ZIWA Victoria linachangia pato la Taifa kwa takribani Dola za kimarekani Bilioni 3 hadi Bilioni 4 kwa Mwaka.
Hayo yamesema Novemba 29 na Katibu Tawala wa Mkoa, Clement lujaji katika kilele cha maadhimisho ya siku ya ziwa Viktoria kitaifa iliyofanyika katika Mkoa wa Mara, Manispaa ya Musoma , iliyofanyika katika Bwalo la Polisi, Mwisenge.
Alisema kuwa ziwa Viktoria ni raslimali muhimu katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na lina hazina kubwa zaidi ya samaki wa maji baridi Duniani.
Aliongeza kuwa samaki wanovunwa kwa mwaka ni kati ya tani 400,000 hadi 500,00o kwa mwaka, sambamba na hilo pia ziwa hilo ni kivutio cha utalii na chanzo cha mto Nile ambao una maporomoko ya Owen, Jinja-Uganda yanayotumika kuzalisha umeme unaosambazwa katika nchi za Uganda, Kenya, Tanzania na Rwanda.
Aidha madhumuni ya maadhimisho hayo ni kuwapa fursa wananchi na wadau wa Bonde la Ziwa Vikroria kukutana ba kuonesha shughuli mbalimbali za kuendeleza bonde hilo na mafanikio yake pia kupata fursa ya kubadilishana uzoefu na kutafakari mbinu mpya za kutimiza azma ya kukuza uchumi wa eneo la nchi wanachama.
Hata hivyo pamoja na nia nzuri ya serikali kukutananisha wadau hao, wengi wa wadau hao hawakuweza kushiriki kikamilifu katika kilele hiki, zikiwemo nchi zinazonufaika na Ziwa hilo.
Alisema kuwa changamoto zinazolikabili ziwa ni pamoja na kuwepo kwa gugu maji, kuongezeka kwa vitendo vu auvuvi haramu wa kutumia baruti na mabomu, uharibifu wa uchafuzi wa vyanzo vya maji na kwamba takwimu zinaonyesha kuangamia kwa ziwa hivyo basi hamna budi kuchukua hatua za makusudi ili kunusuru ziwa hilo.
Miongoni mwa hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kuhifandhi Ziwa Viktoria ni pamoja na kubni na kutekeleza Mradi wa kuhifadhi na kutunza Mazingira ya ukanda wa Bone la Ziwa Viktoria pamoja na ziwa lenyewe liwe sakama na kitovu cha uhai na maendeleo endelevu ya wananchi wa eneo lote la ziwa na viumbe wengine wanaoishi katika ukanda.
Serikali imeweka sheria mbalimbali zinazolenga kutunza mazingira zikiwemo sheria ya mazingira Namba 20 ya Mwaka 2004.
Aidha Mwaka 2009,Serikali ilipitisha Sheria Namba 11 ya Rasilimali za maji na Sheria Na.12 ya huduma za maji safi na Usafi wa Mazingira ambazo zinalenga kulinda na kutunza vyanzo vya maji.
Kifungu cha 52(1) cha Sheria Na.12 ya huduma za Maji na usafi wa mazingira zinatoa adhabu ya faini ya kiwango cha Sh. Milioni 1 au kifungo cha kwenda jela miezi 12 au vyote viwili kwa pamoja kwa mtua yeyote atakayesababisha uchafuzi wa chanzo cha maji.
Awali akisoma hotuba yake kwa mgeni rasmi, Afisa Maji Bonde la Ziwa Viktoria
( LVBWO) ,ofisi ndogo ya Musoma, Jumanne Sudi alitanabaisha kazi zinazofanywa na ofisi hiyo kuwa ni pamoja na kutoa hati ya haki ya kutumia maji,kushughulikia maombi na kutoa vibali vya kutiririsha vya majitaka kwenye ziwa na mito baada ya kuridhika na viwango vya maji hayo kulingana na viwango vilivyowekwa, kukusanya na kutunza takwimu za maji kutoka kwenye miti, ziwa na maji chini ya ardhi kwa ajili ya kuratibui matumizi endelevu.
No comments:
Post a Comment