AGIZO LA WAZIRI TAMISEMI LAKIUKWA
RORYA.
BARAZA la Madiwani Wilaya ya Rorya kwa pamoja limetoa pendekezo la kufanya marekebisho ya haraka katika ujenzi wa wodi la Wazazi lililoko Changuge, kutokana na vyoo vyake kujengwa nje ya wodi hilo,na wajawazito kukosa huduma,kufuatia agizo la Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri alipofanya ziara katika Wilaya hiyo.
Walisema kutokana na kuchelewa kwa uvunjwaji wa ukuta na kutengeneza vyoo upya kwa agizo la Naibu Waziri, Mkandarasi huyo hana budi kuharakisha ujenzi huo kwa kuwa wanawake kwa sasa wanapata taabu ya sehemu ya kujifungua na huku wodi likiwa halina choo na ucheleweshwaji wa Ujenzi upya.
Mkandarasi wa ujenzi huo, Mhini Construction wa Wilaya ya Tarime alipaswa kukabidhi jengo hilo mapema juni 15 mwaka huu,ambapo mradi wa ujenzi wa wodi hiyo ulianza Juni 9 2010.
Fedha ambayo ilikuwa tayari imelipwa ni kiasi cha Sh. M. 35,470,0720,Ambapo gharama kuu ya mradi hadi ungekamilika ilikuwa kiasi cha Sh. Milioni 40.
Lengo la Mradi wa ujenzi wa wodi ya wazazi Changuge ilikuwa kulaza wajawazito walio na uchungu, kujifungua na kutunza watoto ambao wanazaliwa kabla ya muda wao wa kuwaruhusu wazazi kwenda nyumbani wakiwa salama na lingehudumia watu 36 kwa siku endapo lingekamilika.
Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri, alipofanya ziara yake katika Wilaya hiyo Mei 24 mwaka huu alikataa kufungua wodi hiyo kutokana na kutokidhi viwango ikiwa ni pamoja na vyoo vya wodi hiyo kujegwa nje ya wodi na Milango ya wodi hiyo ikiwa na mbao zisizokidhi viwango, na kutoa agizo kwa mkandarasi wa ujenzi huo kutwalipwa fedha zilizobaki na kuhakikisha linafanyiwa marekebisho ya haraka, lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika.
NYAVU ZACHOMWA MOTO.
JUMLA ya nyavu 45 na samaki wachanga aina sangara zenye thamani ya Sh Milioni 4,522,000 zimeteketezwa kwa moto katika oparesheni iliyofanyika katika Wilaya ya Rorya mwezi Agosti na Septemba mwaka huu.
Mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Wilaya ya Rorya, Cosmas Ngangaji kwenye kikao cha baraza la Madiwani kilichokaa hivi karibuni imebainisha kuwa kitengo cha uvuvi,katika doria za ulinzi wa Rasilimali ya uvuvi ilifanyika oparesheni hiyo.
Aidha vituo vya Sota, Nyang’ombe, Kibuyi na Ruhu vikiendelea kupokea samaki aina ya Sangara kutoka kwa wavuvi na kuzipeleka viwandani kwa ajili ya kuchakatwa na kupelekwa kwenye soko la Nchi za Ulaya.
Alisema Agosti 15 nyavu zipatazo 15 aina ya timba zenye matundu ( Mesh) yenye ukubwa wa inchi 3 zikiwa na thamani ya Sh. 1,350,000 zilikamatwa.
Aliongeza kuwa nyavu aina ya timba (Monofilament) zapatazo 18 zenye macho ya 3.1\2 zikiwa na thamani ya Sh. 1,620,000 zilikamatwa pamoja na samaki wachanga aina ya sangara zenye thamani ya Sh. 60,000 zilichomwa moto na samaki ziligawiwa wananchi.
Samaki wengine wachanga aina hiyo hiyo walikamatwa katika kisiwa cha Bugambwa Kibuyi zenye thamani ya Sh. 150,000 ambazo pia ziligawiwa wananchi.
Aidha nyavu zingine aina Monofilament 4 za nchi 3 zenye thamani ya Sh. 360,000 pamoja na samaki wachanga wenye wa Sh. 90,000 zilichomwa moto na samki ziligawiwa wananchi.
Kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ruhu na wadau, Nyavu wa aina ya Timba (Monofilament) za nchi 4.5 zenye thamani ya Sh. 100,000 na samaki wachanga aina ya sato wenye thamani ya Sh. 72,900 zilikamatwa na kugaiwa wanachi na nyavu kuteketezwa kwa moto.
Vile vile mwezi Septemba nyavu zingine nane aina ya Monofilament ya inchi 3 zilichomwa moto,zikiwa na thamani ya Sh. 720,000.
Katika tukio hilo vatu watatu wamefikishwa mahakamani ya Wilaya ya Tarime kwa tuhuma ya kuvua samaki kwa kutumia madawa katika Shauri Na. CC.371/2011 dhidi ya Tumaini Makasa, Amani Makasa, Iddi Obeid na Nyarongo Waryoba, Shauri jingine linasubiri uthibitisho kutoka maabara ya Taifa ya Uvuvi ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani.
Aidha Wilaya ya Rorya ina mkakati wa kuboresha ukusanyaji mapatto kutokana an ada za leseni za uvuvi,biombo vya majini na usajili wa biombo vipya na ulinzi wa rasilimali za uvuvi.
No comments:
Post a Comment