MWANZA
CHAMA
cha Mapinduzi Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza kimefanya maadhimisho ya
kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kufanya michezo mbalimbali ikiwemo
ya mbio za baiskeli yaliyosisimua wakazi
wa Jiji la Mwanza.
Mbio
hizo zilizoanzia katika ofisi za CCM Makao Makuu kuelekea Barabara ya
kenyata-Usagara zilianza majira ya mbili asuhuhi na kuleta hamasha kubwa kwa
wakazi wa Wilaya ya Nyamagana ambao kwa pamoja walikuwa wakiwashingilia huku
wakisidikizwa na gari la Katibu wa CCM Wilaya hiyo likiwa na bendera kubwa ya
Chama.
Mshindi
wa kwanza katika mbio hizo alikuwa Gegedi Maduhu (25) mwenye namba 850, Mfanyabiashara ya
bodaboda ya baiskeli na Mzaliwa wa kijiji cha Mwamoto-Ngokolo Mkoa wa Shinyanga
aliyemaliza mbio hiyo na kuwaacha wenzake kwa takribani dakika 10 na kumaliza
mbio hiyo 10:40 katika Uwanja wa Kumbukumbu wa
Nyamagana.
Mshindi
wa Pili alikuwa Paulo Mathias ( 19)
mwenye namba 831 Mkazi wa
Shamaliwa kata ya Igoma Mwanza ambaye ni Mkulima wa mpunga aliyemaliza mbio
hiyo 10:44 na Mshindi wa tatu alikuwa Kulwa Kalamo (20) mwenye namba 834
aliyemaliza kwa muda wa 10:46 na alipewa kombe na fedha taslimu Sh.300,000.
Aidha
akizungumza na Uhuru, mara baada ya
kukamilika kwa mbio hizo, Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Nyamagana,Raphael
Shillatu alisema kuwa mchezo huo ni sehemu ya kuhamasisha wananchi.
“Mchezo
huu ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi kupitia michezo
ili kuleta hamasha kwa vijana kwani
michezo ni ajira, pia huleta Mshikamano, Umoja, Upendo, Utulivu na Amani
na kukiwezesha chama kuwa na timu itakayofanya kazi pamoja na kuhakikisha
ushindi kuanzia chaguzi za Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu 2015”Alisema
Shillatu.
Aliongeza
kuwa mkakati huo ni ahadi yake wakati akiwa
anagombea Kiti hicho kuwa atahakikisha anaimarisha michezo yote ifikapo
maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama ikiwa ni pamoja na riadha ya Baiskeli, mpura
wa Miguu kwa wanaume ,bao,na baadae kuanzisha michezo mbalimbali kwa wanawake
ambao nduyo wenye hamasha kubwa hadi
ukomo wa Uongozi wake ikiwa ni Utekelezaji wa Ilani kwa vitendo.
Aidha
washindi hao walipewa vitita vya fedha zilizokuwa zimefugwa kwenye bahasha
ambapo hata hivyo hazikutangazwa kwa
ajili ya usalama wao na kupewa bendera za CCM na mlingoti wake kupeperusha
bendera hizo maeneo ya makazi yao.
No comments:
Post a Comment