Saturday, June 3, 2017

EWURA yawataka wazalishaji wa Gesi kupunguza gharama za mtungi.

BUTIAMA.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imewataka wafanyabiashara wa mafuta ya gesi asilia kupunguza kiwango cha kununua gesi kwa watumiaji ili wananchi wa kipato cha chini waweze kuhimiri bei ya gesi na kuwasaidia katika kupunguza matumizi ya ukataji miti ovyo unosasabisha kutoweka kwa uoto wa asili ambapo kwa sasa watumiaji wa mkaa wanaongezeka na kusababisha mazingira kuharibika.


Akizungumza na waandishi wa habari katika banda la Mamlaka hiyo, kuwanja wa Mwenge-Mwitongo Wilaya ya Butiama, Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) Kanda ya Ziwa,Nyirabu Musira,amesema kuwa upunguzaji wa bei utasababisha upungufu wa matumizi ya mkaa ambao ulikuwa ukitumiwa na wananchi.

Hii ni katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani ambayo kitaifa inafanyika kijijini Mwitongo Wilaya ya Butiama alipolelewa na kuzikwa hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Leo kuna kongamano la hifadhi ya Mazingira linaloendelea katika Ukumbi wa Romani Katoliki jirani na kanisa alilokuwa anasali Baba wa Taifa, ambapo Waziri wa Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba.

No comments:

Post a Comment