Friday, May 6, 2011

MAPENZI NA SHULE

BY:BELDINA NYANKEKE

MUSOMA.

Schoolgirl pregnancies is the problem that growing daily and it needed serious measures to end it so that to allow girls to accomplish their educational goals.

In Mara region it is difficult to punish those who involving in impregnated school girls since they get support from parents who normal want the matter to be solved out of police or other responsible organs.

Some people who interviewed by The Citizen say that some parents use their children’s pregnancies as source of income by explanation that a person who involving in the matter is ready to pay some amount so that the issue could be settled at family level.

They say that once a person is mentioned by a girl that he is the one who impregnated her they are ready to settle the issue out of court since he believes hat when the parents of the girl will file the case probably he will have a case to answer.

“It is difficult to take measures on those who involving in the matter since most of parents here prefer to settle the issue out of court” says Bwire Masau

Mr Masau says that the situation is due to the habit that some residents of the region have by explanation girls’ education has not given a priority in some community in the region.

He says that some parents are happy after noting that their daughter is pregnant since they know that she will no longer go on with her studies and instead she will get married so that the parents will dowry.

Speaking to The Citizen a the Executive Director for ABC foundation a Non Governmental organization that deals with women and children’s right in Musoma Municipality Mr Justus Nyarugendo says that it is difficult to file make a person who involve in school girl pregnancies since there is no corporation between parents and women rights organizations.

He says that many parents tend to seek help from the NGOs that deal with children and women rights only if the accused refuted to settle the matter out of court by paying some money to the parent of student.

He says that parents also use those NGOs as the place where they can threaten accused so that the accused will be ready to provide the amount they have been asked by parents so that to end the matter.

“They use these NGOs to threaten the accused so once a person heard that the matter has been presented to NGO he will try his level best to convince the parents so that to bring back at the family level the issue so that to be discussed and find solution” he explains

He adds that many NGOs that deal with children rights face hard time to fire those people who involve in school girls pregnancies by explanation there is no cooperation between parents, schoolgirls and NGOs.

He says that if the habit will not be ended the situation might be worse since men will use the opportunity to destroy girls’ future.

Mr Nyarugendo says that it is needed joint efforts from government and other stakeholders to educate residents of Mara region on the importance of girls education so that they could be able to take measures when their schoolgirls are impregnated.

He gives an example of a patron (46) of club which deals with the mitigation of women rights in Musoma municipality who allegedly to impregnate a 13 years girl and then the parents of the girl decided to settle the issue locally.

He explained that accused impregnate the girl last year when she was in standard seven whereby she did her standard seven national exams and then she selected to join Nyasho Secondary in Musoma Municipal but she failed to do so due to pregnancy.

Mr Nyarugendo says that previously the parents of that girl decided to bring the issue to his office so that his NGO to look on how it can help him but when they are in the process of filing case at the court the father of girl disappeared and when they contacted him he refuted to give corporation.

He says that due to that they failed to go on with the process since there was no cooperation between his office and the parents of the girl and that they decided to investigate the reason behind the issue.

He said that later they recognized that the accused gave Sh 300,000 to the parents of the girl so that to end the case locally.

“This is a good example of parents within the region at large and we have experience difficulties in dealing with school girls pregnancies” he insists

according the report submitted by the assistant Mara Regional Secretary Mr Reginald Kombania during the regional Consultative (RCC) meeting held in Musoma recently 632 schoolgirls from Primary and Secondary Schools in the region were forced to left schools after they were being impregnated between2006 and 2010.

Mr Kombania said that during the period 373 school girls from Primary schools were impregnated while 259 girls were from Secondary Schools.

He said that the Musoma District council is leading in the region by having big number of schoolgirls who were impregnated whereby he explained that during the time 190 from Primary schools were impregnated while 145 students were from secondary schools from the district.

He added that, Musoma Municipal has the less number of students who were impregnated whereby he said that during the time 16 school girls from Primary Schools were impregnated while nine girls were from secondary schools within Municipality.

Mr Kombania said that pregnancies is the big challenge that facing education sector in the region the situation that he said that has lead to girls to not achieve their educational goals.

He said that due to that regional authority has directed district authorities to take serious measures on those who impregnate and marry school girls as the way of reducing and ending the problem.

He said that regional authorities have distributed an Education Act No 25 of 1978 to all leaders and from district up to ward levels so that they can start implements it.

He added that all districts were ordered to search for all people who involved in the matter and make sure that they appeared before court so that they can be a lesson to other people.

He said that all districts authorities were ordered to search for all school girls who were married but they don’t have pregnancies so that to back them at schools to continue with their studies.

Mr Kombania said that in order to end the problem districts have to put strategies of building hostels at each secondary schools so that to accommodate all girls the situation that will help them to not to rent rooms at areas which are not friendly to them.


WANASIASA WAPEWA ONYO!!!

MUSOMA.

KAIMU Mkuu wa Mkoa wa Mara,John Henjewele amewaharisha viongozi wa vyama vya siasa kutotumia nafasi yao vibaya kwa kuwashawishi wananchi kukataa kutenga maeneo yao yaliyoko vijijini kwenda mijini kwa kuofia kupoteza mamlaka yao kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wamekiuka utekelezaji wa sera na sheria ya Ardhi ya vijiji namba 5 ya mwaka 1999.

Akifunga semina juu ya utekelezaji wa sheria ya ardhi ya vijiji ya namba 5 ya mwaka 1999 kwa viongozi wa Mkoa wa Mara alitoa tahadhari hiyo mara baada ya kuzuka mijadala kutoka kwa wenyeviti wa halmashauri kuwa hakuna haja ya kuongezwa vitongoji kuja mjini kwa kuwa tayari mji umekwishajaa.

Akitoa hoja katika semina hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Musoma vijijini Magina Magesa alidai kuwa hakuna haja ya kumega kata zilizoko vijijini kuja Manispaa ya Musoma kuwa wananchi hawana miundo mbinu inayostahili na Kwamba kata hizo endapo zitaletwa mjini,watakuwa na hofu kwa kuwa kipato chao kinategemea ufugaji na kilimo.

Akitoa mada juu ya upanuzi na kukua kwa Miji,Afisa mipango miji Mkuu,wa wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mganga Majura alitanabaisha taratibu za kuzingatia wakati wa upanuzi wa miji kwa mujibu wa sheria kifungu kwa kifungu alisema kuwa Katika kifungu Na. 7(1) hubainisha kuwa kila mamlaka husika ni mamlaka ya upangaji katika eneo lake la utawala.

Pia Katika kifungu Na. 7(2) hutamuka waziwazi kuwa Waziri wa Serikali za Mitaa ndie mwenye mamlaka ya kuamua kupanua mipaka ya miji hapa nchini na kifungu Na. 7(3) hubainisha kwamba endapo kuna vijiji vitamezwa na mipaka mipya ya mamlaka yeyote basi vijiji hivyo vitatakiwa kufutwa katika daftari ya usajili wa vijiji kwanza.

Aidha, katika kifungu Na. 7(4) inamtaja Waziri mwenye dhamana na masuala ya Mipango miji kuweza kutangaza katika gazeti la umma ingawa baada ya kushauriana na Waziri wa Serikali za Mitaa, chombo chochote kuwa mamlaka ya upangaji au shirika na kinginecho

Aliongeza kuwa vifungu mbalimbali vya Sheria hiyo pia hubainisha majukumu mbalimbali ya Mamlaka ya Upangaji inatakiwa kuyafanya na katika kifungu Na. 8(1) kinamtaja Waziri mwenye dhamana na Mipangomiji kuwa na mamlaka ya kutangaza katika Gazeti la umma eneo lolote la ardhi kuwa eneo la kupangwa (declaration of planning areas) .

Alisema kuwa katika kutekeleza sera ya umilikishwaji wa ardhi vijijini wananchi wawe na uwezo wa kupata cheti cha ardhi na kila kijiji kuwa na daftali la kijiji ili kubainisha ardhi inayomilikiwa na kupima mipaka ya kila kijiji Tanzania Bara hatua kwa hatua.

Kata ambazo ziko Wilaya ya Musoma vijijini ambazo zitaingizwa mjini ni pamoja na Nyankanga, Nyakatende, Etaro na Nyegina.

Akichangia mada juu ya uhawilishaji,Afisa ardhi kutoka Wilaya ya Bunda,Dennis Masami alionyesha wasiwasi wake juu fidia kwa kuwa na mlolomgo mrefu na upatikanaji wa fedha kutoka serikalini za kuweza kugharamia utekelezaji wa zoezi hilo.

“Kuna tatizo kubwa kwa mabaraza kwa kuwa hayana nguvu ya kisheria kutoa maamuzi katika maeneo yaliyopimwa na mabaraza yanaongozwa na watu wasio kuwa na taaluma ya sheria,ufanisi wa kuweza kutekeleza mjaukumu yao kwa kuwa hauna utaratibu mzuri wa malipo ya kazi zao”Alisema Masami.

Akitoa wito alisema kuwa sheria ya baraza la kata ifanyiwe marekebisho ili baraza lipewe wataalamu wenye taaluma ya sheria,pia Wenyeviti na wajumbe wake waajiriwe na serikali kwani itapunga kero nyingi ambazo kwa sasa wananchi wanakabiliana nazo.

Kaimu Mkuu wa Mkoa huyo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, John Henjewele aliitaka wizara kutoa kipaumbele kwa Mkoa wa Mara kwa kuwa migogoro mingi ya ardhi iko Mkoani hapo hasa katika wilaya ya Tarime ambapo imefikia hatua ya malumbano hata kusabisha ugomvi kutokana na ardhi.,Sanjali na mafunzo zaidi kwa wataalamu ili waweze kutatua migogoro ya ardhi ambayo ni kikwazo kikubwa mkoani humo.

Wizara ya nyumba na maendeleo na makazi ilianza kuhamasisha na kuwezesha mikoa na wilaya ili kuanza utekelezaji katika vijiji ili umilikaji wa ardhi kimila vijijini kurasimisha ardhi kuwa mtaji hai ambapo wamiliki wa ardhi wapewe hatia za kumiliki ardhi kimila na kuboresha usalama wa kumiliki ardhi zao.


UJUE UPANUZI WA MIJI (MADA)

UPANUZI NA KUKUA KWA MIJI

By: MAJURA, MCW
AFISA MIPANGOMIJI MKUU
WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI


MTILIRIKO WA MAWASILISHO
• .
TAFSIRI AU MAANA YA MIJI (MAKAZI - HUMAN SETTLEMENTS)
• 2. KILICHOMO AU KINACHOFANYA MIJI
• 3. HAJA YA UWEPO WA MIJI
• 4. NGAZI MBALIMBALI ZA MIJI KINADHARIA
• 5. HATUA MBALIMBALI ZA MAKUZI YA MIJI
• 6. SABABU ZINAZOLETELEZA MIJI KUKUA
• 7. FAIDA ZA MIJI KUKUA
• 8.SHERIA, SERA NA KANUNI ZINAZOSIMAMIA MAKUZI NA MAENDELEZI YA MIJI NCHINI
• 9. TARATIBU ZA KUFUATA KATIKA KUPANUA MIJI KWA MUJIBU WA SHERIA NA NJIA MBADALA ZINAZOWEZA KUTUMIKA KUIPANUA
• 10. HITIMISHO.

TAFSIRI YA MJI
• 1. Mji au makazi ya watu ni sehemu yenye mkusanyiko wa watu na shughuli zingine zinazoendana na uendeshaji ya mikusanyiko hiyo ili kuiwezesha kujiendesha bila kuathiri uwepo wake.
• 2. Dhana ya mji endelevu inayopigiwa chepeo siku hizi na wataalamu mbalimbali inatokana na kutambua kuwepo kwa shida zitokanazo na uharibifu wa mazingira ukisukumwa na ubinafsi uliokithiri wa wanadamu wa leo ambapo kila mmoja anataka kujinufaisha pekee yake kadri inavyowezekana.

NINI KILICHOMO MIJINI
Ili mji uweze kuonekana na kufanya kazi za kimji unatakiwa uwe na shughuli zifuatazo (au baadhi yake) aghalabu kwa uwiano fofauti tofauti kulingana na kusudi la kuanzisha mji husika:
1) ViwandaSehemu ya kuishi watu (makazi halisi)
2) Huduma za umma (maofisi mbalimbali)
3) Burudani (michezo, maeneo ya wazi, makaburi nk.
4) Biashara nk.

HAJA YA KUWEPO KWA MIJI
Ø Miji ni vitovu vya ustaarabu na kuchochea maendeleo (vyuo vya mafunzo na utafiti)
Ø Miji husaidia kuwahifadhi watu wengi kwa pamoja katika eneo moja kwa madhumuni maalumu kama kambi ya wafanyakazi katika viwanda, ofisi na kutoa huduma kulingana na shughuli kuu
Ø Miji pia imetumika kwa nyakati mbalimbali katika historia kama ngome ya kulinda watu dhidi ya maadui nk.

NGAZI ZA MIJI KINADHARIA (Hierarchy of Settlements):
Makazi au miji inagawanywa katika makundi mbalimbali kufuata vigezo tofauti tofauti
u Vitongoji (hamlets)
u Vijiji (villages)
u Miji Midogo (Trading Centres)
u Miji (Towns) Manispaa (Municipalities)
u Majiji (Cities)
u Metropolitans
u Mkusanyiko wa majiji chini ya uongozi mmoja (Mega Cities).



HATUA MBALIMBALI ZA MAKUZI YA MIJI
Miji yote, isipokuwa michache iliyoanzishwa kwa makusudi na kwa kutumia nguvu, raslimali maalumu na misukumo ya kisiasa, inapitia katika taratibu, mifumo na mielekeo inayofanana. Hapa inamaana kwamba karibu miji yote huanza kama vijiji, miji midogo na hatimaye kufikia hadhi kubwa za nyakati hizo

SABABU ZINAZOLETELEZA MIJI KUKUA
Kuna sababu nyingi zinazosukuma miji kukua:
Ongezeko la watu wanaokaa katika mji husika
Maamuzi ya kisiasa kuipanua au kuanzisha miji fulani kwa makusudi maalum
Kuongezeka kwa shughuli (biashara, viwanda au kupatikana kwa miundombinu madhubuti kama reli na barabara) nk.


FAIDA ZA MIJI KUKUA
Ongezeko la thamani ya ardhi (increase of land value)
Matumizi ya ardhi kwa manufaa zaidi ya wakazi wa miji husika (Optimum utilization of land resources)
Kuwezesha utoaji huduma za kijamii na kimaendeleo kwa gharama nafuu zaidi za kiuendeshaji (economies of scales)


SHERIA, SERA NA KANUNI MUAFAKA HAPA NCHINI
Sheria ya Mipango miji na Vijiji ya mwaka 1956 (Cap 378) iliyokuwa ikitumika baada ya uhuru na kuendelea
Sheria ya Mipango miji Na. 8 ya mwaka 2007 kimsingi inayotumika sasa kwa kiwango kikubwa
Sera ya Mipango miji ya mwaka 2000
Sheria ya Serikali za Mitaa Na. 4 ya 1999
Sheria ya Mazingira Na. 191 ya mwaka 2004
Sheria na Sera za Sekta mbalimbali zinazohusiana na maendelezi ya miji
Kanuni zilizotungwa kusimamia na kufafanua sheria mbalimbali husika katika utekelezaji wake.


NGAZI ZA MIJI ZINAZO TAMBULIKA KISHERIA NCHINI
Ngazi za miji zinazotambulika kisheria nchini ni:
v Vitongoji/Vijiji (Minor Settlements)
v Miji midogo (Townships)
v Miji (Towns)
v Manispaa (Municipalities)
v Majiji (Cities)
v Mkusanyiko wa Majiji (Meg cities).

TARATIBU ZA KUZINGATIA WAKATI WA UPANUZI WA MIPAKA YA MIJI:
Sheria Mipangomiji Na. 8 ya mwaka 2007
Ø Katika kifungu Na. 7(1) hubainisha kuwa kila mamlaka husika ni mamlaka ya upangaji katika eneo lake la utawala
Ø Katika kifungu Na. 7(2) hutamuka waziwazi kuwa Waziri wa Serikali za Mitaa ndie mwenye mamlaka ya kuamua kupanua mipaka ya miji hapa nchini Katika kifungu Na. 7(3) hubainisha kwamba endapo kuna vijiji vitamezwa na mipaka mipya ya mamlaka yeyote basi vijiji hivyo vitatakiwa kufutwa katika daftari ya usajili wa vijiji kwanza
Ø Aidha, katika kifungu Na. 7(4) inamtaja Waziri mwenye dhamana na masuala ya Mipangomiji kuweza kutangaza katika gazeti la umma ingawa baada ya kushauriana na Waziri wa Serikali za Mitaa, chombo chochote kuwa mamlaka ya upangaji au shirika na kinginecho
Ø Vifungu mbalimbali vya Sheria hiyo pia hubainisha majukumu mbalimbali Mamlaka ya Upangaji inatakiwa kuyafanya
Ø Katika kifungu Na. 8(1) kinamtaja Waziri mwenye dhamana na Mipangomiji kuwa na mamlaka ya kutangaza katika Gazeti la umma eneo lolote la ardhi kuwa eneo la kupangwa (declaration of planning areas)


HITIMISHO
Utaona kuwa miji kama walivyo wanadamu hupitia hatua mbalimbali za kukua na kwamba tupende tusipende itaendelea kukua ingawa kwa uwezo tofauti tofauti kulingana na lishe ipatikanayo.
Hivyo mamlaka husika zina wajibu wa kuelewa hatua hizo na kuzisimamia kikamilifu na kwa wakati

Thursday, May 5, 2011

MEYA WA MANISPAA YA MUSOMA AMPIGA MAMAYE

NA GHATI MSAMBA
MUSOMA.

MSTAHIMIKI Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurura,amemshambulia Mama yake kwa kumchapa kwa viboko kwa kutumia fimbo maeneo ya makalio,Mgongoni na sehemu nyingine za mwili wake kwa kosa la kukutwa na watu wa jinsia ya kiume ambao hawakufamika majina na mahusiano yao.

Akizungumza na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari Mama wa meya huyo,Scholastika Malima alisema tukio hilo lilifanyika Aprili 26 mwaka huu (Jumanne) majira ya saa 1.30 usiku nyumbani kwake mtaa wa Nyamatare Mjini Musoma.

Alisema kuwa kisurura alimkuta na wanaume wakiwa wamekaa na mama yake na kumwuliza kwanini anapeleka wanaume katika nyumba hiyo wakati aliishamuzuia na alipomjibu kuwa hawa wameniletea simu ili aione kama inafaa kwa kuinunua ndipo alipochukua fagio na kumtumia na kuchukua fimbo na kuanza kumpiga nayo.

Kwa mujibu wa Mama Malima alisema kuwa purukushani hizo zilisaidiwa na wanae wawili wa kiume ambao hata hivyo hakutaka kutaja majina yao, na kufanya maamuzi ya kwenda kwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Mara Sekondari,Julius Manyori ambaye alichukua hatua kwa mujibu wa sheria ya kuandika barua kwenda kituo cha polisi,barua ya tarehe 27.4.2011 ambayo haina kumbukumbu namba lakini ina muhuri.

“Lakini baada ya kuwasiliana na simu na Mwanangu aishiye mkoani Arusha alinishauri niesinde kituoni na badala yake tuzungumze na tuyamalize kifamilia.’’alisema mama huyo.

“Nashangaa huyu Meya amekuwa akinisumbua sumbua mara kwa mara lakini sijawahi kumchukulia hatua yoyote kutokana na kutokuwepo ushahidi lakini kwa siku hiyo aliyonipiga walikuwepo wanangu wawili wa kuzaa”,Aliongeza.

Alidai kuwa yeye alishazoa kukaa na watu kutokana na umaarufu wa mumewe wakati alipokuwa akifanya kazi ya uhakimu wakati wa uhai wake na kwamba yeye vile vile alikuwa akifanya kazi ya ualimu.

Licha ya hayo mama kisurura alisema wanamsubiri Meya aweze kurudi kutoka safari ili waweze kutatua kifamilia pamoja na kumlipa pesa zake za matibabu.

Mwenyekiti wa Mtaa Julius Manyori, ambaye pia alihojiwa na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari endapo madai hayo aliyafikisha kwake alikiri kuwa Mama huyo alikwenda kutoa malalamiko hayo kwake na ndipo alipomwandikia barua kwa kuwa kesi hiyo ni ya jinai.

“Nilimwambae aende kituo cha polisi ili apewe hati ya matibabu(PF3),kwa mujibu wa sheria ,lakini sijui amefikia wapi,kwani kazi yangu niliishaifanya”Alisema Manyori

Jitihada za kumpata Msitahimiki Meya wa Manispaa ya Musoma Alex kisurura kuzungumzia suala hili alikata na kuizima simu yake ya mkononi baada tu aliposikia utmbulisho wa kuwa ni waandishi wa habari.

Alisema kuwa Meya kisurura ni mwanae aliyemlea wakati alipoolewa na baba yake yaani mumewe aitwaye Kisurura ambaye kwa sasa ni marehemu ambaye amemlea akiwa mdogo hadi sasa ambapo anaishi nae.


Tuesday, May 3, 2011

HABARI NA GHATI MSAMBA
MUSOMA.

VIONGOZI wa Mkoa wa Mara wamepata mafunzo juu ya utekelezaji wa sera na sheria ya ardhi ya vijiji ya namba 5 ya mwaka 1999.

Akitoa maelekezo ya sheria hiyo katika semina ya siku mbili ya mafunzo hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa uwekezaji wa mkoa wa Mara Naibu katibu mkuu wa Wizara ya ardhi Maria Bilia alisema kuwa lengo ni kuelimisha wananchi na wataaalamu juu ya utekelezaji wa sheria ya asrdhi ya vijiji waweze kupata fursa ya kuchangia na kutoa changamoto zinazojitokeza katika masuala mbalimbali ya migogoro ya ardhi mkoani hapa.

Alisema kuwa katika kutekeleza sera hiyo ya umilikishwaji wa ardhi vijijini wananchi wawe na uwezo wa kupata cheti cha ardhi na kila kijiji kuwa na daftali la kijiji ili kubainisha ardhi inayopmilikiwa na kupima mipaka ya kila kijij Tanzania Bara hatua kwa hatua.

“Ni muhimu kuelewa kuwa ili hati za haki miliki za kimila zianze kutolewa shart kwanza ziwepo masjala za ardhi katika ngazi ya Wilaya na kijiji,kijiji husika kiwe na cheti za ardhi ya kijijimambacho ndicho kinachotoa mamlaka kwa halmashauru ya kijiji katika kusimamia ardhi ya kijiji kwa mujibu wa sheria”alisema Bilia.

Alisema kuwa Wizara ya nyumba na maendeleo na makazi ilianza kuhamasisha na kuwezesha mikoa na wilaya ili kuanza utekelezaji katika vijiji ili umilikaji wa ardhi kimila vijijini kurasimisha ardhi kuwa mtaji hai ambapo wamiliki wa ardhi wapewe hatia za kumiliki ardhi kimila na kuborsha usalama wa kumiliki ardhi zao.

Aliongeza kuwa hali hiyo itafanya wananchi kuwa na uwezo wa kupata fursa na dhamana ya kutumia hati hizo katika vyombo vya fedha ,mahakamani na hata kusomesha watoto wao katika vyuo vikuu vya elimu ya juu.

“Miongozo mbalimbali ya Serikali na chama tawala inahimiza matumizi bora yanardhi ili kuondoa umaikini na kuongeza uwezo wa serikali kutambua kisheria miliki mbalimbali zaardhi na katika uchumi wa kisasa haitoshi kuwa na haki ya kutumia ardhi bila miliki hiyo kutambuliwa kisheria”alisema Naibu katibu huyo.

Bilia alisema kuwa Wazara inaendelea kupanua wigo wa utekelezaji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika utoaji wa elimu kwa uuma na kuboresha usalama wa miliki na matumizi bora ya ardhi na kuratibu uasisi na uanzishwaji wa masjala za ardhi za wilaya na vijiji na utoaji w vyeti vya ardhi,pamoja na hati miliki za kimila kwa wananchi.

Naye Kaimu kamishna msaidizi usimamizi wa ardhi vijijini Suma Mbyopyo malisema kuwa matatizo yaliyosababisha kutungwa kwa sera ya Taifa ya ardhi ni pamoja na idadi ya watu kuongezeka na mifugo,ongezeko la mahitaji ya matumizi ya ardhi ,mashamba,maeneo ya malisho ya mifugo mwamko wa watu kutambua umuhimu wa ardh na uharibfu wa mazingira.

Mkuu wa Wilaya ya tarime John Henjewele ambaye alikuwa mwenyekti wa semina hiyo aliwataka viongozi na wataalam kutumia mafunzo hayo katika kutatua migogoro ya ardhi ambayo ni kikwazo kikubwa mkoani humo .

“kutokana na kutotolewa kwa sheria hizi za ardhi kumeendeleza kuwpo kwa migogoro ya mara kwa mara na kusababisha mapigano ya koo na koo kutoelewana kwani ardhi ni rasilimali mama hivyo itabaki kuwa msingi bora katika kuleta maendeleo yetu”alisema Henjewele.

SEMINA, SHERIA YA ARDHI ZIFIKE VIJIJINI SI MIJINI.


KAIMU KAMISHNA WA ARDHI,ANNA MDEMU AKITOA HOTUBA,KATIKA SEMINA YA VIONGOZI WA MKOA WA MARA,JUU YA SHERIA YA VIJIJI NA 5 YA MWAKA 1999.KATIKA UKUMBI WA UWEKEZAJI ULIOPO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA MARA.