Friday, April 29, 2011

MBUNGE AKATAA KUTUMIA OFISI YAKE.

KATIKA hali isiyo ya kawaida Mbunge wa jimbo la Musoma Mjini Vicent Nyerere amekataa ofisi yake kwa madai kuwa siyo nzuri.

Habari kutoka katika chanzo chetu cha habari kutoka Mjini Musoma kimesema kuwa Mbunge huyo tangu achaguliwe na wananchi hajawahi kufika ofisi kwake licha ya wananchi lukuki kumsaka ofisi hapo kutoa hoja zao bila mafanikio.

Chanzo hicho kimesema kuwa Mbunge huyo amedai kuwa ofisi hiyo siyo nzuri na kwamba anasubiri kumalizika kwa jengo jipya la ghorofa moja lililopo katika halmashauri ya Mji wa Musoma,mkabala kabisa na ilipo ofisi yake aliyoikataa.

Mwandishi wa habari hii alifanikiwa kufika katika Halmashauri ya Mji wa Musoma na kugundua kuwa ni kweli ofisi hiyo haitumiki,na kushuhudia tangazo lililobandikwa ofisini kwa Meya wa Mjini Alex Kisulula kuwa ndiyo ofisi ya Mbunge na Meya.

Chanzo hicho kimezidi kusema kuwa Mbunge huyo alikabidhiwa ofisi hiyo kuwa ndo atakuwa anaitumia lakini cha kushangaza ameamua kutumia ofisi ya Meya bila kutoa taarifa ya maandishi kwa uongozi huska wa halmashauri hiyo.

Katika uchaguzi uliomalizika Mwaka jana, Mbunge huyo alishinda na kutangazwa kuwa Mbunge wa Musoma Mjini,ambapo tangu achaguliwe hajawahi kushiriki vikao vyovyote vya halmashauri,Baraza la Madiwani,Bodi ya barabara na vinginevyo.

Pia katika uchaguzi huo viti 10 vya udiwani vilichokuliwa na Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) ambapo CCM ilipata viti vitatu.

Kata zilizoko Mji wa Musoma ni Mukendo,Iringo, Kitaji, Nyamatare, Buhare, Bweri, Makoko, Nyasho, Nyakato, Mwisenge, Kigera, Mwigobero,Kamunyonge.

Jitihada za kumpata Mbunge huyo kuzungumzia ni kwa nini hataki kutumia ofisi aliyopangiwa na kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Mji wa Musoma hazikuzaa matunda.

No comments:

Post a Comment