Wednesday, July 25, 2012

MNARA WA MASHUJAA KUJEGWA MUSOMA.

MUSOMA.
Na: Ghati Msamba.



MKUU  wa Mkoa wa Mara, John Tuppa amewataka viongozi n awadau mbalimbali kuhakikisha kunajengwa Mnara wa kumbukumbu ya Mashujaa bila kupuuuza alama mbalimbali za mashujaa zilizopo ikiwemo ya mnara mdogo uliopo sasa.

 Aliyasema hayo katika maaddimisho ya siku ya mashujaa iliyofanyika kimkoa kwenye viwanja vya kanisa la Roman Cathoric (RC) Rwamlimi nje kidogo ya Manispaa ya Mji wa Musoma.

Alisema kuwa zoezi la ujenzi wa mnara mpya likisimamiwa na kuratibiwa ipasavyo mwakani, maadhimisho hayo yanaweza kufanyika katika Mnara mpya kuliko kwenda eneo jingine.

Aliongeza kuwa nia na madhumuni ya kuchagua Mnara mdogo kwa kuwa ina kumbukumbu ya kuanguka kwa ndege tatu za  kivita za Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) zilizoanguka mwaka 1979.

“Hapa  pana nasaba kubwa na maadhimisho hayo kuliko kufanyia kwenye viwanja vya wazi, na kilichotoleta si dhehebu la dini bali ni alama ya Mnara yenye uhusiano na maadhimisho haya”

“Hatuna malipo yanayolingana na ushujaa waliouonyesha mashujaa wetu, hatuna.Tuendee kuwakumbuka na kuwaombea Amen”Alisema Tuppa.

Aliwataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuendelea kufuata nyayo za mashujaa wetu, kulinda hazina za ujasiri, uzalendo, umoja na amshikamano walizotuachia na kutocheza amani iliyopo kwani haikujegwa siku moja  na kwamba  endapo tutadhubutu kuiachia itaondoka mara moja lakini itagharimu muda mwingi na jasho jingi kuirudisha.


Aidha maadhimisho hayo yanayanyika Julai 25, badala ya Septemba 1, 1964 ya kila mwaka  kwani julai 25,1979 ndiyo siku ambayo Taifa la Tanzania liliwapokea mashujaa rasmi waliokuwa wanarudi nchini wakitokea Uganda baada ya kumaliza kazi kubwa ya kishujaa ya kumng’oa nduli Idd Amin Dada, kwa mapokezi yaliyafanyika Nyakanazi  Mkoani Kagera na Septemba 1 ndiyo jeshi jipya la Wananchi wa Tanzania lilipoundwa baada ya jeshi la Zamani lililoridhiwa kutoka kwa wakoloni lilipovujwa.

Mkuu wa Mkoa huyo ameipongeza Parokia ya Ramwilimi na Kanisa Katoliki kwa kuutunza na kuulea Mnara huo na ushirikiano waliotoa kwa Serikali kila ilipohitajika kufanya shughuli  zake katika eneo hilo snajala na madhehebu mengine yalishiriki katika maadhimisho hayo bila kujali mahali maadhimisho  hayo yamefanyika.

Aidha ametaka wananchi kushiriki katika zoezi la sense ya watu na makazi la litakalofanyika Agosti 26 2012 na kuhudhuria kwa wingi ili kutoa maoni ya katiba Mpya pale itakapopita kupokea maoni juu ya katiba hiyo.


Kufanyika kwa Maadhimisho hayo kunatokana na agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Dk. Jakaya Kikwete kutoa maelekezo siku hii isiadhimishwe Mkoa wa Dar es Salaam pekee badala yake iadhimishwe kila Mkoa.

No comments:

Post a Comment