Wednesday, November 30, 2011

AFISA UVUVI MKOA WA MARA LAWAMANI

MUSOMA


WADAU wa mazingira katika Manispaa ya Musoma Mkoa wa Mara wameilalamikia sekta ya uvuvi Mkoani MARA kwa kutokuwa makini katika ufuatiliaji wa vitendo vya uvuvi haramu vinavyofanyika ndani ya ziwa Victoria ambavyo vinasababisha uharibifu wa mazingira,

Hayo wamesema Novemba 29 katika siku ya maadhimisho ya siku ya Ziwa Victoria yaliyofanyika katika ukumbi wa uwekezaji Mkoani Mara ulioko katika Manispaa ya Mji wa Musoma, ambapo walitaka kujua kulikoni zana haramu zinazidi kutumika na kupelekea Samaki wanaovuliwa ndani ya ziwa victioria kutokuwa na kiwango cha kimataifa wakati wanadai kuwa samaki wanaovuliwa wana kiwango cha Kimataifa.

Walisema hata kama wanawapatia semina juu ya utunzaji wa mazingira ya ziwa Victoria lakini iwapo hawatakuwa wafuatiliaji itabakia kuwa maneno ya karatasi tu kwa kuwa mara kwa mara wamekuwa wakitoa semina kama hizo lakini ufuatiliaji wake kwa vitendo umekuwa ni mdogo .

Walimtaka Afisa Uvuvi Mkoa Mara awaeleze kwa nini zana haramu kama makokoro ya kuvulia samaki wachanga,dawa za sumu wanazotumia wavuvi kuvulia samaki bado zinazidi kuongezeka ndani ya ziwa, sehemu madawa hayo yanapouzwa wanapafahamu na hata nyumba wanazohifadhia zana hizo wanazifahamu wakati polisi na BMU wapo kila koma na kazi yao ni nini, huku baadhi yao wakimtuhumu kushirikiana na wavuvi haramu.

Akijibu maswali yaliyoulizwa na wadau hao Afisa Uvuvi Mkoani Mara Apolinary Kyoja alionekana kutokuwa na majibu sahihi ya moja kwa moja ya kuwaeleza wadau hao kulingana na maswali yaliyoulizwa badala yake aliwaomba ushirikiano katika kutoa taarifa.

Kyoja amewataka wadau hao kumsaidia kupambana na wavuvi haramu kwa maana kuwa yeye peke yake hawezi kufuatilia kila mahala kwani hana vyenzo za kutosha za kufuatilia kila sehemu kwa kuwa kila mtu ni mlinzi wa ziwa Victoria.

Amesema kila mtu anatakiwa awe mlinzi wa ziwa hilo kwani hata yeye anao uwezo wa kuzunguka kila mahala kukagua usafi wa ziwa ila anachokiomba kutoka kwa wananchi ni kusaidiana nae ili kutokomeza tatizo la uchafuzi wa ziwa hasa kwa kupashana taarifa pale wananchi wanapoona wavuvi haramu wakitumia zana haramu za uvuvi.

Akizindua semina iliyoendana na maadhimisho hayo ya siku ya ziwa Victoria Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mara ,NDUGU GEOGFEY NGATUNI amesema kuwa wananchi wanatakiwa kutunza mazingira hususani ya ziwa Victoria kwa kuwa maji hayo ndiyo yanayotumika katika shughuli mbalimbali viwandani na kwa matumizi ya majumbani.

Amesema wavuvi wanapoendelea kutumia zana hizo haramu wanasababisha madhara mengi kwa afya ya binadamu na kwa mazingira hali inayoadhili uchumi wa Taiafa letu.

Kauli mbiu ya ziwa Victoria ni Ziwa Victoria ni uhai wetu,mali yetu tuilinde.

ZIWA VIKTORIA LACHANGIA KIPATO KIKUBWA SERIKALINI.

MUSOMA.

ZIWA Victoria linachangia pato la Taifa kwa takribani Dola za kimarekani Bilioni 3 hadi Bilioni 4 kwa Mwaka.

Hayo yamesema Novemba 29 na Katibu Tawala wa Mkoa, Clement lujaji katika kilele cha maadhimisho ya siku ya ziwa Viktoria kitaifa iliyofanyika katika Mkoa wa Mara, Manispaa ya Musoma , iliyofanyika katika Bwalo la Polisi, Mwisenge.

Alisema kuwa ziwa Viktoria ni raslimali muhimu katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na lina hazina kubwa zaidi ya samaki wa maji baridi Duniani.

Aliongeza kuwa samaki wanovunwa kwa mwaka ni kati ya tani 400,000 hadi 500,00o kwa mwaka, sambamba na hilo pia ziwa hilo ni kivutio cha utalii na chanzo cha mto Nile ambao una maporomoko ya Owen, Jinja-Uganda yanayotumika kuzalisha umeme unaosambazwa katika nchi za Uganda, Kenya, Tanzania na Rwanda.

Aidha madhumuni ya maadhimisho hayo ni kuwapa fursa wananchi na wadau wa Bonde la Ziwa Vikroria kukutana ba kuonesha shughuli mbalimbali za kuendeleza bonde hilo na mafanikio yake pia kupata fursa ya kubadilishana uzoefu na kutafakari mbinu mpya za kutimiza azma ya kukuza uchumi wa eneo la nchi wanachama.

Hata hivyo pamoja na nia nzuri ya serikali kukutananisha wadau hao, wengi wa wadau hao hawakuweza kushiriki kikamilifu katika kilele hiki, zikiwemo nchi zinazonufaika na Ziwa hilo.

Alisema kuwa changamoto zinazolikabili ziwa ni pamoja na kuwepo kwa gugu maji, kuongezeka kwa vitendo vu auvuvi haramu wa kutumia baruti na mabomu, uharibifu wa uchafuzi wa vyanzo vya maji na kwamba takwimu zinaonyesha kuangamia kwa ziwa hivyo basi hamna budi kuchukua hatua za makusudi ili kunusuru ziwa hilo.

Miongoni mwa hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kuhifandhi Ziwa Viktoria ni pamoja na kubni na kutekeleza Mradi wa kuhifadhi na kutunza Mazingira ya ukanda wa Bone la Ziwa Viktoria pamoja na ziwa lenyewe liwe sakama na kitovu cha uhai na maendeleo endelevu ya wananchi wa eneo lote la ziwa na viumbe wengine wanaoishi katika ukanda.

Serikali imeweka sheria mbalimbali zinazolenga kutunza mazingira zikiwemo sheria ya mazingira Namba 20 ya Mwaka 2004.

Aidha Mwaka 2009,Serikali ilipitisha Sheria Namba 11 ya Rasilimali za maji na Sheria Na.12 ya huduma za maji safi na Usafi wa Mazingira ambazo zinalenga kulinda na kutunza vyanzo vya maji.

Kifungu cha 52(1) cha Sheria Na.12 ya huduma za Maji na usafi wa mazingira zinatoa adhabu ya faini ya kiwango cha Sh. Milioni 1 au kifungo cha kwenda jela miezi 12 au vyote viwili kwa pamoja kwa mtua yeyote atakayesababisha uchafuzi wa chanzo cha maji.

Awali akisoma hotuba yake kwa mgeni rasmi, Afisa Maji Bonde la Ziwa Viktoria

( LVBWO) ,ofisi ndogo ya Musoma, Jumanne Sudi alitanabaisha kazi zinazofanywa na ofisi hiyo kuwa ni pamoja na kutoa hati ya haki ya kutumia maji,kushughulikia maombi na kutoa vibali vya kutiririsha vya majitaka kwenye ziwa na mito baada ya kuridhika na viwango vya maji hayo kulingana na viwango vilivyowekwa, kukusanya na kutunza takwimu za maji kutoka kwenye miti, ziwa na maji chini ya ardhi kwa ajili ya kuratibui matumizi endelevu.

Friday, November 18, 2011

WATUMISHI WABOVU KUPOTEZA KAZI.

MUSOMA.

MKUU wa Mkoa wa Mara,John Tuppa, amewataka watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Musoma kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kuwa ndicho chama kilichoshinda katika uchaguzi Mkuu na kinachotakiwa kutekeleza Ilani yake huku akiwakemea watendaji wabovu na ambao hawawajibiki katika kazi zao.

Aliyasema hapo jana alipokutana na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma katika ziara yake ya kwanza katika ukumbi wa Halmashauri uliopo katika Manispaa ya Musoma,tangu ateuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Alisema CCM ilishinda na Ilani yake ndiyo inayoongoza na ndiyo yenye kutekelezwa hivyo amewataka kuitekeleza na kuhakikisha watumishi wao wanafanya kazi pasipo kuingiza siasa kwani muda wake umepita na sasa utekelezaji, na kwamba siasa wawaachie wanasiasa wenyewe wakiwa majukwaani.

“Nimekuja leo kunitambulisha kwenu,tufahamiane uso kwa uso kabla sijaanza ziara ya kukutana na watendaji kwani nikachokiomba kwenu ni ushirikiano kwani nyie watumishi mnaoshughulika na wananchi ili mtatue kero zao” Alisema Tuppa.

Alisema kama watumishi wa halmashauri hawatatui kero za wananchi wanachi nao wataichukia serikali yao. “Kila mtu atimize wajibu wake mimi sitaki majungu, sitaki kuona mtu anakuja kwani anipatia majungu majungu kuwa mtu fulani hafai, nitakachofautailia ni ni vitendo vyenu,kama mnafanya kazi, na ukinidhibitishiea kuwa haufai nitaanza na wewe” Alisisitiza.

Aidha aliwataka kuhakikisha kuwa mipango ya halmashauri inakwenda sawa na kupata matokeo chanya na kuwataka kuepuka na hali ya kuwa na hati yenye mashaka kwani Waziri Mkuu ametoa agizo endapo hati itaendelea kuwa ya mashaka atawajibishwa Mkuu wa Mkoa.

“Waziri Mkuu kaniagiza niafatilie vinginevyo ataniwajibisha, kwani mmepata hati ya mashaka, kabla sijaanguka kwenye sementi, naweka godoro, Matatizo yetu tuyatatue wenyewe si kufuatana fuatana kwami kil amtu anajua kilichomleta ni kufanya kazi na ameisomea kazi hiyo, nikikwambia ufanye moja, mbili ,tatu, fanya na kama hukufanya nitakushumshughulikia mtumishi huyo” Alisema Mkuu wa Mkoa.

Akisoma taarifa ya Wilaya kwa Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Dk. Karaine Kunei alisema Wilaya hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula kutokana na chakula chake kikuu aina ya muhogo kukumbwa na ugonjwa wa batobato.

Akizungumzia juu elimu ya elimu ya sekondari alisema jumla ya watoto 376 wa shule mbalimbali za sekondari walipata ujauzito na hivyo kushindwa kuendelea na elimu na kwamba hali ya maambukizi ya vvu katika halmashauri hiyo iko juu kwa asilimia 6.4.


Wilaya ya Musoma ina jumla ya shule za sekondari 42 sita kati ya hizo zikiwa za taasisi mbalimbali na ina kata 43 na vijiji 116.


Mkuu wa Mkoa wa Mara alianza ziara yake ya kikazi juzi ambapo alikutana na viongozi wa vyama vya siasa na kufanya mazungumzo nao, ataendelea na ziara yake katika Wilaya za Bunda, Rorya, Tarime na Serengeti.

Monday, November 14, 2011

HABARI MOTO MOTO KUTOKA WILAYA YA WAJANJA

AGIZO LA WAZIRI TAMISEMI LAKIUKWA

RORYA.

BARAZA la Madiwani Wilaya ya Rorya kwa pamoja limetoa pendekezo la kufanya marekebisho ya haraka katika ujenzi wa wodi la Wazazi lililoko Changuge, kutokana na vyoo vyake kujengwa nje ya wodi hilo,na wajawazito kukosa huduma,kufuatia agizo la Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri alipofanya ziara katika Wilaya hiyo.

Walisema kutokana na kuchelewa kwa uvunjwaji wa ukuta na kutengeneza vyoo upya kwa agizo la Naibu Waziri, Mkandarasi huyo hana budi kuharakisha ujenzi huo kwa kuwa wanawake kwa sasa wanapata taabu ya sehemu ya kujifungua na huku wodi likiwa halina choo na ucheleweshwaji wa Ujenzi upya.

Mkandarasi wa ujenzi huo, Mhini Construction wa Wilaya ya Tarime alipaswa kukabidhi jengo hilo mapema juni 15 mwaka huu,ambapo mradi wa ujenzi wa wodi hiyo ulianza Juni 9 2010.

Fedha ambayo ilikuwa tayari imelipwa ni kiasi cha Sh. M. 35,470,0720,Ambapo gharama kuu ya mradi hadi ungekamilika ilikuwa kiasi cha Sh. Milioni 40.

Lengo la Mradi wa ujenzi wa wodi ya wazazi Changuge ilikuwa kulaza wajawazito walio na uchungu, kujifungua na kutunza watoto ambao wanazaliwa kabla ya muda wao wa kuwaruhusu wazazi kwenda nyumbani wakiwa salama na lingehudumia watu 36 kwa siku endapo lingekamilika.

Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri, alipofanya ziara yake katika Wilaya hiyo Mei 24 mwaka huu alikataa kufungua wodi hiyo kutokana na kutokidhi viwango ikiwa ni pamoja na vyoo vya wodi hiyo kujegwa nje ya wodi na Milango ya wodi hiyo ikiwa na mbao zisizokidhi viwango, na kutoa agizo kwa mkandarasi wa ujenzi huo kutwalipwa fedha zilizobaki na kuhakikisha linafanyiwa marekebisho ya haraka, lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika.



NYAVU ZACHOMWA MOTO.

JUMLA ya nyavu 45 na samaki wachanga aina sangara zenye thamani ya Sh Milioni 4,522,000 zimeteketezwa kwa moto katika oparesheni iliyofanyika katika Wilaya ya Rorya mwezi Agosti na Septemba mwaka huu.

Mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Wilaya ya Rorya, Cosmas Ngangaji kwenye kikao cha baraza la Madiwani kilichokaa hivi karibuni imebainisha kuwa kitengo cha uvuvi,katika doria za ulinzi wa Rasilimali ya uvuvi ilifanyika oparesheni hiyo.

Aidha vituo vya Sota, Nyang’ombe, Kibuyi na Ruhu vikiendelea kupokea samaki aina ya Sangara kutoka kwa wavuvi na kuzipeleka viwandani kwa ajili ya kuchakatwa na kupelekwa kwenye soko la Nchi za Ulaya.

Alisema Agosti 15 nyavu zipatazo 15 aina ya timba zenye matundu ( Mesh) yenye ukubwa wa inchi 3 zikiwa na thamani ya Sh. 1,350,000 zilikamatwa.

Aliongeza kuwa nyavu aina ya timba (Monofilament) zapatazo 18 zenye macho ya 3.1\2 zikiwa na thamani ya Sh. 1,620,000 zilikamatwa pamoja na samaki wachanga aina ya sangara zenye thamani ya Sh. 60,000 zilichomwa moto na samaki ziligawiwa wananchi.

Samaki wengine wachanga aina hiyo hiyo walikamatwa katika kisiwa cha Bugambwa Kibuyi zenye thamani ya Sh. 150,000 ambazo pia ziligawiwa wananchi.

Aidha nyavu zingine aina Monofilament 4 za nchi 3 zenye thamani ya Sh. 360,000 pamoja na samaki wachanga wenye wa Sh. 90,000 zilichomwa moto na samki ziligawiwa wananchi.

Kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ruhu na wadau, Nyavu wa aina ya Timba (Monofilament) za nchi 4.5 zenye thamani ya Sh. 100,000 na samaki wachanga aina ya sato wenye thamani ya Sh. 72,900 zilikamatwa na kugaiwa wanachi na nyavu kuteketezwa kwa moto.

Vile vile mwezi Septemba nyavu zingine nane aina ya Monofilament ya inchi 3 zilichomwa moto,zikiwa na thamani ya Sh. 720,000.

Katika tukio hilo vatu watatu wamefikishwa mahakamani ya Wilaya ya Tarime kwa tuhuma ya kuvua samaki kwa kutumia madawa katika Shauri Na. CC.371/2011 dhidi ya Tumaini Makasa, Amani Makasa, Iddi Obeid na Nyarongo Waryoba, Shauri jingine linasubiri uthibitisho kutoka maabara ya Taifa ya Uvuvi ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani.

Aidha Wilaya ya Rorya ina mkakati wa kuboresha ukusanyaji mapatto kutokana an ada za leseni za uvuvi,biombo vya majini na usajili wa biombo vipya na ulinzi wa rasilimali za uvuvi.

Saturday, November 12, 2011

UKAGUZI WA SHULE WILAYA YA RORYA ZERO!!!!

RORYA.

Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Rorya, Cosmas Ngangaji, amesikitishwa na mahudhurio mabaya ya wanafunzi wa shule ya Msingi Irienyi,pamoja na shule zipatazo 30 kutokaguliwa kwa takribani miaka saba, wakati wakaguzi wa shule walipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya shule za Msingi katika Wilaya ya Rorya.

Aliyasema hayo,wakati akizungumza na Blog hii, juu ya matatizo yanayoikabili Wilaya hiyo kwa upande wa elimu,mara baada ya kumalizika kwa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika Novemba 11.

Alisema kuwa wakaguzi hao walifanya ziara mapema septemba 10 mwaka huu na kubaini upungufu mkubwa wa mahudhurio ya wanafunzi kutoka wanafunzi 788 wanaopaswa kuwa madarasani na kukuta wanafunzi 217 tu sawa na asilimia 27.5.

Alisema kuwa katika hali isiyo ya kawaida kuna shule zipatazo 30 ambazo haizijawahi kukaguliwa kati ya miaka 6-7 na kwamba zina hali mbaya sana.

Aliongeza kuwa pamoja na matatizo hayo pia kuna upungufu mkubwa wa wa madawati hasa shule ya msingi Ryagati ambapo jumla ya madawati 193 yanahitajika na kwamba mpaka sasa yapo madawati 47,kwa kuwa haikupata mgao wa madawati ya Mbunge wa jimbo la Rorya,Lameck Airo na mgao kutoka mfuko wa jimbo.


Aidha umefanyika pia ukaguzi maalumu kwa kata zipatazo mbili za Bukwe na Nyathorogo kwa shule za Msingi za Chuchuri na Mori ambazo pia zina mapungufu ikiwa ni pamoja na kuongeza ujenzi wa vyumba za madarasa katika shule ya Msingi Chuchuri,ambapo Shule ya Msingi Nyathorogo imeaza ujenzi wa vumba viwili vya madarasa ya awali.

Wednesday, November 2, 2011

KWA KHERI MDOGO WANGU.

KWA KHERI MDOGO WANGU OLIVA VEDASTUS MASHAURI, ULITUTOKA TAREHE 28.10.2011, UTAKUMBUKWA NA MWANAO MPEDWA, VEDASTUS.BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LITUKUZWE.