Saturday, February 23, 2013

MPASUKO CHADEMA TARIME.




 TARIME.


VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA)  Wilayani
Tarime  wameshindwa kuafikiana  katika kikao cha kamati tendaji
kilichofanyika juzi kupata mwafaka uliosababisha kufugwa kwa ofisi.

Wanamtaka Mwenyekiti  wa Chama Taifa Freeman Mbowe kuwashuruhisha. 
 
Mjumbe mmoja alisema kuwa kwa sasa kunampasuko mkubwa ndani ya chama
cha Chadema ambapo tayari kuna makundi mawili yanayodaiwa kuwa kundi
moja ni la Mwenyekiti wa Vijana Taifa John Heche  na kundi la George
Waitara ambao wanadaiwa   kuwa wapo mbioni na kwamba wanajipanga kugombea 2015
 
Katibu Mwenezi wa Chama cha Chadema Wilaya Marwa Maruri  alikiri kwa
baadhi ya viongozi  kuondoka  wakati kikao kinaendelea.
 
Baadhi ya wanachama  Mjini Tarime walisema kuwa  sababu ya kufungwa
kwa ofisi kwa muda wa siku 3 imekuja baada ya Kaimu Mwenyekiti wa
Chadema Wilaya Lucas Ngoto kusimamishwa  uongozi na kamati Tendaji
jambo ambalo  alikuafikiwa na baadhi ya wananchama na kuibua mgogoro
mkubwa ambao umewafanya baadhi yao kugawanyika makundi.



Wednesday, February 13, 2013

MBWAMWITU HAWATATOWEKA TENA-SERENGETI




SERENGETI

Mkurugenzi  wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori(TAWIRI) Dk.Simon Mduma amesema kuwa tishio la kutoweka Mbwa Mwitu katika hifadhi ya Serengeti kutokana na magonjwa mbalimbali ya mbwa litatoweka kwani tayari wamepata chanjo ili kuweza kumaliza magonjwa yanayosababisha kutoweka kwa Mbwa Mwitu.


Mbwa hao waliochukuliwa eneo la Loliondo wamefugwa katika Hifadhi ya Taifa (TANAPA) kwa miezi mitatu hili likiwa ni kundi la pili lenye mbwamwitu 15 ambapo kundi la kwanza lilitolewa Agosti 30 mwaka huu likiwa na mbwamwitu 11 waliachiwa ndani ya hifadhi hiyo mwaka 1980 na kulikuwepo   Mbwa Mwitu wapatao 500.

Aidha Mbwamwitu wapatao 15 ambao walikuwa wamefugwa katika eneo la Nyamuma ndani ya hifadhi hiyo kwa ajili ya juhudi za kuwarudisha wanyama hao ambao walitopotea miaka ya 1990 wanaendelea vizuri.


 Kukosekana kwa wanyama hao ndani ya hifadhi hiyo kumesababisha kukosekana kwa kivutio kingine muhimu ambapo watalii wanahitaji kuwaona.

Alitoa pongezi kwa  mashirika mbalimbal ikiwemo ofisi ya Rais,ambayo ilichangia Sh. M.30 kwa ajili ya mradi  wa mbwa mwitu kwani  imesaidia kuongeza kivutio muhimu.



Alisema kuwa kuna changamoto ambazo wanakabiliana nazo ikiwa ni pamoja mashirika mengi kutofadhili mradi huo ambapo kwa sasa kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom ndio pekee iliyotoa ufadhili wa zaidi ya milioni 450.

Kutokana na kuruhusiwa kwa mbwamwitu hao sasa imeongezeka na kufanya idadi ya wanyama hao kufikia 26 ndani ya TANAPA ambapo Agosti 30 mwaka huu waliachiwa 11.


Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete aliagiza Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI) kuhakikisha Mbwamwitu waliofunguliwa  katika mbuga ya Serengeti wanakuwa salama muda wote ili wasitoweke tena.


Sunday, February 3, 2013

CCM MWANZA WAHADHIMISHA KWA MICHEZO



MWANZA

CHAMA cha Mapinduzi Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza kimefanya maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kufanya michezo mbalimbali ikiwemo ya mbio  za baiskeli yaliyosisimua wakazi wa Jiji la Mwanza.

Mbio hizo zilizoanzia katika ofisi za CCM Makao Makuu kuelekea Barabara ya kenyata-Usagara zilianza majira ya mbili asuhuhi na kuleta hamasha kubwa kwa wakazi wa Wilaya ya Nyamagana ambao kwa pamoja walikuwa wakiwashingilia huku wakisidikizwa na gari la Katibu wa CCM Wilaya hiyo likiwa na bendera kubwa ya Chama.

Mshindi wa kwanza katika mbio hizo alikuwa Gegedi Maduhu  (25) mwenye namba 850, Mfanyabiashara ya bodaboda ya baiskeli na Mzaliwa wa kijiji cha Mwamoto-Ngokolo Mkoa wa Shinyanga aliyemaliza mbio hiyo na kuwaacha wenzake kwa takribani dakika 10 na kumaliza mbio hiyo 10:40 katika Uwanja wa Kumbukumbu wa  Nyamagana.

Mshindi wa Pili alikuwa Paulo Mathias ( 19)  mwenye namba  831 Mkazi wa Shamaliwa kata ya Igoma Mwanza ambaye ni Mkulima wa mpunga aliyemaliza mbio hiyo 10:44 na Mshindi wa tatu alikuwa Kulwa Kalamo (20) mwenye namba 834 aliyemaliza kwa muda wa 10:46 na alipewa kombe na fedha taslimu Sh.300,000.

 Aidha akizungumza na  Uhuru, mara baada ya kukamilika kwa mbio hizo, Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Nyamagana,Raphael Shillatu alisema kuwa mchezo huo ni sehemu ya kuhamasisha wananchi.


 “Mchezo huu ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi kupitia michezo ili kuleta hamasha kwa vijana kwani  michezo ni ajira, pia huleta Mshikamano, Umoja, Upendo, Utulivu na Amani na kukiwezesha chama kuwa na timu itakayofanya kazi pamoja na kuhakikisha ushindi kuanzia chaguzi za Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu 2015”Alisema Shillatu.

Aliongeza kuwa mkakati huo ni ahadi yake wakati akiwa  anagombea Kiti hicho kuwa atahakikisha anaimarisha michezo yote ifikapo maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama ikiwa ni pamoja na riadha ya Baiskeli, mpura wa Miguu kwa wanaume ,bao,na baadae kuanzisha michezo mbalimbali kwa wanawake ambao nduyo wenye hamasha kubwa  hadi ukomo wa Uongozi wake ikiwa ni Utekelezaji wa Ilani kwa vitendo.

Aidha washindi hao walipewa vitita vya fedha zilizokuwa zimefugwa kwenye bahasha ambapo hata hivyo hazikutangazwa  kwa ajili ya usalama wao na kupewa bendera za CCM na mlingoti wake kupeperusha bendera hizo maeneo ya makazi yao.

BODI YA HOSPITALI YA RUFAA YA MUSOMA

BODI ya Hospital ya Rufaa ya Musoma ikiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uteuzi, wakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara,John Tuppa,kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo Baba Askofu Amos Muhagachi ambaye baada ya kuteuliwa alimtoa Katibu wa Hospital,Faustin Bigambo kwa utendaji mbovu katika Hospitali hiyo ili apangiwe kazi nyingine.

Saturday, February 2, 2013

UWT MUSOMA MJINI WAADHIMISHA KUZALIWA CCM



Wilaya ya Musoma Mjini imefanya maadhimisho ya miaka 36 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kutembelea wagonjwa katika wodi mbalimbali katika Hospital ya Rufaa ya Musoma sanjari na kufanya usafi wa Mazingira,kutoa sabuni pamoja na Juice kwa watoto wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Musoma Mjini ,Amina Masisa,amesema kuwa katika kuadhimisha kuzaliwa kwa CCM,shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwa ni pamoja na usafi wa mazingira
kata za Kamunyonge,Kitaji, Iringo,Nyasho,Mwisenge,Bweri,Makoko,Kigera, Mwisenge zimeungana na wajumbe kufanya usafi katika kata hizo ikiwa ni pamoja na maeneo ya Stend Kuu ya mabasi(Bweri),Soko kuu Mjini,mwalo wa Mwigobero na kwenye Zahanati.

Amesema,Chama cha Mapinduzi kina mvuto wa peke yake na  kwamba wamekuwa wakipokea wanachama wapya hasa kwa jumuiya hiyo na kwamba wamejizatiti kikamilifu katika kuhakikisha Chama kinaendelea kushika dola kuanzia mwakani kwa upande wa chaguzi za Serikali za Mitaa na 2015.
Uchaguzi Mkuu.

Kilele cha maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi kitaifa kitafanyika katika Mkoa wa Kigoma ambapo,Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk.Jakaya Kikwete atakuwa mgeni rasmi.