Tuesday, July 17, 2012

WATU WANNE WAMEFARIKI MMOJA KWA KUJINYONGA

MUSOMA.



WATU wanne wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti likiwemo la kujinyonga na ajali ya gari.

Akizungumza na blog hii, ofisini kwake Kamanda wa Polisi,Kamishna Mwandamizi wa Polisi (SACP), Absalom Mwakyoma alisema tukio la ajali lilitokea majira ya saa 9:40  Alasiri ,Julai 14 ambapo  watembea kwa miguu watatu walifariki dunia katika barabara iendayo Saragana- Kusenyi Suguti.

Alisema ajali hiyo ilihusisha  gari aina ya Jpsum yenye namba za usajili T 752 BQR likiendeshwa na Antony Kusaga(45) mwenye mali hiyo ambaye aliwagonga waenda kwa miguu, Asha Mwero(16) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari ya Suguti Wilaya ya Musoma Vijijini ambaye alifariki dunia siku hiyio hiyo akipata matibabu katika hospitali ya Mkoa Musoma.

Aliwataja wengine wawili waliofia hapo hapo kuwa ni Nyakwesi Mwero ( 15) na Rebina Mwero (4) wote wakazi wa kijiji cha Suguti katika Wilaya ya Musoma Vijijini.

Alikitaja chanzo cha ajali kuwa inasadikiwa kuwa ni mwendo kasi aliokuwa nao dreva na kwamba dreva huyo alijisalimisha mwenyewe katika kituo cha polisi na kwamba tayari amefikishwa mahakamani.


Katika tukio jingine lilitokea Julai 17,asubuhi katika maeneo ya Mahakama kwenye nyumba ya Marehemu Dokta Emmanuel Magoti,  mtu mmoja ambaye bado hajajulikana jina lake mwenye jinsia ya kiume amekutwa akiwa amefariki baada ya kujinyonga ambapo mwili wake umepelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospital ya Mkoa Musoma.


Amewataka wakazi wa Mji huo kwenda katika Chumba hicho kutambua mwili wa marehemu ili mwili wake ukazikwe vinginevyo utazikwa na serikali


No comments:

Post a Comment