Thursday, November 30, 2017
MJUE MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM MKOA WA MARA (Musoma Mjini)
Mmiliki wa Blog hii akiingia katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Mara, amechaguliwa kuwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Mkoa wa Mara kutoka Wilaya ya Musoma, na alishinda kwa kishindo katika nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa, ikiwa ni Wilaya moja ya Musoma, ikiwa imeungana na Musoma Vijijini ambayo ni Wilaya kichama kwa sasa.
WAGOMBEA WAKIJINADI.
Wegesa Hassan Witimu akipiga magoti kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT Mkoa wa Mara, kuomba ridhaa ya kuwa Mwenyekiti,katika uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa CCM, Mkoa wa Mara, Wilaya ya Musoma Mjini.
WAJUE WAGOMBEA WA UWT MKOA WA MARA.
Wagombea wa nafasi ya kiti cha Umoja wa Wanawake(UWT) Mkoa wa Mara, wa kwanza ni Veronica Mwijarubi Kunenge(138), Mwajuma Hamisi Magoti(55) na Wegesa Witimu akishinda kwa kura 245.
Sunday, November 19, 2017
MAONESHO YA KILIMO MSETO MUSOMA-MARA
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adamu Kigoma Malima, akikagua mabanda ya maonesho katika viwanja vya VI- Agro forest,Bweri Musoma.
KILIMO MSETO-MUSOMA
MKUU wa Mkoa wa Mara,Adamu Malima, amesema kuwa ili kuendeleza kilimo cha mkataba cha pamba katika Mkoa wa Mara haina budi kushirikiana kwa dhati kwa vikundi vya wakulima kuwa pamoja na kuhakikisha kilimo cha pamba kinakuwa kwa kasi kwa maendeleo ya Mkoa wa Mara.
Akizungumza katika kilele cha maonesho ya kilimo mseto kwa niaba yake,yaliyomalizika jana Afisa kilimo Mkoa wa Mara, Dennis Nyakisinda alisema kuwa ili vikundi vya wakulima viweze kupata tija ya kilimo bora haina budi kituo cha sasa kilimo Mseto cha (Vi Agroforestry) cha na kanisa la AICT Dayosisi ya Mara na ukerewe kiwe kituo cha mafunzo ya kilimo mseto cha Mkoa wa Mara ambacho kitakuwa kitovu cha mafunzo ya kilimo bora na ufugaji.
‘’Kituo hiki kitakuwa kitakuwa bora cha mfano kwa masuala mbalimbali jinsi ya kupanda miti,kutambua majina ya miti, ufugaji, ukulima wa kisasa kwa ajili ya maendeleo ya mkoani hapo na nchini kwa ujumla’’Alisema Nyakisinda.
Aidha alitaka Shirika la viwanda vidogo vidogo(SIDO) Mkoa wa Mara kuhakikisha linawashaidia wajasiliamali ili wapate uwezo kwa kupata ujuzi ili waweze kuanzisha vyao wenyewe kwa ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Amesema ili kukabiliana na changamoto za tabia nchi hawana budi kuzingatia kilimo mseto ambacho ndicho kilimo pekee chenye tija.
Ameongeza kuwa wakati huu ni wakati wa mapinduzi ya viwanda na kwamba kilimo mseto ndiyo injini pekee ya maendeleo ya mapinduzi ya viwanda nchini na kwamba wakulima hawana budi kushirikiana na mashirika mbalimbali ili kuweza kufanikiwa katika kukuza uchumi wa viwanda na kuyataka madhehebu mengine kuiga mfano wa kanisa la AICT kwani bila kuwa na chakula hakuna ibada.
Amewashukuru wafadhili wa Shirika la Vi Agroforestry la nchini Sweden na Kanisa la AICT la Dayosisi ya Mara na Ukerewe kwa kuwa kipaumbele kwa kuchangia nguvu kubwa ya kupanda miti ili mkoa huo uwe na mandhari nzuri na kuzitaka na taasisi nyingine kuwaunga mkono.
Maonesho hayo ya kilimo cha mseto ya siku tatu alipambwa na mabanda ya maonesho ya bidhaa mbalimbali zikiwemo, utengenezaji wa mkaa wa udogo uliochanganywa na kinyesi cha Ng’ombe, ufugaji wa kuku wa kienyeji kwa njia ya kisasa,utengenezaji wa sabuni ya maji, mche na mbegu bora aina ya Mkombozi.
Subscribe to:
Posts (Atom)