Monday, February 10, 2014




MADUKA zaidi ya 1000 katika Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara, yamefungwa kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mgomo baridi unaotokana na kuletwa kwa mashine ya lisiti kwa ajili ya kutoza kodi (EFD) na ambazo zinadaiwa kuwa ni za gharama kubwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mjumbe wa bodi ya wafanyabiashara Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara,Yusuph Kyenche,anasema kuwa mgomo huo utafanyika kwa muda wa siku tatu na endapo hakutakuwa na mwafaka kwa kukaa meza ya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa watagoma kwa mwezi mzima.


Maduka yaliyofugwa ni pamoja na yaliyoko Mjini Musoma, Kamnyonge, Nyasho, Bweri na Makoko yakiwemo maduka ya dawa muhimu ambayo yanatoa huduma za matibabu lakini upande wa soko kuu la chakula la Manispaa likiwa wazi huku wananchi wakiendelea kupata huduma za vyakula.

Akizungumza na wafanyabiashara hao katika bustani ya Malkia Elizabeth, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Tuppa amewataka wafanyabiashara hao kukaa pamoja na viongozi wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Mara ili kufikia mwafaka.

Baada ya kumaliza kwa kikao hicho viongozi wa wafanyabiashara hao walikaa pamoja na kuchagua viongozi watakaokwenda kuzungumza na Mkuu wa Mkoa na maafisa wa TRA.
Akizungumzia kuhusu usalama wa Mji endapo kutatokea fujo, Kamishina Msadizi wa polisi (ACP) Paulo Kasabago alisema hali ya usalama mpaka sasa ni shwari, na kwamba jeshi hilo limejipange kukabiliana na vurugu zozote zitakazofanyika.


“Sisi tuko imara, ukiwalazimisha ndo utaleta tatizo lakini kama wao wanaona hiyo ni njia bora kufanya hivyo ni sawa wafanye tu mpaka siku watakayoamua kufungua na hakuna atakayewalazimsha kufungua maduka kwa nguvu,tutateseka ila si busara kwa nini tujitese,Alisema Kasabago.



Askari polisi wawili mahututi



ASKARI POLISI wapatao tisa wamejeruhiwa na kati ya hao wawili hali
zao si nzuri,wakati wanashughulikia tukio la ajali ya Bus la Super
Samy lenye namba za usajili T227 CDV,ambalo linafanya safari zake
kutoka Mwanza-Musoma, iliyomgonga mwendesha pikipiki Desderi Charles
ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Kiabakari na kufa papo hapo.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Paulo Kasabago (ACP) amesema kuwa mnamo februari 9 katika kijiji cha Songoma Wilaya ya Butiama barabara ya Musoma-Mwanza Mkoa wa Mara,gari yenye namba za usajili T427 BB6 Mitsubishi Fuso mali ya Kisuka
Igogwe Mkazi wa kiabakari likiendeshwa na Garusi Onyango iligonga gari
la polisi PT.1499 L/Rover Defender mali ya RPC Mwanza.

Kabla ya tukio hilo kuwapata askari hao gari hilo lilikuwa likitokea
Wilaya ya Tarime kuelekea Mwanza ambapo lilikuwa limeegeshwa huku
askari wakiwa wanashughulikia tukio la ajali ya bus hilo ambapo
marehemu alikuwa anatoka shule jirani kuwasalimia wanae na alikuwa
amepanda pikipiki yenye namba za usajili T622 AUS.

Askari hao ni D.2216 RSMJohn, E.212 CPL Esore Mwita, H.3532 PC Dominic
Michael, G.6862 PC Erick, G.5112 PC Emmanuel, G.5900 PC Sebastian,
G.7087 PC Thomas, na G.2227 PC Musa na G.3212 PC Elikana.

Katika tukio hilo watembea kwa miguu wapatao wawili waliokuwa eneo la
tukio waligogwa na kupata majeraha, amewataja kuwa ni Jumanne
Abdalah(39) mkazi wa Butiama na Emmanuel Kubunja (30) mkazi wa Bunda
na wote wamelazwa katika hospitali ya Serikali.

Jeshi la polisi linamtafuta dereva wa Fuso ambaye ametoroka baada ya
ajali hiyo na linamshikilia dereva wa Bus kwa mahojiano ambapo mwili wa
marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Serikali Musoma.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara anatoa wito kwa madereva
kuzingatia sheria za usalama barabarani wakati wanapokuwa wanaendesha
vyombo vya moto.

Saturday, February 8, 2014

Auawa akipambana na Polisi.


MTU mmoja anayesadikiwa kuwa ni jambazi ameuawa na askari polisi katika kijiji cha Nyabisarye Kata ya Bweri Wilaya ya Musoma,majira ya saa moja asubuhi baada ya kupambana na askari akiwa ni SMG moja iliyofutwa namba na imekatwa kitako na mtutu, Marwa Keryoba mwenye umri kati ya miaka 30 na 38 Mkazi wa Kebeyo Sirari.

Marehemu alipigwa risasi baada ya askari polisi kumtaka ajisalimishe ambapo walipiga risasi hewani na kukaidi amri ya askari hao na kuanza kukimbia huku akiwa amebeba silaha hiyo huku akiwarushia risasi, ambapo alifia njiani akiwa anapelekwa hospitali ya Mkoa kwa matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Ferdinand Mtui ikitokea kanda Maalumu ya Tarime na Rorya inasema kuwa katika upekuzi nyumbani kwa marehemu vilipatikana vitu mbalimbali vikiwemo simu za mkononi, CD 2 za picha mbalimbali, deki moja, viatu doti mbili, tochi mbili na mipira ya baiskeli pamoja na bidhaa mbalimbali za dukani.


Marehemu aliuawa kutokana na taarifa zilizopatikana toka kwa mtuhumiwa mwenzake anayeitwa Charles Range au Kichune au Josephat Chacha au Chalres Josephat Msong’o( 38) Mkazi wa Kenyamanyori Kata ya Turwa Wilaya ya Tarime aliyekamatwa tarehe 6/2/ 2014 Mkoani Tanga.

Mtuhumiwa huyo anatuhumiwa kujihusisha na mauaji na unyanga’nyi wa kutumia silaha yaliyotokea Wilaya ya Tarime kuanzia Jan 25-27 mwaka huu na katika mahojiano na polisi mtuhumiwa huyo anakiri kuhusika na matukio hayo pamoja na wenzake.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa kipolisi wa Tarime na Rorya, Justus Kamugisha ametoa shukrani kwa wananchi wa Wilaya ya Tarime na Rorya, Mkoa ya Mara na Tanga kwa ushirikiano katika kuwezesha kukamatwa kwa watahumiwa hao na jeshi hilo litatoa zawadi ya Sh. Milioni moja kwa atakayetoa taarifa za mtu anayemiliki silaha kinyume na sheria.

Aidha ametoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi kutoa taarifa za wahalifu ili kuendelea kuweka Mji wa Tarime na Musoma kuwa salama.