Saturday, November 12, 2011

UKAGUZI WA SHULE WILAYA YA RORYA ZERO!!!!

RORYA.

Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Rorya, Cosmas Ngangaji, amesikitishwa na mahudhurio mabaya ya wanafunzi wa shule ya Msingi Irienyi,pamoja na shule zipatazo 30 kutokaguliwa kwa takribani miaka saba, wakati wakaguzi wa shule walipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya shule za Msingi katika Wilaya ya Rorya.

Aliyasema hayo,wakati akizungumza na Blog hii, juu ya matatizo yanayoikabili Wilaya hiyo kwa upande wa elimu,mara baada ya kumalizika kwa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika Novemba 11.

Alisema kuwa wakaguzi hao walifanya ziara mapema septemba 10 mwaka huu na kubaini upungufu mkubwa wa mahudhurio ya wanafunzi kutoka wanafunzi 788 wanaopaswa kuwa madarasani na kukuta wanafunzi 217 tu sawa na asilimia 27.5.

Alisema kuwa katika hali isiyo ya kawaida kuna shule zipatazo 30 ambazo haizijawahi kukaguliwa kati ya miaka 6-7 na kwamba zina hali mbaya sana.

Aliongeza kuwa pamoja na matatizo hayo pia kuna upungufu mkubwa wa wa madawati hasa shule ya msingi Ryagati ambapo jumla ya madawati 193 yanahitajika na kwamba mpaka sasa yapo madawati 47,kwa kuwa haikupata mgao wa madawati ya Mbunge wa jimbo la Rorya,Lameck Airo na mgao kutoka mfuko wa jimbo.


Aidha umefanyika pia ukaguzi maalumu kwa kata zipatazo mbili za Bukwe na Nyathorogo kwa shule za Msingi za Chuchuri na Mori ambazo pia zina mapungufu ikiwa ni pamoja na kuongeza ujenzi wa vyumba za madarasa katika shule ya Msingi Chuchuri,ambapo Shule ya Msingi Nyathorogo imeaza ujenzi wa vumba viwili vya madarasa ya awali.

No comments:

Post a Comment