Saturday, March 2, 2013

UJIO WA MAKAMU WA RAIS, UWANJA WA NDEGE WASAFISHWA.

MUSOMA.

 UWANJA Ndege wa Musoma,wafanyiwa usafi leo asubuhi hadi mchana kwa ajili ya maandalizi ya maandalizi ya ujio wa Makamu wa Rais, Dk.Mohammed Gharibu Bilal,anayetarajiwa kuwasili kesho Mjini hapa kuzindua rasmi usafiri wa feri itokayo Musoma kwenda Wilaya ya Rorya, kivuko hicho kina utata wa jina aidah kiitwe Mv. Musoma ana Kinesi ama Rorya.

Makamu pia atazindua barabara ya Sirari.

Awali uwanja huo ulikuwa kichaka, lakini kwa sasa una mwonekano mzuri,ambapo hata hivyo kampuni ya ndege ya Auric Air inafanya safari zake, mara nne kwa wiki kutoka Musoma-Mwanza-Musoma kwa nauli ya Sh.70,000,ikiunganisha na ndege zingine kutoka Mwanza kwenda bongo, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment