Saturday, April 16, 2011

BAJETI YA HALMASHAURI YA SERENGETI

HALMASHAURI ya Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara imekisia kutumia jumla ya kiasi cha shilingi Bilioni 23,216,215,911.20 katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2011/2012.

Afisa Mpango wa halmashauri hiyo Joseph Kitanana aliyasema hayo kwenye kikao cha baraza la madiwani cha kupitisha bajeti ya mwaka huo wa fedha kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Kitanana akisoma taarifa ya makisio ya bajeti ya fedha hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Kimulika Kalikinga alisema upitishaji wa bajeti hiyo ni sambamba na na mwongozo wa Taifa wa mpango ya maendeleo wa miaka mitano wa serikali za mitaa kwa mwaka 2011/12 hadi 2015/16 kwa mujibu wa ilani ya uchaguzi ya CCm ya mwaka 2010/15.

Alifafanua kuwa katika kipindi cha wa kati na bajeti 2011/12 hadi 2015/2016 halmashauri itaendelea kutekeleza majukumu ya miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo Shilingi mili.12,714,110,499.20 ni kwa ajili ya mishaharana matumizi mengineyozitatumika sh. Milioni 3,183,993,576 na katika miradi ya maendeleo zitagharimia shilingi milioni 7,318,376,836 .

Alisema kuwa kati ya kiasi hicho shilingi milioni 1,171,772,000 ni vyanzo vya mapato ya ndani,ambapo shilingi milioni 797,515,000 ni makusanyo ya halmashauri na shilingi milioni 337,992,000 ni fidia ya vyanzo vilivyofutwa sawa na ongezeko la asilimia 30.79 ikilinganishwa na makusanyo ya halmashauri hiyo kwa mwaka 2010/2011 wa kiasi cha shilingi milioni 551,959.

Katika elimu ya utalawa na watu wazima zitatumika shilingi Milioni 415.931,elimu ya shule za msingi shilingi mil.7,482,shule za sekondari zitagahrmu shilingi mil.2.724 na katika shughuli za ukaguzi wa shule zitatumia shilingi mil.14.1 na katika mradi wa kilimo zitatumika shilingi milioni 352.124 ambapo mifugo ni shilingi milioni 316.118.

Alizitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni utekelezaji wa miradi katika sekta ya miundombinu unaokabiliwa na upungufu wa wakandarasi wenye na ujuzi,vifaa n auzoefu wa kutosha.

Aidha kupanda kwa bei za mafuta aina ya petrol sanjali na vyakula,mali ghafi na pembejeo vitadhiri bajeti na hali ya ugumu wa maisha kwa wakazi wa Wilaya hiyo zitakuwa kikwazo.

Akizungumzia zaidi Wilaya hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo,Kimulika Galikinga aliwataka madiwani hao kupendekeza mikakati ya maendeleo na badal ayake kuachana na itikadi za vyama.

No comments:

Post a Comment