TARIME.
VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA) Wilayani Tarime wameshindwa kuafikiana katika kikao cha kamati tendaji kilichofanyika juzi kupata mwafaka uliosababisha kufugwa kwa ofisi. Wanamtaka Mwenyekiti wa Chama Taifa Freeman Mbowe kuwashuruhisha.
Mjumbe mmoja alisema kuwa kwa sasa kunampasuko mkubwa ndani ya chama
cha Chadema ambapo tayari kuna makundi mawili yanayodaiwa kuwa kundi moja ni la Mwenyekiti wa Vijana Taifa John Heche na kundi la George Waitara ambao wanadaiwa kuwa wapo mbioni na kwamba wanajipanga kugombea 2015
Katibu Mwenezi wa Chama cha Chadema Wilaya Marwa Maruri alikiri kwa
baadhi ya viongozi kuondoka wakati kikao kinaendelea. Baadhi ya wanachama Mjini Tarime walisema kuwa sababu ya kufungwa kwa ofisi kwa muda wa siku 3 imekuja baada ya Kaimu Mwenyekiti wa Chadema Wilaya Lucas Ngoto kusimamishwa uongozi na kamati Tendaji jambo ambalo alikuafikiwa na baadhi ya wananchama na kuibua mgogoro mkubwa ambao umewafanya baadhi yao kugawanyika makundi. |
Saturday, February 23, 2013
MPASUKO CHADEMA TARIME.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment