Sunday, January 1, 2017
LADY DJ DEE KUTUMBUIZA DREAM GARDEN-MUSOMA.
MWANAMUZIKI mahili kutoka Mkoa wa Mara, Lady Jay De usiku huu anatoa Burudani kabambe katika Resort ya Dream garden iliyopo katika Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara ambapo atawaburudisha wakazi wa Mkoa wa Mara.
Hapa niko na Mkurugenzi wa Resort hiyo Abbas Chamba ambaye amesema kuwa huduma kubwa itatolewa katika bar hiyo ambayo kwake ameitaja kuwa ni ya aina yake katika Mkoa na Manispaa na yenye sifa kwa kuwa iliweza kujumuisha wagenii wa kitaifa katika Mkutano mkuu wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ALAT mwaka ulioisha ambapo tuzo ya kimataifa ya Tanzania Mayors Award ilifanyika katika ukumbi huu.
Mwaka mpya huu utawafurahisha wakazi wa Mkoa wa Mara waishioo nje na ndani ya nchi kupata burudani ya kipekee kwa kuwa watajumuika na mwimbaji wa kitaifa na kimataifa wa nyimbo za Kiswahili ambaye pia Mkoa wa Mara ndio makazi yake rasmi kwa kuwa ni mzaliwa wa Mkoa huu.
Lady Jay Dee atatumbuiza nyimbo zote alizoziiimba mwaka wa jana ukiwemo 'Ndi, Ndi, Ndi, ulio na washabiki wengi ncbi na nyingine za zamani.
Nao washabiki wa muziki wake bila kutaja majina wamesema kuwa ni mwanamziki anayefaa, na kumtaka achukue wanaziki wengine wenye uwezo ambao wapo katika Mkoa huu, akisemo mwimbaji mwenye sauti mithili ya Kasuku, Abdalla Ukwaju anayeibia bendi ya Magereza ya Mkoa wa Mara.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment