Monday, March 4, 2013

MAGUFULI AWAPONGEZA CHADEMA KUTEKELEZA ILANI



MUSOMA.


WAZIRI wa Ujenzi Barabara na Viwanja vya Ndege,Dk.John Magufuli amekipongeza Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kwa kutekeleza Ilani ya CCM.

Aliyasema hayo jana wakati  akimkaribisha Makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilal wakati wa  kuzindua ukarabati wa barabara  ya Nyanguge-Musoma inayopakana na mpaka wa Mikoa ya Simiyu na Mara,sherehe zilizofanyika katika kijiji cha Mmazami, Wilaya ya Butiama.

Alisema kuwa ushiriki wa Meya wa Manispaa ya Musoma (CHADEMA), Alex Kisurura  unaonyesha dhahiri kuwa anatekeza vyema ilani ya Chama cha Mapinduzi, na kusimamia vyema ujenzi wa barabara za Manispaa kwa fedha ambayo ni ya Serikali inayoongozwa na CCM.

“Serikali hii inaongozwa na Chama cha Mapinduzi,haina ubaguzi wowote,kwani  imetoa fedha jumla y a sh. Milioni 496 za ujenzi wa barabara zake na kati ya hizo  tayari wamepewa sh. Milioni 341 inaonyesha Meya huyu, Alex Kisurura  ana mwili wa CHADEMA lakini  moyo ni wa CCM tumpongeza”alisema magufuli huku akishangiliwa na wananchi.

Aliongeza kuwa “Tunawajengea barabara,km 2 kwa watembea kwa miguu na pikipiki upande wa kulia na kushoto,kama wanataka kuandamana waandamane sana ila waachie nafasi za magari kupita huku wakijua kuwa barabara hiyo imejengwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi”alisema Magufuli.

Alisema katika kuhakikisha mtandao wa barabara za lami  zinajengwa na kwamba  fedha nyingi zimetolewa katika Wilaya za Mkoa wa Mara, ambapo alitoa pongezi kwa  Serikali  ya awamu ya nne kwa jitihada zake katika kuhakikisha Mkoa wa Mara unapata maendeleo.

Wilaya zilizotengewa  fedha  ni pamoja na Serengeti Sh. Milioni 57.6, Musoma Milioni 496,Bunda Sh. Milioni 975,Butiama Sh. Milioni 334,halmashauri ya Wilaya ya Musoma Sh. Milioni 519 ,Wilaya ya Rorya Sh. Milioni 977 na Wilaya ya Tarime Sh. Milioni 854.

Aidha amelitaka Shirika la Umeme Tanesco kutoa kibanda chake ili kupisha upanuzi wa barabara ambapo hawatalipwa fidia yoyote.

Makamu wa Rais yuko ziarani Mkoa wa Mara,ambapo leo atafanya uzinduzi kivuko cha Mv.Musoma kinachofanya safari zake kutoka Musoma kwenda Kinesi Wilaya ya Rorya ambacho pia nia hadi za Rais Jakaya Kikwete kuleta kivuko kipya ili kupunguza hadha kwa wananchi.

Pia amekutana na viongozi wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Mara katika ukumbi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa.

No comments:

Post a Comment