Tuesday, July 17, 2012

MUSOMA.


JUMLA ya Wakufunzi wapatao 136 kutoka katika  Wilaya za Mkoa wa Mara, wamepata mafunzo ya Sensa ya watu na Makazi ya Mwaka 2012


Akifungua mafunzo hayo ya siku 12, yaliyoanza Julai 16 katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Mara, Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa alisema zoezi la Sensa halitakwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii kwani makarani wapo kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.

Alisisitiza kwa wananchi kwamba kuwa suala la Msingi ni kwamba kila mtu atakayelala nchini Agosti 25 kuamkia Agosti 26 ni lazima ahesabiwe mara moja tu.
“Ninawaomba wananchi wote mtoe ushirikiano wa kutosha kwa makarani wa Sensa ili kupata taarifa muhimu na sahihi kwa ajili ya mipango endelevu ya maendeleo ya nchi yetu”Alisema Tuppa.Na kuongeza “ kuweni marafiki kwa makarani hapo ili wafurahie kazi yao na matokeo yake yawe mazuri.


Aidha amevitaka vyombo vya dola, kamati za ulinzi na usalama za kila ngazi, Mgambo pamoja na vikundi vya ulinzi wa jadi chini ya dhana ya ulinzi shirikishi vichukue nafasi zao ili kuhakikisha zoezi la sensa linafanyika kwa usalama toka mwanzo hadi mwisho,sanjali na  ulinzi wa vifaa vya sensa.


Aliwataka kufuatilia mafunzo hayo kwa makini na usikivu wa hali ya juu ili hapo baadae wawe walimu wazuri watakaoendesha shughuli zote kwa usahihi na kwamba yapo maboresho makubwa yaliyofanywa katika madodoso na mfumo mzima wa utunzaji wa kumbukumbu kutokana na kukua kwa sayansi na teknolojia kwa kutumia teknojia ya Scanning ijuliknayo kama Optical Mark Reader(OMR)ambayo iliyotumika mwaka 2002.

Teknojia hiyo iliipa heshima kubwa nchi yetu katika Nyanja za kimataifa na kupelekea baadhi ya nchi za kiafrika kujifunza na kuchaguliwa kuwa mjumbe wa kamisheni ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa.


Alitoa pongezi kwa Wilaya ya Tarime ambayo ilitoa ushirikiano wa kutosha katika jaribio la sense iliyofanyika katika kata za Matongo, Nyangoto A na B mwaka 2011, viongozi wa madhehebu ya dini, Vyama vya siasa, Mashirika yasiyo ya kiserikali, Taasisi mbalimbali za Umma na binafsi, vyama vya walemavu,Wazee, vyombo vya habari,Wabunge, Madiwani.


Aliwashukuru pia Wazee wa mila na Koo, viongozi wa serikali za Mitaa, viongozi n awatendaji ngazi ya Tarafa, Kata, vijiji hadi vitongoji na mitaa katika kazi kubwa ya kuhamasisha wananchi wa Mkoa wa Mara ili washiriki katika zoezi la Sensa.

Awali akisoma hotuba yake Mratibu wa Sensa Mkoa wa Mara, Ramadhan Mbega alisema kuwa mafunzo hayo yanashirikisha wakufunza wapatao 136 toka ngazi ya Mkoa na Halmashauri zote n akwamba uchaguzi wa wakufunzi hao ulifanywa kwa umakini wa hali ya juu na hivyo wana imani nao na kwamba wanatarajia kupata matokea chanya mwisho wa mafunzo hayo.


Alisema kuwa lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwatayarisha watendaji wote watakaohusika katika zoezi la kukusanya taarifa kwa kufuata maelekezo kikamilifu kwa uelewa wa pamoja na kutoa ufahamu kwa wakufunzi jinsi ya kufundisha, kutafsiri na kutumia melekezo kwa makrani na wasimamizi, pamoj ana vifaa mbalimbali vya sensa.


Kufuatia sense zilizotangulia Mkoa wa Mara ulikuwa na watu 723,327 mwaka 1978,wanaume 118,476 wanawake 134,534 Mwaka 1988 wakikuwa watu 946,418 kati ya hao wanaume walikuwa 444,446 na wanawake 501,972, ambapo sensa ya mwaka 2002 walikuwa watu 1,362,397 wanawake wakiwa 713,690 na wanaume 649,707

No comments:

Post a Comment