MKUU wa Mkoa wa Mara,John Tuppa, amewataka watumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Musoma kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kuwa ndicho chama kilichoshinda katika uchaguzi Mkuu na kinachotakiwa kutekeleza Ilani yake huku akiwakemea watendaji wabovu na ambao hawawajibiki katika kazi zao.
Aliyasema hapo jana alipokutana na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma katika ziara yake ya kwanza katika ukumbi wa Halmashauri uliopo katika Manispaa ya Musoma,tangu ateuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Alisema CCM ilishinda na Ilani yake ndiyo inayoongoza na ndiyo yenye kutekelezwa hivyo amewataka kuitekeleza na kuhakikisha watumishi wao wanafanya kazi pasipo kuingiza siasa kwani muda wake umepita na sasa utekelezaji, na kwamba siasa wawaachie wanasiasa wenyewe wakiwa majukwaani.
“Nimekuja leo kunitambulisha kwenu,tufahamiane uso kwa uso kabla sijaanza ziara ya kukutana na watendaji kwani nikachokiomba kwenu ni ushirikiano kwani nyie watumishi mnaoshughulika na wananchi ili mtatue kero zao” Alisema Tuppa.
Alisema kama watumishi wa halmashauri hawatatui kero za wananchi wanachi nao wataichukia serikali yao. “Kila mtu atimize wajibu wake mimi sitaki majungu, sitaki kuona mtu anakuja kwani anipatia majungu majungu kuwa mtu fulani hafai, nitakachofautailia ni ni vitendo vyenu,kama mnafanya kazi, na ukinidhibitishiea kuwa haufai nitaanza na wewe” Alisisitiza.
Aidha aliwataka kuhakikisha kuwa mipango ya halmashauri inakwenda sawa na kupata matokeo chanya na kuwataka kuepuka na hali ya kuwa na hati yenye mashaka kwani Waziri Mkuu ametoa agizo endapo hati itaendelea kuwa ya mashaka atawajibishwa Mkuu wa Mkoa.
“Waziri Mkuu kaniagiza niafatilie vinginevyo ataniwajibisha, kwani mmepata hati ya mashaka, kabla sijaanguka kwenye sementi, naweka godoro, Matatizo yetu tuyatatue wenyewe si kufuatana fuatana kwami kil amtu anajua kilichomleta ni kufanya kazi na ameisomea kazi hiyo, nikikwambia ufanye moja, mbili ,tatu, fanya na kama hukufanya nitakushumshughulikia mtumishi huyo” Alisema Mkuu wa Mkoa.
Akisoma taarifa ya Wilaya kwa Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Dk. Karaine Kunei alisema Wilaya hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula kutokana na chakula chake kikuu aina ya muhogo kukumbwa na ugonjwa wa batobato.
Akizungumzia juu elimu ya elimu ya sekondari alisema jumla ya watoto 376 wa shule mbalimbali za sekondari walipata ujauzito na hivyo kushindwa kuendelea na elimu na kwamba hali ya maambukizi ya vvu katika halmashauri hiyo iko juu kwa asilimia 6.4.
Wilaya ya Musoma ina jumla ya shule za sekondari 42 sita kati ya hizo zikiwa za taasisi mbalimbali na ina kata 43 na vijiji 116.
Mkuu wa Mkoa wa Mara alianza ziara yake ya kikazi juzi ambapo alikutana na viongozi wa vyama vya siasa na kufanya mazungumzo nao, ataendelea na ziara yake katika Wilaya za Bunda, Rorya, Tarime na Serengeti.
No comments:
Post a Comment