Wednesday, April 16, 2014

BALOZI CHINA AENDELEA KUDUMISHA UHUSIANO




Ilikuwa wiki ya shamra shamra katika Mkoa wa Mara kwa kupata ugeni mzito kwa mara ya kwanza, kutoka China, Balozi wa China Dk. Lu Youqing katika Wilaya za Musoma, Rorya Tarime na Butiama.

Akiwa Manispaa ya Musoma alizindua urafiki kati ya Mji wa Xiang Tan kwa Rais Mao Zedong aliyekuwa Rais wa China kuanzia mwaka 1949-1976 na Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Baba wa Taifa la Tanzania.

Nia ya ziara yake ikiwa ni uwekezaji katika Mji huu,huduma za elimu na afya bora kwa wakazi wa Mkoa wa Mara.
Balozi ameambatana na maafisa kutoka ubalozi wa China,Taasisi ya Mama Salma ya WAMA ambayo iligawa vyerehani 18,dawa za Malaria, kandambili, mipira,radio aina ya Tec Sun R-102 mini size Am/Fm stereo Receiver kadhaa za walimu.

No comments:

Post a Comment