Friday, June 15, 2012

WAHAMIAJI HARAMU WAKAMATWA


JUMLA ya wahamiaji haramu na walowezi  wapatao 319 wamekamatwa kwa kipindi cha Januari- Mei Mwaka huu.

Akizungumza na BLOG hii ofisini kwake, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mara, Jacob Sambai alisema kuwa kati ya hao wapo waliofikishwa mahamakani na wapo walirurejeshwa kwao pia waliotumikia kifungo.

Alisema kuwa kati ya hao wapo Wakenya 259, Wathiopia 44, Warundi nane,Wasomali watatu, Waganda watatu na Wakongo wawili.

Alisema kuwa  hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuwafukuza nchini ambapo waliofukuzwa ni wapatao 197 kutoka nchi mbalimbalimbali na wanaoendelea kuchunguzwa ni 39, waliokutwa ni wakimbizi ni nane, waliofugwa kwa amri ya mahakama ni tisa na kwa wale ambao kesi zao ziko mahakamani ni saba, waliogundulika ni watanzania kutoka na mwingiliano na kufanana kwa lugha kati ya makabila ya Wakurya wa Kenya na Wajaluo wa Kenya ni tisa na walioharalisha ukazi ni 60.  

Alisema kuwa Idara hiyo ina changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na uhalifu wanaofanyiwa wafanyakazi wawapo kazini kuchomwa visu hadharani,Mauaji,  uvamizi wa kutumia silaha hali ambayo inahatarisha maisha yao, ubora na ufanisi wa kazi jambo ambalo watumishi wamekuwa na hofu kubwa ya kufanya kazi huku wakihofia usalama wao.

“Kuna baadhi ya wenzetu si vizuri kuwataja majina yao waliwahi kuvamiwa kwa kutumia silaha,kwa bahati njema walipona na wengine kuchomwa visu wakiwa kazini,madhalani basi limekuja na abiria unawaambia washuke ili wagongewe hati ya kusafiria passport, ghafla anakuja mtu usiyemfahamu anakutaka vidole, mmoja wetu alifanyiwa hivyo, sasa hii ni hatari sana” Alisema Sambai.

Alisema kuwa chagamoto zingine zinazoikabili Idara hiyo ni pamoja na  mwingiliano wa makabila kati ya Wakenya wa kabila la Wajaluo na Wakenya wa kabila la Wakurya ambao wanafanana tabia na  Wakurya Watanzania na Wajaluo wa Tanzania, kwa hiyo inakuwa ngumu kuwatofautisha na kuwatambua kutokana na lugha zao kufanana na baadhi yao wamekuwa na mahusiano ya kindugu, Uhaba watumishi na ukosefu wa nyumba za watumishi.

Aidha kumekuwepo na baadhi ya viongozi wakiwemo wenyeviti wa vijiji na baadhi viongozi wa vyama vya siasa hasa madiwani wamekuwa na asili ya wakenya, hivyo inakuwa ngumu kumtaja mtu ambaye ameingia nchini na anaishi bila kibali kutokana na mahusiano kati yao jambo ambalo limekuwa likikwamisha utendaji kazi.

Ukubwa wa mipaka umekuwa changamoto kubwa kwa idara hiyo kutokana na urefu wake na umbali kwa vituo vya ukaguzi vya Kogaja na Shirati kuwa nje ya mpaka, hivyo ni vyema zikahamishwa ili kuweka ufanisi wa kazi na kufufuliwa  kwa kituo cha Bolega kilichoko Wilaya ya Tarime ambapo awali kilikuwa na msaada mkubwa.

.

Alisema kuwa kwa mwaka huu Idara ya Uhamiaji Mkoa huu imeweza kutoa semina katika Tarafa zipatazo nane zenye kata 56 na vijiji au mitaa 210 katika Wilaya za Bunda Tarafa ya Kikopya na Chamriho, Wilaya ya Rorya Tarafa ya Girango  na Tarafa ya Nyancha, Wilaya ya Serengeti Tarafa ya Logolo na Gurument, Wilaya ya Tarime Tarafa ya Nyancha,vijiji vya Ichange na Inchugu, Wilaya ya Musoma inatarajiwa kufanyika katika Tarafa ya Nyancha na Makongoro.

Semina hizo zilikuwa na  lengo la kuweka ufanisi na kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ambapo namba za simu za viongozi zilitolewa kwao ili kutoa taarifa panapotokea mtu ameingia nchini na anaishi bila kuwa na vibali pia aliwasisitiza viongozi hao kuwapa moyo wananchi kwani wamekuwa na uwoga wa kuwataja wahamiaji haramu kutokana na kuhofia usalama wao wa kuhatarisha maisha.


No comments:

Post a Comment