Saturday, August 18, 2012

MWENGE WA UHURU WAFUNGUA MIRADI MUSOMA


 MUSOMA.

 Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilayani Musoma umezindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo.


Miradi iliyozinduliwa ni pamoja na ufunguzi wa matanki matano ya maji yenye uwezo kuchukua lita 5000 za maji katika Shule ya Sekondari ya Ufundi ( Musoma Alliance) ambapo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amewahi kusoma hapo.

Akizungumza mara baada ya kweka jiwe la Msingi kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Capt. Honest Erenest Mwanosa alisema uwekaji wa huduma hiyo itawasaidia wanafunzi hao kufanya masomo yao badala ya ile ya awali ya kutembea hatua kadhaa kwenda ziwani kuyatafuta hali ambayo ilikuwa inawapa shida wanafunzi.


Aliwataka pia wanafunzi hao kusoma kwa bidii kwani elimu ndio msingi wa maisha, badala ya kuweka migomo isiyo ya lazima.  

Akizungumza na Mliki wa Blog hii, Mwanafunzi wa kidato cha tano katika Sekondari hiyo, Sabaya Kinyi alitoa shukrani kwa Serikali na kuiomba kufanya ukarabati shule hiyo ambayo majengo yake ni muda mrefu na sasa yanaelekea kuwa chakavu pia kuongezewa walimu kwani shule hiyo ina upungufu wa walimu.

Mwenge huo ukiwa Kata ya Bweri-Songe, uliweka jiwe la msingi kwenye nyumba bora ya mwananchi iliyogharimu kiasi ya Sh Milioni 180.

Aidha uliweka jiwe la msingi vyumba viwili vya maabara ya sekondari ya Bweri  ambavyo mara baada ya kukamilika utagharimu kiasi cha Sh. Milioni 68 ambapo sasa umegharimu Sh. Milioni 34 na kuzindua klabu ya TAKUKURU.

Akisoma hotuba kwa Kiongozi huyo, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Bweri, Alphonce Kameta, alisema Mradi huo utakapokamilika wanafunzi watapata fursa nzuri ya kujifunza masomo ya sayansi kwa vitendo na hivyo kupata maarifa na ujuzi wa kutosha kuwawezesha kufanya vyema katika masomo ya Sayansi.

Naye Mwenyekiti wa Klabu ya wapinga rushwa wa Shule ya Sekondari Kamunyonge, Salum Masesa  alisema kuwa klabu za wapinga rushwa ambayo kwa sasa ina wanafunzi 20, imeanzishwa kwa lengo la kuwajenga wanafunzi kimaadili na kuwashirikisha katika mapambano dhidi ya rushwa na kuwawezesha kutambua nafasi na wajibu wao katika mapambano ya rushwa na hivyo kushiriki ipasavyo kuzuia na kupambana na rushwa

Alisema kutoka na elimu waliyipata na wanayoendelea kuipata wako tayari kushiriki katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa taarifa, kukemea,kuelimisha wanafunzi wenzao  na jamii kwa ujuml ana kwamba tayari kulitumikia Taifa kwa uaminifu mkubwa.

Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi katika wodi ya watoto iliyoko Nyakato, ambapo Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Nyakato, Shadrack Ndaro, alitoa taarifa ya ujenzi wa wodi hiyo kwamba kwa kipindi cha Mwaka 2010/2011 awamu ya kwanza zilitumika Sh. Milioni 30 hadi hatua ya kupaua na michango ya wananchi Sh. Milioni 2 na hadi kukamilika utagharimu jumla ya Sh. Milioni 56 fedha ambazo zimetokana na Mradi wa CDG (central Development Government).

Aidha Mwenge huo uweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya Kwangwa kilometa 2, kufungua vyumba vinne vya madarasa shule ya msingi kigera vilivyogharimu Sh. Milioni 62.2 na kupanda miti ya vivuli na matunda pia kufungua jengo la kuhifadhia maiti (Mochwari)lililogharimu Sh. Milioni 190 hadi kukamilika, jengo ambalo ndani yake lina ofisi sanjali na  Kantini  ya Chuo cha VETA ambayo imegharimu Sh.Milioni 18.8, kukagua na kuhamasisha kikundi cha vijana cha useremala na Saccos ya akinamama iliyoko uwanja wa Mpira wa Karume.


Mwenge huo umemaliza Mbio zake Mkoa wa Mara na  huko  Wilaya ya Bunda. 




MAKARANI WA SENSA WAENDA FIELD

 MUSOMA.

MAKARANI wa Sensa, katika Sensa ya watu na Makazi Wilaya ya Musoma Mjini wanaendelea na Mafunzo ya vitendo ambapo wamekwenda kutembelea maeneo ya kazi (AE) watakazofanyia kazi kwa kuzitambua.

Katika zoezi hilo ambalo liligawanyika kwa makundi makundi kwa makarani wa Dodoso fupi walikwenda maeneo mbalimbali wakiongozwa na Ramani zilizopo.

Aidha wamekwenda maeneo ya Kitaji B,C,D Mwigobero na Iringo ambapo wamebaini Mambo mbalimbali na baadae mchana huu watafanya majumuisho kwa wakufunzi wa Madarasa.

Semina hiyo itamalizika kesho ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika kufunga mafunzo hayo na Makarani hao kuanza kazi ifikapo usiku wa Tarehe 25/8/2012 usiku wa manane.

Wakati huo huo zoezi la kuandikisha vitambuliho vya makazi liko Mbioni ambapo ianelezwa kwamba linatajiwa kuanza mara baada ya zoezi la Sensa ya watu na makzi kuisha.

Mafunzo kwa makarani wa Sensa yalianza wiki iliyopita na kufunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Jackson Msome.



 

Friday, August 10, 2012

TAASISI ya Kuzuia na kupambana na rushwa(TAKUKURU) Mkoa wa Mara, imemfikisha Mahakamani Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ,Christopher Nyandiga

MUSOMA



TAASISI ya Kuzuia na kupambana na rushwa(TAKUKURU) Mkoa wa Mara, imemfikisha Mahakamani Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ,Christopher Nyandiga kwa makosa ya kutumia nyaraka zenye lengo la kumdanganya mwajiri wake kinyume cha sheria na kuisababishia  serikali hasara ya jumla ya  Sh Milioni 24.



Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Naibu Mkuu wa Taasisi hiyo Mkoa, Yustina Chagaka imesema kuwa Mhandisi huyo ambaye kwa sasa yuko Wilaya ya Ledewa alifanya makosa na kudanganya mwajiri wake kinyume na kifungu cha 22 cha sheria ya kuzuia na kupambana an rushwa Namba 11 ya mwaka 2007 na kifungu cha 10(1) cha jedwali la wkanza kikisomwa pamoja na vigungu vya 57(1) na 60(2) vya sheria ya uhujumu uchuni Namba 200 kama ilivyofanyiwa mapitio mwaka 2002.



Ilisema baada ya uchunguzi uliofanywa na  TAKUKURU umebaini kuwa kampuni inayomilikiwa na mshitakiwa iitwayo Mbully Enterprises and Covil Works ilipewa zabuni na halmashaur ya Wilaya ya Bunda ya kutoa Wind mill aina ya Poldaw ya mita 5.8/mita 8.2 kwa gharama ya Sh. Milioni 24, kuisimika (installation)  kwa gharama ya Sh. Milioni 2,  kuifanyia majaribio (testing) kwa gharama ya Sh. Milioni 1  na  Jumla yake ikiwa  Sh Milioni 27 kwa ajili ya mradi wa umwagiliaji mazao katika kijiji cha Kasuguti.




Aidha uchuguzi uliofanywa umebaini kuwa Mnano Disemba 2007 kwa niaba ya Kampuni hiyo iliyowasilisha hati ya madai(invoice) namba 0152 na delivery note namba 0252 kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda zenye maelekezo ya uongo.



Maelezo hayo yalisema kuwa alinunua na kuwasilisha Wind Mill moja aina ya Poldaw ya mita 8.2 yenye thamani Sh Milioni 24 huku akijua kuwa si kweli kwa sababu Wind Mill hiyo haikuwa ya Poldaw ya Mita 8.2 bali ilikuwa chakavu ambayo haifai kwa matumizi yaliyokusudiwa.



 Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Mara inatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa.

MWENGE WA UHURU KUANZA MBIO ZAKE MKOA WA MARA.


MUSOMA


MBIO za Mwenge wa Uhuru zinaanza  Agosti 13 katika Mkoa wa Mara ambapo utawasili katika Kijiji cha Robanda Wilaya ya Serengeti na kupokelewa Nabi -Gate  ambapo kutafanyika makabidhiano kati ya Mkoa wa Arusha na kuingia Mkoa wa Mara.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, inasema Mara baada ya kuokelewa utaanza mbio zake kwa kuzindua miradi mbalimbali ya Maendeleo.
Miradi itayowekewa jiwe la Msingi ni pamoja na Sekondari ya Robanda, kisima cha Motukeri, jengo la kituo cha wakulima Natta na kupokea taarifa ya ujenzi.

Ukiwa Wilaya ya Serengeti Mwenge huo  utafanya uzinduzi wa nyumba bota ya mwanakijiji wa Nyichoka,kupokea taarifa ya mwenye nyumba nay a ujenzi wa jengo la huduma ya Mama na Mtoto na kufungua jengo pia kuweka jiwe la msingi katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji ambapo zawadi na cheti zitatolewa kwa club ya wapinga rushwa.


Aidha katika Wilaya ya Tarime Mwenge huo utafungua SACCOS ya Masanga,kuweka jiwe la Msingi kituo cha  Afya cha Nyanungu, kutembelea shamba la Migomba la ekari tanio na kuzindua uvunaji maji ya mvua matenki mawili, kufungua jengo la utawala la Magoto Sekondari, kufungua ofisi ya Kata ya Nyarero,kuzindua daraja la Ronsoti na barabara yenye urefu wa Mita800, wodi ya Wazazi ya hospitali ya Wilaya,mradi wa kitalu cha kahawa na chai.

Mwenge huo ukiwa katika Wilaya hiyo pia utazindua klabu ya kuzuia rushwa na madawa ya kulevya, kufungua zahanati ya Ikoma, kuzindua kisima cha maji katika Sekondari ya Mirare, kufungua Saccos na kuweka jiwe la msingi Utegi Saccos, utatembelea hifadhi ya mazingira na ufugaji wa nyuki pamoja na kukabidhi Mizinga mitano ya nyuki na kisima cha Maji na kuweka jiwe la msingi baabara ya Buturi sekondari na kufanya ukaguzi wa Kilimo cha umwagiliaji na kukabidhi power tiller nne,Trekta mbili na mashine ya kukoboa mpunga na kutembelea kikundi hc kuteketeza nyavu haramu kilichoko Kinesi.

Katika Manispaa ya Musoma Mwenge huo utaweka jiwe la misngi kwenye nyumba bora ya mwananchi, kufungua mradi wa maji Shule ya Sekondari ya Ufundi,kuweka jiwe la msingi maabara ya sekondari ya Bweri  na kuzindua klabu ya TAKUKURU, kuweka jiwe la msingi katika wodi ya watoto iliyoko Nyakato, kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara ya Kwangwa kilometa 2, kufungua vyumba vinne vya madarasa shule ya msingi kigera na kupanda miti ya vivuli na matunda pia kufungua Kantini  ya Chuo cha VETA.

Utafungua pia jengo la kuhifadhi maiti(Mochwari), kukagua na kuhasisha kikundi cha vijana cha useremala na Saccos ya akinamama iliyoko uwanja wa Mpira wa Karume na kutoa hundi ya Sh. 100,000.


Agosti 17 Mwenge huo utaelekea katika Wilaya ya Butiama ambapo makabididhiano yatafanyika kijiji cha  Nyankanga na kuelekea Butuguri.




Thursday, August 9, 2012

MAKARANI WAANDAMIZI WA SENSA WAPATA MAFUNZO


 MUSOMA.

Makarani waandamizi wasimamizi wa Washiriki wa Sensa ya watu na makazi wameombwa kufuatilia na kusikiliza kwa makini mafunzo watakayopewa na wawezeshaji wa zoezi hilo ili kuleta ufanisi katika zoezi hilo.

Hayo yamesemwa LEO na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Jackson Msome wakati akifungua semina kwa  Makarani Waandamizi na wasimamizi wa sensa na makazi katika ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mara.

Jackson Msome amesema kuwa mafunzo hayo yatawawezesha washiriki kupata mbinu za kuuliza maswali, namna ya kujaza dodoso refu na  taarifa mbalimbali za kaya na   kutambua namna ya kuhifadhi siri na taarifa za kaya ambazo wamezipata.

Amesema kamati imewaamini kufanya kazi hiyo hivyo washiriki wanaombwa watambue dhamana kubwa waliyopewa na serikali hivyo ufanisi na uhodari wao katika kazi utapimwa kwa mafanikio ya sensa iyo itakayoanza Agosti 26, 2012.

Aidha  Serikali inapenda kuona sensa hiyo ikipata mafanikio makubwa hivyo semina hiyo inalenga kuwajengea uwezo mkubwa na ufanisi ili kila wilaya ifanikishe zoezi hilo kwa ufanisi zaidi kwa maslahi ya taifa kwa ujumla.

Aidha ametaka viongozi kutoa ushirikiano kwa vyombo vya habari kwani ndio sekta muhimu katika kuelimisha wananchi kuhusiana na sensa ya watu na makazi na kwamba vyombo vya habari vina nguvu na mchango mkubwa katika kutoa elimu ya uhamasishaji hivyo ni vema kama vyombo hivyo vitatumia nafasi hiyo kuhamasisha  wananchi ili watoe ushirikano wa  kutosha katika zoezi hilo.


Mafunzo hayo ya Sensa ya watu na makazi yamefunguliwa rasmi Agosti 9 katika Wilaya ya Musoma  na jumla ya washiriki wapatao 200 wamehudhuria mafunzo hayo na kwamba yatafanyika muda wa  siku kumi na moja.

Wednesday, August 8, 2012

KASHESHE HILO KWA MKAZO ZAIDI!!!!!!!!!!

MUSOMA.
BARAZA la madiwani wa halmashauri ya Musoma limegawanyika kwa mara ya kwanza na kufanya baadhi ya madiwani kutoka nje na kususia  kikao baada ya kutofatiana kimtazamo juu ya ugawaji wa halmashauri ndani ya wilaya ya Butiama.
Tofauti hiyo ilitokea jana wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambayo makao makuu yake bado yapo ndani ya Manispaa ya Musoma.
Baadhi ya madiwani hasa upande wa  kambi ya upinzani walikuwa wakidai kuwa wananchi wa kata ambazo zimegawanywa na kuwa halmashauri ya Musoma hawatatendewa haki endapo  watakuwa chini ya Mkuu wa wilaya ya Butiama.
Akichangia hoja hiyo diwani wa kata ya Bukima Ruti Mayamba  alisema wawo kama wawakilishi wa wananchi hawatakuwa wamewatendea haki kutoka kata za majita na Lukuba kwani watakuwa mbali na huduma za kiutawala .
Mayamba alisema huduma zitakuwa karibu endapo watakuwa chini ya mkuu wa wilaya ya Manispaa ya Musoma.
“Tunataka kata hizi kumi na saba ziungane na kata 13 za Manispaa ya Muasoma ili kutengeneza wilaya ya Musoma”,alisema Mayamba.
Kwa upande wa  madiwani  wa chama Tawala waliazimia kuwepo na halmashauri mbili ya Musoma na Butiama ndani ya wilaya ya Butiama ambazo zitakuwa chini ya Mkuu wa wilaya hiyo ya Butiama.
 
Kikao cha baraza  la madiwani ndicho kikao kilichotajiwa kutoa maamuzi ya mugawanyo huo wa hamashauri mbili zilizopo ndani ya wilaya ya Butiama ambapomapendekezo yalielekezwa kuwepo na halmashauri mbili za musoma na Butiama ambazo zitakuwa chini ya Mkuu wa wilaya ya Butiama kwa kupigwa kura.
 
Katika mgawanyo huo wa halmashauri mbili zenye jumla ya kata 34, katika  halmashauri ya Musoma kuna kata 17 ambazo ni pamoja Nyegina,Etaro,Nyakatende,Mugango,ambazo zinaweza kuja Manispaa kwa maana ya Musoma Mjini.
 Kiriba ,Bukumi,Suguti Nyamrandirira,Nyambono,Bugwema, Murangi,Bukima,Buringa,Bwasi,Makojo,Tegeruka na Busambara ambapo makao makuu ya halmashauri hiyo yatakuwa Suguti-Kwikonero.

Halmashauri ya Butiama nayo inakata Kata 17 ambazo ni Nyankanga,Buruma,Bukabwa,Bwiregi,Nyamimange,Buswahili,Sirolisimba,Mirwa,Buhemba,Muriaza,Kukirango,Busegwe,Butiama,Masaba,Bisumwa na Kyanyari ambapo makao makuu ya halmashauri hiyo yatakuwa Butiama
  

MAJITA WAPINGA MAKAO MAKUU YA WILAYA.

 MUSOMA VIJIJINI (MAJITA)

BARAZA la madiwani wa halmashauri ya Musoma limegawanyika kwa mara ya kwanza na kufanya baadhi ya madiwani kutoka nje na kususia  kikao baada ya kutofatiana kimtazamo juu ya ugawaji wa halmashauri ndani ya wilaya ya Butiama.
Tofauti hiyo ilitokea Agosti 7 wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo ambayo makao makuu yake bado yapo ndani ya Manispaa ya Musoma.
Baadhi ya madiwani hasa upande wa  kambi ya upinzani walikuwa wakidai kuwa wananchi wa kata ambazo zimegawanywa na kuwa halmashauri ya Musoma hawatatendewa haki endapo  watakuwa chini ya Mkuu wa wilaya ya Butiama.
Akichangia hoja hiyo diwani wa kata ya Bukima Ruti Mayamba  alisema wawo kama wawakilishi wa wananchi hawatakuwa wamewatendea haki kutoka kata za majita na Lukuba kwani watakuwa mbali na huduma za kiutawala .
Mayamba alisema huduma zitakuwa karibu endapo watakuwa chini ya mkuu wa wilaya ya Manispaa ya Musoma.
“Tunataka kata hizi kumi na saba ziungane na kata 13 za Manispaa ya Muasoma ili kutengeneza wilaya ya Musoma”,alisema Mayamba.
Kwa upande wa  madiwani  wa chama Tawala waliazimia kuwepo na halmashauri mbili ya Musoma na Butiama ndani ya wilaya ya Butiama ambazo zitakuwa chini ya Mkuu wa wilaya hiyo ya Butiama.
 
Kikao cha baraza  la madiwani ndicho kikao kilichotajiwa kutoa maamuzi ya mugawanyo huo wa hamashauri mbili zilizopo ndani ya wilaya ya Butiama ambapomapendekezo yalielekezwa kuwepo na halmashauri mbili za musoma na Butiama ambazo zitakuwa chini ya Mkuu wa wilaya ya Butiama kwa kupigwa kura.
 
Katika mgawanyo huo wa halmashauri mbili zenye jumla ya kata 34, katika  halmashauri ya Musoma kuna 17 ambazo ni  pamoja na    Nyegina,Etaro,Nyakatende,Mugango, Kiriba ,Bukumi,SugutiNyamrandirira,Nyambono,Bugwema, Murangi,Bukima,Buringa,Bwasi,Makojo,Tegeruka na Busambara ambapo makao makuu ya halmashauri hiyo yatakuwa Suguti-Kwikonero.

Halmashauri ya Butiama nayo inakata 17 ambazo ni Nyankanga,Buruma,Bukabwa,Bwiregi,Nyamimange,Buswahili,Sirolisimba,Mirwa,Buhemba,Muriaza,Kukirango,Busegwe,Butiama,Masaba,Bisumwa na Kyanyari ambapo makao makuu ya halmashauri hiyo yatakuwa Butiama
  

MUSOMA.

Madiwani wa Manispaa ya Musoma wametakiwa kusimamia
ukusanyaji wa mapato kikamilifu ili kuiwezesha Manispaa kupata fedha
zitakazotumika kuwahudumia wananchi wake.

Hayo yamesemwa na Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurura katika kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa.

Alisema halmashauri hiyo ya manispaa inavyo vyanzo vingi vyamapato,ambavyo vikikusanywa  vizuri vitasaidia katika kuboresha huduma muhimu kwa wananchi kama vile huduma ya maji na barabara..

Naye Mchumi wa Manispaa ya Musoma John Masero alisema baadhi ya Madiwani na watumishi wa Manispaa wanatuhumiwa kwa kuwa na maslahi binafsi katika suala la kutoa zabuni mbalimbali katika Manispaa.

Masero alilieza baraza hilo kuwa  hayo kufuatia baadhi ya Madiwani katika baraza hilo kushinikiza kupunguzwa kwa masharti katika mchakato wa kutoa zabuni hali ambayo  itaipunguzuia Manispaa mapato.

Akichangia hoja hiyo diwani wa kata ya Kigera Charles Ocharo ameziomba Idara husika
kufanya uchunguzi juu ya  tuhuma hizo ili wote watakaobainika wachukuliwe hatua za kisheria.

Manispaa inatajia kujenga barabara za Mitaa kwa kiwango cha Lami na katika Mitaa kadhaa sanjali na kuweka vibao vya Mitaa ya baadhi ya  majina ya  waasisi wake ili waendelee kuezniwa ikiwa pamoja na Mtaa wa  Lucas Musiba eneo la Nyasho Kona, ambao kibao chake hakijulikanai kilipelekwa wapi.