MUSOMA
WAZIRI Wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi
amepiga marufuku ujenzi usio na utaratibu ulio nje ya mpango kazi
kabambe(Master Plan) wa 2015-2035 uliozinduliwa jana katika Manispaa
ya Musoma ambao utagharimu kiasi cha Sh. Bilioni 15 ikiwa na pamoja na
miundo mbinu.
Alisema pia kuwa ni marufuku wananchi kujenga bila kuwa na kibali cha
ujenzi kutoka katika halmashauri za miji, mji na Manispaa na kwamba
watavunjiwa nyumba zao bila kulipwa fidia yoyote.
Aidha aliagiza uongozi wa Manispaa, kitengo cha mipango miji
kuhakikisha inatumia mpango kazi huo na kutumia wataalamu wazalendo
kwa kuwapatia ushauri wa kitaalamu endapo kutakuwa na utata.
‘’Ni marufuku Wizara ya Ardhi kutumia wataalamu kutoka nje kutupangia
mji, zitumike kampuni za kizalendo,kwani tumetumia gharama kubwa
katika kupanga mji wa Mwanza na Arusha kwa kuweka kampuni za kizungu
kwa kiasi cha zaidi ya Bilioni 22, lakini katika kupanga Master Plan
ya halmashauri ya Manispaa ya Musoma kampuni ya kizalendo ya upimaji
CRM Land Consultant zimetumika Sh Milioni 288 na kazi ni nzuri na ni
kitaalamu.
Alisema kuwa serikali iko tayari kuwajengea uwezo kampuni za kizalendo
ili kuweza kupanua wigo wa wataalamu wa nchini ili kupunguza gharama
zisizo za lazima na kuongeza kazi ya urasimishaji ili mji ukae katika
Madhari nzuri.
Amewaagiza watendaji wa mitaa kusimamia kuendeleza miji kwani mji
umepangwa upya kwa kuweka masharti ya uendelezaji wa ujenzi na sio
kufanya kazi moja ya ukusanyaji wa mapato kwani rasilimali zilizopo
zikitumika zitasaidia kukuza uchumi na kutoa hati kwa wananchi ili
ziwasaidie kuchukua mikopo itakayowasaidia kufungua biashara kubwa
ambayoo itawaingizia halmashauri mapato.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Manipaa hiyo Joseph Masero alisema kuwa
Manipaa ya Mji wa Musoma ilipata hadhi ya kuwa Manipsaa mwaka 2005 na
mchakato wa kupata mpango kazi kabambe ulianza mwaka 2013 ambapo
Manispaa ndiyo ya kwanza nchini Tanzania kuwa na mpango kazi kabambe
(Master Plan).
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Vicent Naano alisema kuwa mpango kazi huo
utasaidia kuondoa ujenzi holela ili Manispaa iweze kupata eneo la
ujenzi wa viwanda ili kutekeleza Ilani ya CCM na sera ya serikali ya
kuwa na kuwa na viwanda na kuondoa tatizo la ardhi.
Aidha Profesa John Lupala Mkurugenzi alisema kuwa mara baada ya
kurekebishwa kwa sheria mbalimbali za ardhi mipango ilianza kufanywa
kwa kuanza kuandaa mipango iliyoandaliwa ni 26 katika miji 18
lakini kati ya miji hiyo ni Manispaa ya Musoma pekee ndiyo
imekamilisha mpango kazi (Master Plan).
Mtaalamu Mshauri wa kampuni ya mpango kazi kabambe ya (CRM Land
Consultant),Clara Kweka Msale aliwapongeza wataalamu walioshirikiana
nae kuhakikisha wanapanga mji huo ambapo kazi hiyo ilishirikisha
wadau wote.
Friday, April 28, 2017
WAZIRI LUKUVI AGAWA HATI MILIKI
SIMIYU
WAZIRI Wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi
amewakabidhi wakazi wa mji mdogo wa Lamadi Wilaya Busega Mkoa wa
Simiyu hati miliki za viwanja na kuagiza kuvunjwa kwa nyumba
zitakazojengwa kiholela mara baada ya kukamilisha mpango kazi
kabambe(Master Plan) katika Wilaya hiyo.
Zoezi hilo lililofanyika katika viwanja vya mikutano vya stooni ,
Lamadi wilayani humo lililoshuhudiwa na wananchi, huku akitoa elimu
kwa wananchi walioonekana kuhamasika kuwa na makazi bora mara
watakapopata hati miliki ili waweze itakayowawezesha kukopa na
kufungua biashara zao na kuondokana na umasikini.
Alisema kuwa lengo la serikali la kufanya urasimishaji huo ni
kuwataka wananchi kuweza kupata hati zitakazowasaidia kukopesheka
kwenye mabenki ili kujikwamua kiuchumi .
‘’Rais ameniagiza kuja kurasimisha ili wananchi muweze kupata makazi
yaliyo bora na ili kuondokana na makazi holela na kupata hati miliki
za viwanja ili muweze kukopesheka,ukiwa na hati unakuwa umefunga ndoa
ya halali ambayo ni mkataba halali na serikali ambao utakuwa unalipia
kodi ya ardhi kila mwaka na bila kubugudhiwa na Mkuu wa Wilaya au
Mtendaji wa kata’’. Alisema Lukuvi.
Aidha amewataka wananchi kutumia fursa ya hofa ya punguzo ya kulipia
asilimia 2 iliyotolewa na Rais Dk. John Magufuli katika kufanya
urasimishaji wa mpango kazi kabambe(Master Plan ) ili kuendeleza mji
huo kuwa wa kibiashara ambayo kufikia Juni 30 mwaka huu ndio mwisho
na kuweza kupata hati miliki.
Aliongeza‘’Kuna nyumba nyingi ambazo zimejengwa kiholela lakini rais
ametoa hofa rasmi ambapo leo nimekuja kutoa hati 122 kwa atakae ipata
ndio dhamana itakayomwezesha aweze kukuza uchumi wake ambao ni mtaji
wa maendeleo na kuondokana na umaskini’’.
Akiongea kwa hisia kali alisisitiza‘’ Serikali haiwezi Kuja
kuhalalisha maovu tu kila siku na kurasimisha na kutoa hati kwa
makosa yanayofanyika hivyo tumieni hofa hiyo mliyopewa ili
kuhakikisha wananchi wote wa mji wa Lamadi mnafanya urasimishaji wa
kupata makazi yaliyo bora, ili mpima atakapokuja asilazimike kuvunja
nyumba ili uweze kujenga nyumba upya,lakini kwa hawa waliopata
hati,mpango kazi ukija na ikalazimika eneo lile aidha ni barabara
inapita,italazika alipwe,lakini kama hiyo nyumba utakuwa umejenga bila
kibali itavunjwa hata kama umejenga ghorofa.’’Alisisitiza Lukuvi.
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Busega Anderson Mbiginya akisoma
taarifa ya maendeleo ya wilaya hiyo alisema katika kipindi cha
kuanzia oktoba 2016 hadi sasa halmashauri hiyo imefanya upimaji wa
awali wa miundombinu ikiwemo ya shule, zahanati, malambo, majosho na
mabanio ipatayo 102 kati 180 sawa na aslimia 56.67na kufanya
urasimishaji wa makazi yanayoendelezwa kiholela na kutambua miliki
imekamilika kwa kupata viwanja 5,223 na upimaji wa awali viwanja
4,950.
Alisema umilikishaji wa viwanja ulianza Aprili mwaka huu katika eneo
la Lamadi ambapo hadi sasa hati 138 zimeandaliwa na kati ya hizo 122
zimekamilika na zimekabidhiwa .
Alisema kuwa kupitia urasimishaji serikali imefanikiwa kuongeza
mapato yatokanayo na tuzo na huduma za ardhi kwani zaidi ya shilingi
milioni 22.3 zimekusanywa katika kipindi cha wiki mbili na inakadriwa
kuwa shilingi 315 .4 zitakusanywa ikiwa viwanjwa 1,934 vilivyokamilika
kupimwa vitamilikishwa.
Alisema kuwa licha kuwa na mafanikio hayo kuna changamoto
zinazowakabili ambazo ni umbali mrefu wa upatikanaji wa huduma ya
baraza la Ardhi wilaya ambapo kwa sasa wananchi wanapata huduma ya
baraza la ardhi wilaya ya Maswa ambako ni wastani wa km 150 na
darubini ya kupimia (Total Station).
Nao baadhi ya wakazi wa eneo hilo waliopata hati waliishukuru serikali
kwa kuwaletea huduma hiyo kikanda ambapo kwao ilikuwa ni ndoto.
Akizungumza na gazeti hili, Mkazi wa mji mdogo wa Lamadi, ambaye ni
mwanamke,Lyabubi Gatulwa Mkelebe ambaye alichukua hati 3 alisema hati
hizo atatumia kwa kuweza kukopa benki ili aweze kuongeza hekali 50 za
kulima mpunga kwa njia ya kisasa ambapo kwa sasa ana heka 13 za
mpunga.
Saturday, April 15, 2017
Profesa Muhongo awataka wananchi kuzingatia elimu
MUSOMA.
MBUNGE wa Jimbo la Musoma vijijii na Waziri wa Nishati na Madini Pro. Sospeter Muhongo amewaomba wananchi kuweka jitihada kubwa katika sekta ya elimu kwani ndio pekee itakayoleta manufaa katika kukuza uchumi wa familia na Taifa.
Ameyasema hayo jana katika kijiji cha Bugoji, Muhoji na Chumwi katika ziara yake ya kukgua ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuongea na wananchi katika mikutano ya hadhara ambayo ilifanyika katika shule za msingi za Kanderema .
Aidha amewataka wananchi kutobakia kulalamika badala yake waongeze bidii katika utendaji wa shughuli za maendeleo ikwemo kilimo ili kuweza kuondokana na matatizo mbalimbali ya maisha.
Licha ya hayo akizungumzia juu ya mradi wa maji , aliwaeleza wananchi kuwa katika miradi mingine kama vile maji inasimamiwa na halmashauri na kwamba serikali inafanya kazi kwa mpangilio hivyo madiwani ndio wanapaswa kusimamia suala la maji kwa kuweka katika vikao vyao ili atakaposhughulikia suala hilo iwe rahisi.
Akizungumzia suala upungufu wa chakula amesema ni aibu sana kusema kuwa mna njaa huku mnazungukwa na ziwa,sisi ndo tungekuwa watu wa kwanza kusambaza chakula katika mikoa mingine, lakini kwa sasa ni tofauti, tunaomba chakula kutoka mikoa ya Mbeya,tubadilike kutoka kilimo cha kutegemea mvua na sasa tulime kilimo cha umwagiliaji, kwani shamba kama la Bugwema lipo na halitumiki’’ Alisema Muhongo.
Naye katibu wa Mbunge wa jimbo hilo Ramadhan Juma alisema Pro. Muhongo amekwishaleta vifaa vya ujenzi ambapo jumla ya mifuko ya saruji ipatayo 1269 na mabati 5120 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa shule za msingi 111 na sekondari 20 ambapo mgawanyo wa saruji katika ukanda wa Bukwaya shule 13 kati shule 18 ,ukanda wa mugango 13 kati ya 24, ukanda majita 40 kati ya shule 69.shule 4,majita shule 2.
Subscribe to:
Posts (Atom)