Thursday, April 14, 2011
DIWANI wa CHADEMA Kata ya Machochwe katika halmashauri ya wilaya Serengeti mkoa wa Mara Samwel Gibewa amesalimisha bunduki moja ikiwa na risasi zake 21 baada ya kubanwa na Mkuu wa Mkoa huo kanali Mstaafu Enos Mfuru . Diwani huyo amesalimisha silaha mbele ya kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo cha kujadili na kupitisha bajeti ya mwaka 2011/12 hadi 2013/14. Gibewa alisema amelazimika kuisalimisha silaha hiyo aina ya SMG yenye 1960 KA 2823 ya nchi jirani ya Kenya baada ya kushambuliwa na madiwani wenzake ambapo awali alikana kuwa hana silaha yoyote ambayo anamiliki na kwamba madiwani hao ni waongo na pia ni wazushi. “Ni muda wa saa nzima sasa tumazungumzia suala lako,hivi hakuna ajenda nyingine zaidi ya kuanzisha Chuo Kikuu na silaha hiyo?”aliuliza Mfuru na kuongeza kuwa baada ya kikao kufunguliwa anaitaka silaha hiyo iwe imeshalimishwa kwake kwa usalama na iletwe mbele ya kikao cha baraza la Madiwani. “Lazima tuondoke wote ukanipe hiyo silaha,nasema.. leo lazima ukanipe hiyo silaha kwa nini tunapoteza muda kwa kuzxungumizia neon moja tu la silaha? Kanipe hiyo silaha ili ttuendelee na masuala mengine ya wananchi,tumefanya nini la maana badala ya kunga’ng’ania silaha tusipoteze muda watu wote hawa wankuzingizia?”Aliululiza Mfuru huku akiwa na sura ya makunyanzi. Akiwa katika kata ya Machochwe, Mkuu huyo wa Mkoa alikwenda nyumbani kwake na kukabidhiwa silaha hiyo ambayo alikuwa ameifukia kwenye kichuguu kilichoko nyumbani kwake. Kabla ya kwenda kufukua silaha hiyo Mkuu huyo alikwenda kuiona shule ya sekondari ya Machochwe ambayo kama itakuwa imekidhi kiwango cha kuwa Chuo Kikuu ifunguliwe,ambapo pia alikuwa ameitisha mkutano wa hadhara kuzungumza na wananchi kama kweli wamekataa shule hiyo na kwamba ikifunguliwa watachoma moto. Akikabidhi silaha hiyo mbele ya wananchi wa kata yake alisema kuwa silaha hiyo alipewa na kijana mmoja ambaye hakutaja jina lake amtunzie na kutangaza kuwa kama kuna mwanchi yeyote ana silaha akibidhi kwa jeshi la polisi. Aidha baada ya kurejesha silaha na kuonyesha mbele ya baraza la madiwani Mkuu huyo wa Mkoa aliomba baraza la madiwani kumsamehe kwani tayari amemsamehe mbele ya wananchi wa kata ya Machochwe. Naye Mwenyekiti wa Halmashauri,John Ng’oina amewatka madiwani kuzungumza ukwele badla ya kuzunsha taarifa za uongozi ba kuanchana na itikadi za vyama na balada yake watumike wananchi kama walivyowaahidi. “Ni vyema diwani akaachana na yaliyopita kuliko kutumia madaraka yake kukichafua chama na kwamba kama hana uzoefu aombe ushirikiana kwa walio na uzoefu” Alisema Ng’oina. Diwani huyo ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augostino cha Jijini Mwanza, mwaka wa mwisho ambapo anasomea digrii ya kwanza ya elimu. Wiki hii wakazi wawili wa wilaya ya Serengeti,Marwa Mniko mkazi wa kijiji cha Nyamatare na Ngambarusu Ngaria wa kijiji cha Bwitengi walisalimisha silaha zao tatu aina ya SMG na Laifo kwa kamanda wa polisi Mkoa wa Mara,Robert Boaz. Kutokana na matukio ya uhalifu na kumiliki silaha kinyume cha taratibu na sheria kukomaa,jitihada za makusudi zinahitaji ili kuhakikisha jina la Tanzani kuwa nchi ya Amani lizidi kudumishwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment