA ENEO KATIKA HIFADHI YA SERENGETI
NYANUNGU-TARIME.
WAKAZI wa Kijiji cha kegonga kata ya Nyanungu Wilaya ya Tarime wameiomba hifadhi ya Taifa ya Serengeti kugawa eneo la malisho ya mifugo katika bonde hilo ili kuondoa mgogoro uliopo.
Wakizungumza na waaandishi wa habari waliokuwa na ziara katika maeneo ya bonde hilo wananchi hao wameiomba pia Serikali kuangalia upya mipaka iliyowekwa kwa ajili ya kutenga eneo la hifadhi ya mbuga ya Serengeti na eneo la kilimo na mifugo.
Hata hivyo maisha duni na uelewa mdogo wa sheria mpya kwa wakazi wa bonde hilo ndicho chanzo cha kuwepo kwa migongano kati yao na hifadhi ya Taifa ya Serengeti (Senapa).
Elimu ya ufugaji bora na kilimo inatakiwa kutolewa kwa wakazi wa bonde hilo lililoko Wilaya ya Tarime ambalo linapakana na hifadhi hiyo ili kuondokana na migogoro mbalimbali inayojitokeza katika bonde hilo.
Vile vile imeonekana kuwa Maafisa ugani hawatembelei katika maeneo hayo ili kuwasaidia wananchi juu ya kilimo na ufugaji bora wa kisasa ambao una tija kwa wananchi.
Elimu hiyo itasaidia mfumo wa maisha duni waliyonayo wakazi hao ili kwenda maisha bora kwani wana mifugo mingi ambayo wangeweza kuiuza na kubakiza mifugo michache wangeweza kusomesha watoto wao pia kujenga nyumba bora.
Naye Lucia Mariane alisema kuwa kuwa chanzo ya mgogoro huo ni eneo la kuchungia na kulima ambapo alidai kuwa kwa muda mrefu walikuwa wakilitegemea bonde hilo la Nyanungu kwa shughuli hizo, lakini kwa mujibu wa sheria bonde hilo liko ndani ya hifadhi ya Serengeti hivyo hawapaswi kuendesha shughuli zozote za kibinadamu kwa hiyo endapo watapewa mafunzo wataweza kulima na kufuga kisasa hali itakayosababisha wahitaji eneo dogo.
Monday, December 2, 2013
Mwendesha Pikipiki afariki
MUSOMA.
Mwendesha Pikipiki maarufu kama Boda boda Ibrahim yusuph(17) mkazi wa Kamnyonge Mjini Musoma amegongana na gari uso kwa uso akiwa katika harakati za kujinasua na askari wa usalama barabarani kwa kosa la kutovaa kofia,akiwa anaivaa ambapo aliacha njia na kuifuata gari na kufa papo hapo na pikipiki kuteketea kwa moto kufuatia kulipuka kwa tanki la mafuta .
Ajali hiyo imetokea leo asubuhi majira ya saa moja, karibu na stendi kuu ya mabasi iliyoko Kata ya Bweri Manispaa ya Musoma ikihusisha gari lenye namba za usajiriT816 CLS lililokuwa likitokea makutano kuelekea mjini Musoma.
David Goodluck ni shuhuda wa ajali hiyo ambaye ni dereva wa daladala iendayo Wilayani Butiama alisema ameshangazwa na baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo badala ya kutoa msaada kwa majeruhi waliokuwa katika gari hiyo na aliyepoteza maisha ,walianza kuchangamkia samaki zilizomwagika katika mfuko na kutapakaa barabara nzima.
.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara ,SACP Ferdinand Mtui amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)