Saturday, February 23, 2013

MPASUKO CHADEMA TARIME.




 TARIME.


VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo( CHADEMA)  Wilayani
Tarime  wameshindwa kuafikiana  katika kikao cha kamati tendaji
kilichofanyika juzi kupata mwafaka uliosababisha kufugwa kwa ofisi.

Wanamtaka Mwenyekiti  wa Chama Taifa Freeman Mbowe kuwashuruhisha. 
 
Mjumbe mmoja alisema kuwa kwa sasa kunampasuko mkubwa ndani ya chama
cha Chadema ambapo tayari kuna makundi mawili yanayodaiwa kuwa kundi
moja ni la Mwenyekiti wa Vijana Taifa John Heche  na kundi la George
Waitara ambao wanadaiwa   kuwa wapo mbioni na kwamba wanajipanga kugombea 2015
 
Katibu Mwenezi wa Chama cha Chadema Wilaya Marwa Maruri  alikiri kwa
baadhi ya viongozi  kuondoka  wakati kikao kinaendelea.
 
Baadhi ya wanachama  Mjini Tarime walisema kuwa  sababu ya kufungwa
kwa ofisi kwa muda wa siku 3 imekuja baada ya Kaimu Mwenyekiti wa
Chadema Wilaya Lucas Ngoto kusimamishwa  uongozi na kamati Tendaji
jambo ambalo  alikuafikiwa na baadhi ya wananchama na kuibua mgogoro
mkubwa ambao umewafanya baadhi yao kugawanyika makundi.



No comments:

Post a Comment