Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutia saini Mswada wa sheria ya Uchaguzi Mkuu, Bado kuna vichwa visivyo sikia la Mkuu,ambao pamoja na Rasi kuzungumzi rushwa vichwa hivyo vimekuwa vigumu na vinaendelea kumwaga pesa katika majimbo ambayo vitakwenda kugombea.
Hii ni hatari sana katika nchi yetu yenye demokrasia na vyama vyingi, ambapo
Pamoja na Rais kukemea vikali rushwa wanaendela kuwmaga pesa ili wapewe kura na wanachi ambao hawajua nini cha kufanya aizdi ya kupokea pesa zao.
Kwa bahati mbaya hasa wale walioko vijijini wamekuwa wakipewa pesa hizo maskini ya Mungu bila wao kujua kuwa haki zao zinakwenda bure bila mafanikio yoyote,, na kwa kuzingatia pesa ya muda tu ambayo si chochote wala lolote.
Najuta kusema hili na kusikitika sana kwa kuwaRaisi wetu amekuwa muungwana sana kuhakikisha kuwa hata wasionacho waweza kuongoza na kuliongoza Bunge kwa uadilifu wa hali ya juu na kuwajali masiki kabisa walio na kipato cha chini kwani wafahamu kuwa wao pia walipaya uongozi kwa ridhaa yao.
Sasa hao wanaotoa pesa wanataka nini? na walikuwa wapi kuasidia wanachi wakati ule ambao hawakuwa nacho.Tatizo za viongozi wetu nikiwemo na mie ambaye hivi karibuni nitatangaza rasmi nia hukju mjini Musoma,Tusiwashau na tusijishau kurudi majimboni tupatapo uongozi, ili tuweze kuwasidia wenzetu ambao waliotupatia ridhaa ya kuingia madarakani.
No comments:
Post a Comment